Kiswahili kuchaguliwa kama Lugha ya Taifa ilikuwa kosa?

Kiswahili kuchaguliwa kama Lugha ya Taifa ilikuwa kosa?

Yaani hapa bongo bhana tuna vipaji vingi sana tena watu wa maana umewahi kufikiria kwanini hatuvumi sana kimataifa na dunia kiujumla.Hii ni kwasababu ya lungha tunayotumia kama Lungha ya taifa umewahi kufikiria labda ENGLISH ingekuwa ndo lugha yetu ya taifa yaani Kwanza tungekuwa na lafuzi nzuri ya kiingereza kuliko mataifa mengi ya kiafrika yanayozungunza English,tena kungekuwa na fursa nyingi kuliko sasa kama umewahi kuchunguza mataifa mengi wanayozungumza kiingereza wazungu huwa Wana antention nayo kuliko Yale yasiyo zungumza lugha hiyo lakin pia hata Yale mataifa yasiyozungumza kiingereza yanapokuja kwenye taifa letu bado unakuta wanaongea kiingereza tena utazani ni waingereza.Tunamsifia mwalimu Kwa kuliungalinisha ili taifa Kwa luga moja lakin Mimi nasema ilikuwa ni Kwa maslahi yake binafsi kwanini hakutumia kiingereza kutuunganisha ,je umewahi kufikiria kwanini wananchi wa taifa hili ni washamba alafu wanauelewa mdogo wa mambo ukiachillia mbali wale waliosoma soma kidogo ni kwasababu hata sources nyingi zinazofungua uelewa wa watu bado zimeandikwa Kwa kiingereza.MI NA HITIMISHA KWA KUSEMA ILIKUWA MISTAKE KUBWA MNO.
Kwanza kabisa naomba tutofautishe Lugha na Maarifa! Maarifa unayaweza kuyapata kupitia lugha yoyote na haimaanishi kuwa kujua Kiingereza basi ndiyo kuwa na maarifa.

1. Africa tumekosa Elimu sahihi ya sayansi:- Nasema hivi kwanini? Lengo kwa kwenda shule ni kupata maarifa ili uje kutatua changamoto zinazoikabili jamii yako. Elimu tunayoipata mashuleni hautufanyi kuwaza kutatua changamoto zinazotukabili hivo tunajikuta tunaishia kukariri ili tujibie mitihani, tufaulu tupate ajira maofisin. Kama ukiulizwa kwanini Tanzania maskini kwa kiswahili na bado ukashindwa kujibu basi ata uulizwe kwa kiingereza bado utashindwa kujibu atakama unakijua kiingereza vizuri sana, ila ukiulizwa kwa kiswahili ukaweza kujibu ila kwa kingereza ukashindwa basi tatizo lilikuwa lugha tu sawa ukaulizwa kwa kichina au kifaransa utashindwa kujibu ila majibu unayo kwa lugha yako mama.

2. Tanzania ianze kufundisha kwa kutumia kiswahili mpaka vyuoni ila Kiingereza libaki kama somo ikiwezekana Kifaransa, Kijeruman na Kichina pia vifundishwe:- Hoja yangu inakuja kwasababu Watanzania Lugha yetu ya mama ni Kiswahili, na kiswahili ndiyo lugha yetu ya kufikiria, yaani unapokuwa unafikiria changamoto zako za kifedha kwa mfano kuwa ukiamka asubuh utaingilia wapi ili upate fedha hutumii kingereza kuwaza ila unatumia kiswahili, bas tungekuwa tuipata elimu ya siyansi na ufundi kwa kutumia kiswahili ambayo ndiyo lugha yetu mama tungewez kutatua changamoto zinazoikabiri jamii yetu.

3. Kumfundisha kwa kutumia kiingereza au kuongea kiingereza kwasana hakutotufanya tuendelee:- msingi wa hoja hii angalia bara zima la Africa, hasa kusini mwa jangwa la Sahara! Matatizo yetu yanafanana japo tunatumia lugha tofauti, kwaiyo ni vema tukajikita kuboresha mitaala ya elimu zetu ili tuweze kujididimiza katika "Uwazi mtupu" (Abstract thinking) hapa tutakuja majibu kuanzia katika jamii zetu na mpaka katika matatizo ya dunia tutashiriki kuyatatua. Inapaswa kujua kuwa kumwambia mtoto the Biology is the study of living organisms, sio kumfundisha kiingereza bali ilo ni somo la Biology tu kama vile unaweza kumfundisha somo la biology kwa kiswahili pia kuwa ni elimu ya viumbe hai.

Mwisho kabisa:- Hakina Taifa lililoendelea kwa kutumia Lugha ya kuazima.
Uingereza kabla ya kuanza kutumia kiingereza ilikuwa inatumia kifaransa, na msingi wa Elimu tuliyonayo duniani sio Uingereza ila Uarabuni na mataifa mengine kama Ugiriki etc hivo wao kwanini hawakutumia kiarabu kufundishia katika mashule yao?
 
Basi ndio maana huoni umuhimu wa lugha ya kiswahili, maana inaweza kuwa hukifahamu vema!
Bila kiswahili hata hii thread usingeweza kuiandika. Kongole kwa baba wa taifa kwa kuasisi na kuendeleza lugha tamu ya kiswahili
Mi nakuambia ivii tayari tulikuwa na lugha katika makabila yetu na tayari tulikuwa chini mifumo ya kiingereza tungetumia iyoiyo saivi mtu analazimika kujifunza kiingereza kama lugha ya tatu inaku ni mziki
 
Kidogo nizimie kwa kukosa pumzi. Jitahidi uweke vituo panapotakiwa
 
Kwanza kabisa naomba tutofautishe Lugha na Maarifa! Maarifa unayaweza kuyapata kupitia lugha yoyote na haimaanishi kuwa kujua Kiingereza basi ndiyo kuwa na maarifa.

1. Africa tumekosa Elimu sahihi ya sayansi:- Nasema hivi kwanini? Lengo kwa kwenda shule ni kupata maarifa ili uje kutatua changamoto zinazoikabili jamii yako. Elimu tunayoipata mashuleni hautufanyi kuwaza kutatua changamoto zinazotukabili hivo tunajikuta tunaishia kukariri ili tujibie mitihani, tufaulu tupate ajira maofisin. Kama ukiulizwa kwanini Tanzania maskini kwa kiswahili na bado ukashindwa kujibu basi ata uulizwe kwa kiingereza bado utashindwa kujibu atakama unakijua kiingereza vizuri sana, ila ukiulizwa kwa kiswahili ukaweza kujibu ila kwa kingereza ukashindwa basi tatizo lilikuwa lugha tu sawa ukaulizwa kwa kichina au kifaransa utashindwa kujibu ila majibu unayo kwa lugha yako mama.

2. Tanzania ianze kufundisha kwa kutumia kiswahili mpaka vyuoni ila Kiingereza libaki kama somo ikiwezekana Kifaransa, Kijeruman na Kichina pia vifundishwe:- Hoja yangu inakuja kwasababu Watanzania Lugha yetu ya mama ni Kiswahili, na kiswahili ndiyo lugha yetu ya kufikiria, yaani unapokuwa unafikiria changamoto zako za kifedha kwa mfano kuwa ukiamka asubuh utaingilia wapi ili upate fedha hutumii kingereza kuwaza ila unatumia kiswahili, bas tungekuwa tuipata elimu ya siyansi na ufundi kwa kutumia kiswahili ambayo ndiyo lugha yetu mama tungewez kutatua changamoto zinazoikabiri jamii yetu.

3. Kumfundisha kwa kutumia kiingereza au kuongea kiingereza kwasana hakutotufanya tuendelee:- msingi wa hoja hii angalia bara zima la Africa, hasa kusini mwa jangwa la Sahara! Matatizo yetu yanafanana japo tunatumia lugha tofauti, kwaiyo ni vema tukajikita kuboresha mitaala ya elimu zetu ili tuweze kujididimiza katika "Uwazi mtupu" (Abstract thinking) hapa tutakuja majibu kuanzia katika jamii zetu na mpaka katika matatizo ya dunia tutashiriki kuyatatua. Inapaswa kujua kuwa kumwambia mtoto the Biology is the study of living organisms, sio kumfundisha kiingereza bali ilo ni somo la Biology tu kama vile unaweza kumfundisha somo la biology kwa kiswahili pia kuwa ni elimu ya viumbe hai.

Mwisho kabisa:- Hakina Taifa lililoendelea kwa kutumia Lugha ya kuazima.
Uingereza kabla ya kuanza kutumia kiingereza ilikuwa inatumia kifaransa, na msingi wa Elimu tuliyonayo duniani sio Uingereza ila Uarabuni na mataifa mengine kama Ugiriki etc hivo wao kwanini hawakutumia kiarabu kufundishia katika mashule yao?
Mi nachokizungumza we huwezi ukakielewa mpaka utakapokubali kuwa waafrika genetically tuna weakness tatizo ni kutokutambua au kukubali kuwa Sisi genetically tunavitu tumenyimwa lakin haimahanishi hatufai nasema ivo sababu waafrika hata katika michezo Tu ukiangalia tukiwa na wazungu tunafanya vizur kuliko tukiwa peke yetu siyo michezo Tu hata mwafrika aliyeko America au ulaya hawezi kuwa mwafrika aliyeko afrika penyewe hata kila mtu anafahamu waafrika wote tungepelekwa amerka then wao wakaja afrika kule ndo kungekuwa afrika alafu afrika ndo ingekuwa America kwahiyo swala la kusema tujiamini tuliweke pembeni lugha ya kiingereza kuna mahali ingetusogeza
 
Mkuu ngoja nikuambie kitu Sisi hatuwezi kujifananisha na China moja Kwa moja au ujerumani we unazani kwann Sisi bhado maskini kama wengi ukiwauliza watakuambia vita ya Tanzania na idiamini ujerumani amepigana vita ngapi tena akashindwa akafilisiwa na kufilisiwa lakin Leo nitaifa linaloongoza kiuchumi ulaya nzima kama ni ukolony hata China imewahi kuwa kolony tena la mataifa tofauti tofauti lakini ni wapili kiuchumi duniani mi nakuambia hatulingani kama mwanamke alivo halingani mwanaume hata msaada utakao mpa mwanamke siyo ndo utakao mpa mwanaume na utakaomp mwanaume na vice versa ni kweli
Nakubaliana na wewe lakini si kwa habari ya lugha.
wasomi kwa sasa ni wengi, kingereza tunaweza kuandika na kuongea, lakini wapi!
 
Mtoa mada nikiangalia uandishi wako, naishia kucheka tu. [emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Mkuu ngoja nikuambie kitu Sisi hatuwezi kujifananisha na China moja Kwa moja au ujerumani we unazani kwann Sisi bhado maskini kama wengi ukiwauliza watakuambia vita ya Tanzania na idiamini ujerumani amepigana vita ngapi tena akashindwa akafilisiwa na kufilisiwa lakin Leo nitaifa linaloongoza kiuchumi ulaya nzima kama ni ukolony hata China imewahi kuwa kolony tena la mataifa tofauti tofauti lakini ni wapili kiuchumi duniani mi nakuambia hatulingani kama mwanamke alivo halingani mwanaume hata msaada utakao mpa mwanamke siyo ndo utakao mpa mwanaume na vice versa ni kweli
Nyerere alisema:
ujinga, umaskini na maradhi ndio adui mkuu wa maendeleo.

mawazo kama hayahaya ya mleta mada yako ndani ya ujinga.

wengine husema: kuzaliwa katka familia maskini si kosa, kosa kufa maskini... Kingereza unajua, sasa basi, nenda marekani
 
sikia kuhusu kinge cha kenya
 
Mi
Nakubaliana na wewe lakini si kwa habari ya lugha.
wasomi kwa sasa ni wengi, kingereza tunaweza kuandika na kuongea, lakini wapi!
Sikiliza mkuu ni kuambie kitu English kuna mazingira inge create mi nakuambia kuna makampuni mengi na viwanda vingi vinakuja hapa nchini achilia mbali Tu mtu kutokuwa na ujuzi usika lakin kuna mambo unaeza elekezwa Tu chapu na ukapiga kazi lakin kama luga hamuelewani inakuwaje hata machine nyingi mifumo kibao unajifunza Tu you tubu apo na zipo Kwa kizungu.Tatizo za hawa wasomi wetu hawajaandaliwa kufanya manual work wao ni ofisi tu SASA Kwa level za taifa letu izo nafasi ni chache na hazibebi taifa sana kama manual work wanaojielewa
 
Mi na ushahid kibao watu wametengezewa michongo ya kazi tena Kwa mabosi ambao siyo wazungu lakini wanaongea kiingera MTU anakabiziwa Kwa bosi apo kazi ishapatika anashindwa kuongea anatemwa, alafu mtu unadiriki kusema isingetusaidia kwani Kiswahili kinatusaidia nini? Yaan nikuambie ukweli kabisa wala mtu asikudange Nyerere kutubadilishia lugha alikuwa Hana positive means yeyote ya kutusaidia ilikuwa ni mbinu yake ya kikomunist ili aweze kuwatawala wajinga WA kipindi chake ili wasielewe kinachoendelea duniani.kwani alishauriana na Nani Kwamba hii nchi iwe ya kibepari au kijamaa yote ayo yalikuwa maamuzi yake binafsi ambayo yana tuumiza mpaka leo
 
Mi utanishawishi nikuunge mkono endapo utanifafanulia nchi kama China, Japan, Korea, Ufaransa, ujerumani, Saudi, Iran, urusi n.k zimefikaje zilipo bila kutumia kingereza kama lugha ya taifa???

Walichofanya hao na wakafanikiwa bila kutumia kingereza kama lugha ya taifa ndicho tunachopaswa kukifanya.
 
Mi na ushahid kibao watu wametengezewa michongo ya kazi tena Kwa mabosi ambao siyo wazungu lakini wanaongea kiingera MTU anakabiziwa Kwa bosi apo kazi ishapatika anashindwa kuongea anatemwa, alafu mtu unadiriki kusema isingetusaidia kwani Kiswahili kinatusaidia nini? Yaan nikuambie ukweli kabisa wala mtu asikudange Nyerere kutubadilishia lugha alikuwa Hana positive means yeyote ya kutusaidia ilikuwa ni mbinu yake ya kikomunist ili aweze kuwatawala wajinga WA kipindi chake ili wasielewe kinachoendelea duniani.kwani alishauriana na Nani Kwamba hii nchi iwe ya kibepari au kijamaa yote ayo yalikuwa maamuzi yake binafsi ambayo yana tuumiza mpaka leo
We mwenyewe unijibu kwann hatujafanikiwa na tunatumia lugha yetu ,mi sikusema kuwa ndo suluisho pekee lingetutoa Ila naamini lingetusogeza maali tusingekuwa kwenye Hali mbaya kama tuliyo nayo leo
 
Nyerere mwenyewe anatengeneza wajinga alafu anakuambia muishi kijamaa maanake hurusiwi kumzidi mi nasema wasomi wanaongezeka lakin wajinga wanaongezeka xxx kwakuwa Kwanza wao wanazaa zaidi ,mjinga anazaa watoto kumi na moja Acha wa nje msomi anafata uzazi wa mpango anapeleka watoto wake shule tena nzuri mi na waambia huu mfumo wa ujamaa huu ni laana Nyerere alituachia na lugha yake unaambiwa ni identity ya taifa we unajua kisukuma kinatosha ndo identity yako hiyo then jua luga zingine za maana kama kiingereza na spenish
 
Mkuu Mpinzire hongera sana wewe una madini kichwani!

ambae hajakuelewa aende ulaya
Uyo anamaneno mengi na yanawezekana ni matamu, mi nakuambia kama unafeli shule alafu unaambiwa uko vizuri asikuambie tatizo lako liko wapi uyo anakuzika,wapo wengi waliongea kama yeye lakin bhado tuko tulipo na tunazi kuwa na Hali mbaya uhalisia unaoneka si mambo ya siasa
 
Uyo anamaneno mengi na yanawezekana ni matamu, mi nakuambia kama unafeli shule alafu unaambiwa uko vizuri asikuambie tatizo lako liko wapi uyo anakuzika,wapo wengi waliongea kama yeye lakin bhado tuko tulipo na tunazi kuwa na Hali mbaya uhalisia unaoneka si mambo ya siasa
Sujaongea maneno mengi ila nimekupa uhalisia!
Angalia hapa chini matokeo ya dalasa la saba, ao wamefail English ni wachache lakini wanaenda sekondari na huko wanaenda kuangaika kukielewa Kingereza alafu waje waelewe wanachofyndishwa kwa lugha kiingereza, mwisho wa siku ubongo unatengeneza bias unamuambia kariri tu kwanini ujitese! Anakariri ila mwisho wa siku ata hiyo Archimedes' principle aweze kuielezea nje definition.

nakuambua mimi hapa watakaofail kidato cha nne watakuwa wengi zaidi kuliko waliofaulu! Na kufail kwao watafelishwa na lugha ya Kiingereza.
20221203_082600.jpg
 
Mtoa mada umeongea point kubwa sana ingawa baadhi wanaweza kupinga ,tz kutokujua kingereza kimefanya wengi kuwa limited katika shughuli zao .ukijua lugha ya mtu mwengine hilo ndio daraja la mahusiano na ndio maana utaona Kenya, Uganda ,na mataifa mengine mengi yanayo ongea kingereza wanachangamkia fursa kama tz ingekuwa raia wake wengi wanaongea kingereza wangekuwa zaidi ya Nigeria kimziki,kiutapeli ,kimpira,kitechinojia,kibiashara ,na mengine mengi
 
Ndio maana kule Qatar hakuna mtanzania hata mmoja ni wakenya wa nigeria na ghana hizi siasa za kusema kiswahili kiwe lugha ya kufundishia wakati mikataba mingi ina lugha ya kimalkia tutakuja kulia huko mbeleni kwa kushindwa kuendana na matakwa na mabadiliko ya dunia.
 
Back
Top Bottom