okwili
JF-Expert Member
- Jan 5, 2013
- 221
- 35
Habari zenu wana Jf, nita furahi sana endapo ikitokea siku Kiswahili kikatumika katika masomo ya elimu ya juu hisopkuwa. Kwa sababu naona watu wengi Kingeleza kina wapiga chenga na kuwafanya waonekana kana kwambwa hawajui mambo,hawajiami, n.k kumbe sivyo. kuna jamaa yangu mmoja ni muhitimu wa elimu ya juu anadai kwamba hawezi kuongea kingeleza kwa muda wa saa moja. Au ndio alifundishwa kingeleza na mwalimu aliyefeli kingeleza? Na kama tunaona haito wezekana kutumia kiswahili katika masomo ya elimu juu kutokana na lugha kutokujitosheleza ni bora tukubari moja tu kutumia kingereza kwa kufundishia masomo yote hisipokuwa somo la kiswahili. Kwa mafano utakuta mwalimu anafundisha Kingeleza wakati asilimia kubwa anatumia kiswahili je hapo mwanafunzi ataelewa kipi kwa asilimia kubwa?