Gor
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 2,791
- 850
Ndugu zangu watz nimefikia uamuzi wa kuona kuwa lugha ya kiswahili ni mojawapo ya sababisho la umaskini wetu.Mwezi December nilifanya utafiti wa kupima utajiri wa kuongea lugha ya Kiswahili,Kiingereza, na Lugha ya asili ya mama yake(Native language)kati ya mwanafunzi wa std 4 wa TZ na std 4 wa Kenya.Matokeo ni kuwa Mtanzania hakuweza kuongea kwa ufasaha hizo lugha tatu,Mkenya aliweza kuongea kwa ufasaha kabisa lugha zote tatu.Katika kiswaahili Mtanzania alikuwa anaweka 'R' penye 'L' na kinyume chake pia alikuwa anatumia maneno mengi yasio fasaha,Kiingereza hakuweza kutengeneza sentensi ya kumwomba maji mama yake na hakuweza kuongea lugha ya asili yake kabisa!.Hii ilikuwa tofauti sana na Mkenya ambaye aliweza kuongea kiswahili na kiingereza kwa ufasaha mkubwa pia aliweza kuongea lugha ya mama yake ya kiluo vizuri na kiluhya.
Rasimu ya katiba ililiona hilo hivyo kuweka lugha za taifa kuwa kiswahili na kiingereza.Hii ingefanya masomo yote isipokuwa kiswahili kufundishwa kwa kiingereza na hivyo kufanya kizazi hicho cha kitanzania kuongea kiingereza kwa ufasaha wakiwa bado primary school.Kwa mujibu wa mapendekezo ya kamati za bunge la katiba;wajumbe walio wengi wameondoa kiingereza na kuacha kiswahili kitumike kama lugha rasmi ya serikali lakini wajue wanazidi kuwatenga watanzania.Kenya wamefanya kiswahili na kiingereza ziwe lugha za taifa lakini kuanzia bush school(chekechea) ni kiingereza isipokuwa soma la kiswahili.Hii inatufanya tusiweze kujiamini na kuwa "maimuna".Sasa angalieni mapendekezo hovyo za hizi kamati za BMK ya walio wengi!.
Kiingereza ndio lugha kuu ya kitaalam na kibiashara ulimwenguni hivi.Hivyo ni vizuri tufanye watu wetu waweze kuongea kiingereza kwa kufanya kiingereza kufundishwa kuanzia chekechea masomo yote isipokuwa kiswahili tu.Yes we can.
Hebu fikiria itakuwa raha namna gani sokoni,kwenye dala dala,uswahilini,kule manerumango kwa binti kinyogoli ni these,this,what,how are you?,thank you,welcome!.:flame:
Rasimu ya katiba ililiona hilo hivyo kuweka lugha za taifa kuwa kiswahili na kiingereza.Hii ingefanya masomo yote isipokuwa kiswahili kufundishwa kwa kiingereza na hivyo kufanya kizazi hicho cha kitanzania kuongea kiingereza kwa ufasaha wakiwa bado primary school.Kwa mujibu wa mapendekezo ya kamati za bunge la katiba;wajumbe walio wengi wameondoa kiingereza na kuacha kiswahili kitumike kama lugha rasmi ya serikali lakini wajue wanazidi kuwatenga watanzania.Kenya wamefanya kiswahili na kiingereza ziwe lugha za taifa lakini kuanzia bush school(chekechea) ni kiingereza isipokuwa soma la kiswahili.Hii inatufanya tusiweze kujiamini na kuwa "maimuna".Sasa angalieni mapendekezo hovyo za hizi kamati za BMK ya walio wengi!.
Kiingereza ndio lugha kuu ya kitaalam na kibiashara ulimwenguni hivi.Hivyo ni vizuri tufanye watu wetu waweze kuongea kiingereza kwa kufanya kiingereza kufundishwa kuanzia chekechea masomo yote isipokuwa kiswahili tu.Yes we can.
Hebu fikiria itakuwa raha namna gani sokoni,kwenye dala dala,uswahilini,kule manerumango kwa binti kinyogoli ni these,this,what,how are you?,thank you,welcome!.:flame: