Dr Kashiki.200 itampendeza
Hahhahaha umetisha mkuuMwanamke Mrembo asie na busara ni sawa na Pete ya Dhahabu kuivisha kwenye Pua ya Nguruwe..,
Kweli mkuuMabingwa wa kushauri wanawake masuala ya mahusiano uwa ni wale walioshindwa ya kwao hasa ndoa zao zilivunjika.
Chunguza utaona
Matunzo ya mil 5 kwa mwezi, huyo ni Mtoto au faru Abdul?huyo mama mwenye mtoto asinyanyaswe kisa anapambana na mtu mwenye uwezo wa kifedha.
fedha za matunzo ya mtoto anazo zidai ni haki na nilazima atalipwa tu sio hiari, watetezi wa haki za wanawake huu ndio wakati wa kusema na kutetea unyanyasaji na udhalalishaji wa wanawake.
Mvua zinanyesha sana huenda anakimbia jembeAcha umbea Baki huko huko mkoani mvua zinakaribia kuanza ulime utapata tuu hizo taarifa kupitia huku huku jf
Hahahaha Da Mange nadhani anakulaga majani maana akili zake anazijuaga mwenyeweHuyo da mange bana ishu za watu anajifanya yupo nazo deep, nilicheka anavomwambia hamisa eti akusanye documents za show za diamond, akusanye documents za kipato , ushahidi wa bank apeleke mahakamani .
Wakati yeye mzungu alivoenda mahakamani kupunguza child support kalikua kadogo kalihaha kanauliza huko instagram guys nifanye nini ili nitengeneze kipato mzungu kasema child support ni kubwa nami natakiwa nichangie, ndo kakapata idea ya kufungua app yake ambayo sijui kama bado ipo.
Sasa nae kwanini asingekusanya documents za mzungu apeleke mahakamani adai hela ndefu kwa mzungu, ila ndo kwanza ikapunguzwa da mange ni fyatu
Eti documents, mtu kapigwa pmb years kwa kificho hizo documents anajua hata zilipo teh vichekesho vya da mangeHahahaha Da Mange nadhani anakulaga majani maana akili zake anazijuaga mwenyewe
Yy alishindwa halafu anamshauri mwenzake khaaaa
Kama sio wendawazimu n nn basi
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] kwelii!Hahahaa gene umenikatia stimu za usingizi hahaha.
hahhahahahaha eti Faru Abdul...Matunzo ya mil 5 kwa mwezi, huyo ni Mtoto au faru Abdul?
Tarehe 14 NovembaYa Lulu lini, tukumbushane! Nataka kuja huko DSM kuiskiliza
Huyo Malaya alitaka mtoto alipwe pesa ya kuushinda mshahara wa DC....!!!Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Leo Novemba 10, 2017 inatarajia kutoa uamuzi dhidi ya kesi ya matunzo ya mtoto iliyofunguliwa na mwanamitindo Hamisa Mobeto dhidi ya msanii maarufu nchini, Nassib Abdul au Diamond Platinum.
Uamuzi huo unatarajiwa kutolewa na Hakimu Mkazi, Devotha Kisoka upande wa Watoto. Hatua hiyo imekuja baada ya Mahakama kusikiliza hoja za pande zote husika kutokana na.msanii Diamond kuwasilisha pingamizi kupinga kesi hiyo kwa madai kuwa kesi hiyo imefunguliwa kwa kutumia kifungu ambacho si sahihi.
Mwezi uliopita, Mwanamitindo Hamisa alifungua kesi hiyo mahakamani hapo akiiomba mambo mbalimbali likiwemo la matunzo ya mtoto waliozaa na msanii huyo. Katika kesi hiyo, Hamisa alifungua kesi hiyo kupitia mawakili wake Abdullah Lyana na Walter Godluck kutoka kampuni ya uwakili ya Century Attorneys ambapo anaiomba mahakama imwamuru Diamond kutoa matunzo ya mtoto ya kila mwezi.
Kupitia hati hiyo ya madai, mwanamitindo huyo anaomba Diamond amuombe msamaha kwa kumsababishia madhara yaliyoishtua familia yake. Hata hivyo, Diamond aliwasilisha hati ya majibu kinzani akipinga maombi hayo ya Diamond akidai gharama anazodai kulipwa kwa mwezi sh. milioni tano kwa ajili ya matunzo ya mtoto ni kubwa hawezi kuzimudu
============================
UPDATES
Mwanamitindo Hamisa Mobeto amekwaa kisiki mbele ya Diamond Platnumz baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu upande wa Watoto kutupilia mbali kesi aliyofunguliwa mwanamuziki huyo juu ya matunzo ya mtoto Prince Abdul.
Uamuzi huo umetolewa leo Ijumaa Novemba 10 ,2017 na Hakimu Devotha Kisoka wa Mahakama hiyo baada ya kusikiliza hoja za pande hizo mbili husika.
Diamond aliwasilisha pingamizi dhidi ya kesi hiyo iliyofunguliwa na Mobeto akidai kuwa kesi hiyo imefunguliwa kwa kutumia kifungu ambacho si sahihi. Hoja ambayo ilipingwa na Mobeto.
Mobeto alifungua kesi hiyo mahakamani hapo, pamoja na mambo mengine anaiomba matunzo ya mtoto waliozaa na msanii Diamond.
Mobeto anaiomba mahakama imwamuru Diamond kutoa matunzo ya mtoto ya kila mwezi na alifungua kesi hiyo kupitia mawakili wake Abdullah Lyana na Walter Godluck kutoka kampuni ya uwakili ya Century Attorneys. Kupitia hati hiyo ya madai, Mobeto anaomba Diamond amuombe msamaha kwa kumsababishia madhara yaliyoishtua familia yake.
Diamond aliwasilisha hati ya majibu hayo kinzani akipinga maombi hayo ya Mobeto akidai gharama anazodai kulipwa kwa mwezi ya Sh 5 milioni kwa ajili ya matunzo ya mtoto ni kubwa hawezi kuzimudu.
Chanzo; Mwananchi
Anachekesha huyo atafute tu mtu mwingine wa kumpa mimba kwa diamond mambo hayaelewekihahhahahahaha eti Faru Abdul...
Wamerudisha tena shauri mahakamani baada ya kufanya marekebisho...
Hamisa ana danganywa kuwa mahamakama inaweza kukubali alipwe hiyo 5M...hahahaha
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Leo Novemba 10, 2017 inatarajia kutoa uamuzi dhidi ya kesi ya matunzo ya mtoto iliyofunguliwa na mwanamitindo Hamisa Mobeto dhidi ya msanii maarufu nchini, Nassib Abdul au Diamond Platinum.
Uamuzi huo unatarajiwa kutolewa na Hakimu Mkazi, Devotha Kisoka upande wa Watoto. Hatua hiyo imekuja baada ya Mahakama kusikiliza hoja za pande zote husika kutokana na.msanii Diamond kuwasilisha pingamizi kupinga kesi hiyo kwa madai kuwa kesi hiyo imefunguliwa kwa kutumia kifungu ambacho si sahihi.
Mwezi uliopita, Mwanamitindo Hamisa alifungua kesi hiyo mahakamani hapo akiiomba mambo mbalimbali likiwemo la matunzo ya mtoto waliozaa na msanii huyo. Katika kesi hiyo, Hamisa alifungua kesi hiyo kupitia mawakili wake Abdullah Lyana na Walter Godluck kutoka kampuni ya uwakili ya Century Attorneys ambapo anaiomba mahakama imwamuru Diamond kutoa matunzo ya mtoto ya kila mwezi.
Kupitia hati hiyo ya madai, mwanamitindo huyo anaomba Diamond amuombe msamaha kwa kumsababishia madhara yaliyoishtua familia yake. Hata hivyo, Diamond aliwasilisha hati ya majibu kinzani akipinga maombi hayo ya Diamond akidai gharama anazodai kulipwa kwa mwezi sh. milioni tano kwa ajili ya matunzo ya mtoto ni kubwa hawezi kuzimudu
============================
UPDATES
Mwanamitindo Hamisa Mobeto amekwaa kisiki mbele ya Diamond Platnumz baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu upande wa Watoto kutupilia mbali kesi aliyofunguliwa mwanamuziki huyo juu ya matunzo ya mtoto Prince Abdul.
Uamuzi huo umetolewa leo Ijumaa Novemba 10 ,2017 na Hakimu Devotha Kisoka wa Mahakama hiyo baada ya kusikiliza hoja za pande hizo mbili husika.
Diamond aliwasilisha pingamizi dhidi ya kesi hiyo iliyofunguliwa na Mobeto akidai kuwa kesi hiyo imefunguliwa kwa kutumia kifungu ambacho si sahihi. Hoja ambayo ilipingwa na Mobeto.
Mobeto alifungua kesi hiyo mahakamani hapo, pamoja na mambo mengine anaiomba matunzo ya mtoto waliozaa na msanii Diamond.
Mobeto anaiomba mahakama imwamuru Diamond kutoa matunzo ya mtoto ya kila mwezi na alifungua kesi hiyo kupitia mawakili wake Abdullah Lyana na Walter Godluck kutoka kampuni ya uwakili ya Century Attorneys. Kupitia hati hiyo ya madai, Mobeto anaomba Diamond amuombe msamaha kwa kumsababishia madhara yaliyoishtua familia yake.
Diamond aliwasilisha hati ya majibu hayo kinzani akipinga maombi hayo ya Mobeto akidai gharama anazodai kulipwa kwa mwezi ya Sh 5 milioni kwa ajili ya matunzo ya mtoto ni kubwa hawezi kuzimudu.
Chanzo; Mwananchi