Mtu anaweza dhani kuwa maneno deadline na addiction hayana visawe vyake katika lugha ya kiswahili. Unaweza kuta mtu anasema "...hivi deadline ni lini...?" au "....jamaa kesha addict kwenye mapenzi/dawa za kulevya. kumbe angeweza sema hivi ".....hivi makataa ni lini?" au "....jamaa kesha kuwa mraibu wa mapenzi/dawa za kulevya.
Tujifunze kiswahili kina maneno mengi sana ambayo watu hawataki kuyatumia!