Kiswahili kumbe hakieleweki hata hapo kwa jirani Malawi, tunakikuza kuliko uhalisia, ni ajabu

Kwanini viongozi wa serikali/upinzani/vigogo hawapeleki watoto wao hizi shule zenye mitaala ya Kiswahili?

maana inaonekana kumbe kiswahili ni big deal sana huko duniani mkuu.
Kwanini wananchi wa kawaida wanapeleka watoto wao shule zenye mitaala ya kiswahili?

Swali lako jibu lake ni la kiuchumi zaidi kuliko swali lililopo hapa. Lifikirie tena hilo swali.
 
Mbaya zaidi wakati wakingangania kiswahili kifundishwe hadi chuo kikuu, viongozi hao hao wanapeleka watoto wao English Medium school, na International schools,, wakati watoto wa walalahoi wapo Kayumba.
Kweli kiswahili ni kigumu jamani
 
Even apa Tabzania kuna watu hawajui kishwahil na wengi sanaa,Nchi ambazo wananchi zaid ya 50%ya population wanazungumza kishwahil ni Tz na kenya,nchi zingine uganda congo rwanda na burund uko ata 20% ya population zao haifik ya wanaokijua kishwahil
 
Malawi ,zambia na msumbiji hawajui kabisa kishwahil except baadh yavijij vya mipakan mle
Zambia nakonde tu apo hawajui kishwahil
Malawo chitipa ndo hawajui kishwahil
 
Jamaa ng'eng'e linampa shida sana kuzungumza ndio maana kwa kuficha hii aibu haendi hata ulaya au America huko kuna CNN BBC sky hayatamuacha salama,lejea yaliyomkuta Uganda ni aibu tosha,hata huko Malawi nimeona speech yake ni kama amekalilishwa hivi,yaani hata la saba nafuu. Tukubaliane tu kwamba jiwe hii lugha haiwezi.
 
Malawi ,zambia na msumbiji hawajui kabisa kishwahil except baadh yavijij vya mipakan mle
Zambia nakonde tu apo hawajui kishwahil
Malawo chitipa ndo hawajui kishwahil
Hata Pemba tu hapo wanaweza kuongea kiswahili ila mgeni ukapigwa chenge baadhi ya maneno. Canada yenyewe sio nchi nzima inakitumia Kiingereza kama lugha kuu kwa kuwasiliana
 
Malawi ,zambia na msumbiji hawajui kabisa kishwahil except baadh yavijij vya mipakan mle
Zambia nakonde tu apo hawajui kishwahil
Malawo chitipa ndo hawajui kishwahil
Pia ni Kiswahili sio kishwahil
 
Kiswahili ni lugha inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 120 Afrika mashariki na kati, tuendelee kukikuza
 
Umejifunza lugha ngapi za makabila? Wao wanazungumza lugha yao mzee, ni kama wewe ambaye unajua lugha ya kabila lako lakini kabila jirani haufahamu.
Ndio point yangu sasa, ni kuwa Kiswahili hakijaenea kana kinavyosemwa, Malawi tu hawakifahamu japo ni majirani zetu wa karibu kabisa
 
Uganda ukitaka ukimbiwe ongea kiswahili. Ukianza tu wanajua wewe mwizi. Burundi na congo ni sehemu hasa zilizokaliwa na waarabu na walipokusana watumwa wakaacha na mazalia, ndo wanaongea kiswahili. Kiswahili chao ni tofauti lakini tunaweza elewana ila kwingine ni figisu figisu za siasa tu. Museveni kakulia hapa, Wapiganaji wa msumbiji wamelelewa hapa bongo, hata huko Namibia, Angola wote wanaoongea kiswahili ni matunda ya Nyerere basi bila kusahau SA waliotoka Mazimbu, Dakawa na wale PAC wa Kongwa.
 
Nikikuonesha wamalawi wanaojua kiswahili itahalalisha mimi kudai kiswahili kimepanuka Afrika?

Makanisani utakuta mhubiri anaongea kiingereza na mkalimani anatafsiri kwa kiswahili. Ndio kusema umati wote haujui kiingereza?
Hata Wajapani wapo wanaozungumza Kiswahili, ila huwezi kusema Kiswahili kimeenea hadi Japan.

Ili kusema lugha fulani imeenea kwenye nchi fulani basi angalau 50% ya wananchi wake wawe wanaizungumza.
Kitendo cha JPM kuongea Kiswahili ila mtu wa kutafsiri akahitajika inaonyesha Malawi Kiswahili hata hawakielewi kwa kukisikia, achilia mbali kukiongea.
 
Burundi, Congo na Rwanda kiswahili kinazungumzwa kwa zaidi ya 50% hilo nina uhakika nalo.
 
Kwamba 50% ya population ya malawi ilikua iko hapo kusikiliza hotuba?

Narudia swali..

Makanisani mhubiri akiongea kwa kiingereza mkalimani akawepo na kutafsiri kwa kiswahili hiyo inamaanisha umati wote haujui kiingereza zaidi ya mhubiri na mkalimani?
 
Burundi, Congo na Rwanda kiswahili kinazungumzwa kwa zaidi ya 50% hilo nina uhakika nalo.
Huifahamu Congo wala hujawahi kuishi, Congo Kiswahi hakifahamiki kabisa, labda kama unauzungumzia DR Congo ambayo hawafiki hata 30% wanaozungumza Kiswahili.
DRC Kiswahili kinazungumzwa kwenye upande wa Mashariki tu huku tena cha kimagumashi, na Congo ni nchi kubwa sana imeenea hadi kupakana na bahari ya Atlantiki huko Kiswahili hawajawahi kukisikia kabisa
 
Kinazungumzwa Mpakani, hata msumbiji kinazungumzwa Mpakani...ndani hakipo
Yaani nchi ambazo angalau 30% ya wananchi wake wanazungumza Kiswahili ni Tanzania na Kenya tu, wengine hata 5% hawafiki japo ni majirani zetu
Kama ni hivyo basi kuna haja ya kuleta ushawishi ili lugha hii ienee
 
Sasa wewe usiwe boya, 50% ya population ikiwa inajua Kiswahili, basi hata walio kwenye mkutano kwa kuwa ni sample iliyotoka kwenye nchi hiyo hiyo, roughly 50% watakua wanajua Kiswahili, sijui kana unajua hesabu vizuri kuelewa hili

Kanisani mhubiri anaongea Kiingereza kinatafsiriwa Kiswahili sababu majority hawaelewi Kiingereza, wanaolewa English wanakuwa wachache sana ndio maana kunakuwa na mfasiri

Malawo sijasema hawajui Kiswahili wote kabisa, ila wanojua ni wachache mno kiasi kwamba mtu akiongea Kiswahili na taifa la Malawi inabidi kitafsiriwe kwa Kiingereza ndio angalau wananchi wengi wakuelewe
 
Muda huu nipo Bujumbura Burundi (Buyenzi) na nawasiliana na wenyeweji wangu na watu wengine kwa kiswahili bila wasiwasi. Kabla ya pasaka nilikuwa Uvira Congo DR, nimewasiliana na wenyeji kwa kiswahili bila wasiwasi. Tatizo lenu mnakurupuka tu kupost msiyoyafahamu!
Majirani zetu wanaozungumza kiswahili kwa ufasaha ukitoa kenya ni 1.Burundi, 2. Congo, 3.Rwanda then zinafata hizo nchi nyingine. Huko Malawi, Zambia, Mozambique na hata Uganda hakujawahi kuwa na wazungumzaji wengi wa kiswahili kwa kiwango cha kumfanya Rais au kiongozi yeyote kuwasiliana na jamii yao kwa lugha hiyo. Acheni umbumbumbu wa kupost bila research.
 
Kukua kwa kiswahili haimaanishi kiingereza sio cha muhimu na suala la wao kujua kiswahili linategemea na sera zao.. USISAHAU PIA WAMEWAHI KUWA MAADUI ZETU KISIASA... kuna utofauti mkubwa kati yetu na wao.. Wamalawi si kipimo cha kukua kiswahili..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…