Kitabu cha Enoch kinawataja malaika 200 walioasi ambao ndio waliiba Siri na teknolojia za mbinguni kisha wakamfundisha Binadamu

Kitabu cha Enoch kinawataja malaika 200 walioasi ambao ndio waliiba Siri na teknolojia za mbinguni kisha wakamfundisha Binadamu

Ufunuo wa Yohana 12:7-9

[7]Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;

[8]nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.

[9]Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.

Kwenye hii vita ndiyo hiyo uliyoizungumza hapo juu? kama ndio huyo joka anayezungumzwa kama shetani ni yupi ndo huyo Samael au Lucifer?
Aliye mtupa joka hakuona sehemu nyingine isipokuwa huku? Sasa binadamu ameasi kwa kutokutii maagizo. Halafu unawongezea tena joka na malaika zake ambao wanauwwzo wa kudanganya ulimwengu mzima
 
Ila binadamu jamani wanajua kutunga stori na watu kuziamini
 
Nimezunguka kwa sababu ya kujua kama unazo basic Knowledge ya Discusion ambayo tunataka kuingia....

Kwanini nimefanya hivyo??
Wengi sana hapa Jf nimekuwa Nikijenga nao hoja nilikuja kugundua mwishoni kuwa Wengi wao hawana hata ile Basic knowledge ya kitu wanachokijadili zaidi ya Knowledge ya juu...

sasa Niliamua kuwa ili niweze kuIngia kwenye Mjadala wa kisomi lazma nijue na nihakikishe mjadili mwenza anayo angalau elimu ya Msingi ya Kitu kinachojadiliwa..
sawa sijasoma vitabu vingi. Ila am curious to know which book in the bible kingetolewa and why? Hapo tu bosi.
 
sawa sijasoma vitabu vingi. Ila am curious to know which book in the bible kingetolewa and why? Hapo tu bosi.
Sijaelewa Unaposema Kipi kingetolewa but in really maybe ungeuliza Vipi vilitolewa?

So for stater Kuna Kitu kinaitwa Canonical Rules au canonical Criterion..

Hizi ni criteria zilizotungwa Na kukubaliwa kuwa Vitabu vitakavyoingizwa kwenye Biblia Viweze kufuzu Criteria hizo zipo nyingi ila unaweza ukasummerize kwa Criteria 3 tu...

  • Authentic – authentic maana Yake ni kwamba nakala hizo au Vitabu hivyo vinatakiwa kuwa halali na vya kweli na pia zilitakiwa kuwa Nakala halisi na sio Copy ya Waandishi....yaani ilitakiwa kuwa mwandishi awe ni halisia (PiGrapha)
  • Authoritative – mwandishi anatakiwa kutoa taarifa za kweli ikiwemo kuwa aliona tukio likitendeka kwa macho yake na akaliandika au Anaamini kile kilichotokea na ana mamlaka nacho..Yaani kama Daudi aandike zaburi ni yeye yaani Authentic na ni maandishi yake kabisa Authoritation au kama Daudi alikuwa na mwanafunzi wake aliyemsaidia kuandika Maandishi hayo ila ikiwa na uhakika kwamba aliyeandika alikuwepo kipindi cha Daudi na alikuwa na uhusiano na Daudi kwahyo akiandika zaburi atatumia Nafsi ya Tatu Umoja yaani Yiule daudi lakini kama akiwa si Daudi na akaandika Zaburi na akatumia Nafai ya kwanza umoja au Wingi..Inakuwa Ni kinyume cha kanuni na Inakuwa Pseudepigrapha
  • Inspired – vitabu Viwe vimeandikwa kwa Uwezo wa Roho mtakatifu..
KWa kuanzia ni kwamba Vitabu vilivyoondolewa kwenye Biblia na vitabu vilivyoachwa vyote ukivipima Vinapelea kwenye Mizani ya Canon..

So naweza kusema Vitabu vyote kwenye na vilivyoondolewa ni sawa
 
Nop kuna Vitabu vingi havikuwekwa kwenye Biblia sio kwamba Vina contradiction ila vinaendana na imani ya Kipind kile..
Kama wangekuwa bado wanachambua Biblia kuna vitabu sasa hivi vingeondolewa
Dr...
Hii post yako ilisema kama wangeendelea kuna vitabu vingetolewa hapo juu unasema ningeuliza vilibyotolewa.
Anyways, hivyo vilivyotolewa apokrifa na vinginevyo hvikuwa na mashiko kama ulivyoeleza hapo. Lakini kwa wakati wetu huu sioni kitabu Cha kutoa.
 
Dr...
Hii post yako ilisema kama wangeendelea kuna vitabu vingetolewa hapo juu unasema ningeuliza vilibyotolewa.
Anyways, hivyo vilivyotolewa apokrifa na vinginevyo hvikuwa na mashiko kama ulivyoeleza hapo. Lakini kwa wakati wetu huu sioni kitabu Cha kutoa.
Sahihi kabisa..
je Unafahamu Mpaka sasa wanatheolojia wanajadili na wanakubaliana kuwa Kitabu cha Ufunuo hakikupaswa kuwa Kitabu ndani ya Biblia??

Unafahamu kama kwa uchambuzi Wa criteria za canon za kiBiblia Kitabu cha Luka,Marko na Yohana ni miongoni mwa vitabu havikuandikwa na mtu aliyemuona Yesu wala kukaa naye na Viliandika Hadithi kama Walimuona yaani Pseudepigrapha na kuna Vitabu viliondolewa kwenye Biblia kwa sababu tu ya Kuwa Pseudepigrapha..

kWahyo kama wangekuwa wanafanya Uchambuzi bado vitabu hivyo wangeviondoa Kwenye Biblia kwakuwa havikukidhi vigezo..

Na kingine unafahamu kwamba hata vitabu vya Torati vyote Vitano "Pentateuch" They are NonAuthentitative Scriptures???

Kwanini Kwa sababu claimant wa Muandishi anayesemekana ni Musa Sio muandishi halisi..
torati pia Iliwahi kuandikwa na Ezra ambaye sio Musa?? Kipindi cha kutka Wana wa israel Babeli??

Unafahamu chochote Kuhusu Documentary Hypothesis (JEPD theory) inaprove Torati sio.Autharitative na sio Authentitative kitu ambacho hata Theology inaprove hilo..

So kwa mujibu wa those Facts Bado Biblia kama ingekuwa inafanyiwa marekebisho vingi vingeendelea Kupunguzwa
 
Ni maelezo maerefu sana maana inabidi nianze kuelezea kuhusu Races na mihula yake..

Na najua umeamwahi kusikia kuhusu Planet X au Earth X ni kama Warmhole au Kama au black hole wengi wana irelate na Nibiru na Ndiyo hasa itaimeza Dunia Through the Induced Singularity..
Ni mengi sana ya kuongea kuhusu Hii kitu sema Muda wangu ndo hautoshi maana naingia kwa Machale
Planet X au Nibiru naifahamu, pia tokana na Summerian Mythology ndio asili ya Annunaki.
Na mara ya mwisho the great deluge ilitokana na effect ya Nibiru katika dunia, kwamba inapokaribia Dunia kila baada ya miaka 3600 orbit ya dunia inashift na kusababisha maafa.
 
Planet X au Nibiru naifahamu, pia tokana na Summerian Mythology ndio asili ya Annunaki.
Na mara ya mwisho the great deluge ilitokana na effect ya Nibiru katika dunia, kwamba inapokaribia Dunia kila baada ya miaka 3600 orbit ya dunia inashift na kusababisha maafa.
Ni miaka 2000 So inategemea Mwaka 2050 au 2060..
Safi sana Mkuu Uko well Informed
 
Sahihi kabisa..
je Unafahamu Mpaka sasa wanatheolojia wanajadili na wanakubaliana kuwa Kitabu cha Ufunuo hakikupaswa kuwa Kitabu ndani ya Biblia??

Unafahamu kama kwa uchambuzi Wa criteria za canon za kiBiblia Kitabu cha Luka,Marko na Yohana ni miongoni mwa vitabu havikuandikwa na mtu aliyemuona Yesu wala kukaa naye na Viliandika Hadithi kama Walimuona yaani Pseudepigrapha na kuna Vitabu viliondolewa kwenye Biblia kwa sababu tu ya Kuwa Pseudepigrapha..

kWahyo kama wangekuwa wanafanya Uchambuzi bado vitabu hivyo wangeviondoa Kwenye Biblia kwakuwa havikukidhi vigezo..

Na kingine unafahamu kwamba hata vitabu vya Torati vyote Vitano "Pentateuch" They are NonAuthentitative Scriptures???

Kwanini Kwa sababu claimant wa Muandishi anayesemekana ni Musa Sio muandishi halisi..
torati pia Iliwahi kuandikwa na Ezra ambaye sio Musa?? Kipindi cha kutka Wana wa israel Babeli??

Unafahamu chochote Kuhusu Documentary Hypothesis (JEPD theory) inaprove Torati sio.Autharitative na sio Authentitative kitu ambacho hata Theology inaprove hilo..

So kwa mujibu wa those Facts Bado Biblia kama ingekuwa inafanyiwa marekebisho vingi vingeendelea Kupunguzwa
Uko sawa kabisaa. Lakini naona hivyo vitabu vya Luka na wengine uliowataja pamoja vimeandikwa na watu tofauti lakini vina coherence maana yake kuna uvuvio wa ROHO mtakatifu katika uandishi.
 
Hizi mambo za Ancient alien's, Sumerian Tablets, Annunak the book of Enoch, Gospel of Peter, Revelation by Peter, Gospel of Mary Magdalene, Lilith, na mambo yanayofanana na haya, usipokua makini unaacha kumuamini Mungu.
Kwa nini revelation of Peter imeondolewa kwenye Biblia?
 
KITABU CHA ENOCH KINAWATAJA MALAIKA 200 WALIOASI AMBAO NDÎO WALIIBA WALIIBA SIRI NA TEKNOLOJIA ZA MBINGUNI KISHA WAKAMFUNDISHA BINADAMU

Anaandika Robert Heriel
Mtibeli

Kwa Wakristo na waumini wa Dini ya kiyahudi jina Enock siô geni Kwao. NI Moja ya binadamu ambao hawakuwahi kupatwa na umauti.

Kwa wale wasiomjua Enoch. Kw kifupi Enoch ni Moja ya Watu WA mwanzoni katika simulizi za Zamani za kiebrania ambao NI uzao wa Nuhu.

Enoch alizaliwa na Yaredi. Enock ni Babu yake Nuhu(Nuhu NI kitukuu cha Enock)

Kwa Mujibu wa simulizi za kiebrania, enock ndiye Mtu pekee aliyeweza kukutana na MALAIKA tofauti tofauti yàani zaidi ya mmoja. Binadamu Wengine waliowahi kukutana na MALAIKA walikutana aidha na Gabriel au Mikael au Rafael

Enock ndiye Mhusika pekee aliyeweza kuwataja MALAIKA wengi zaidi Kwa majina na Sifa zào za kimaumbile.

Enoch ndiye Mhusika pekee kwèñye Biblia aliyeweza kuelezea Mianga kama Jua na Mwezi na mizunguko yake.
Enock alikuwa MTU wa kusafirishwa na MALAIKA kutoka anga Moja kuelekea ñyiñgine. Ilikuwa kawaidà Kwa Enock kupotea hata miaka 50 bila kujulikana alipo.

Enock ndiye Mhusika pekee aliyeelezea Kwa majina MALAIKA 200 Walioasi na kuzaliana na WANADAMU.

Kwa jinsi nilivyoielewa simulizi ya Enock ni Kwamba, binadamu ni kama mnyama, tofauti yake ni utashi tuu.
Binadamu Hana uwezo wowote WA kubuni kitu hata Moto, sîjui, urembo, sîjui ndege, sîjui computer, sijui bastola, miongoni mwa TEKNOLOJIA zingine.

Stori ya KITABU cha ENOCH Kwa kifupi Ipo hivi;

1. Kûna mbingu 12 na kîla mbingu kuna MALAIKA wake Mkûu anayoiongoza.

2. Malaika 200 waliasi wakiongozwa na Kiongozi wao aitwaye Samzaiya. Viongozi Wengine ni Azazel

3. Katika hao MALAIKA kîla MALAIKA alikuwa na sîfa, uwezo na Ñguvu zake. Wàpo waliokuwa na mbawa Mbili, wàpo mbawa nne(serafi) wàpo WA mbawa sita (Makerubi) na yupo Malaika mmoja aitwaye Samael mwenye mbawa Kumi na Mbili(huyu role yake ipo kitofauti)

4. Malaika hawa walikuja kuzaa na Wanawake wa WANADAMU. Wakazaa majitu, nephili au miunguwatu (demigods)

5. Azazel Moja ya Malaika alioasi aliwafundisha Wanadamu Teknolojia za silaha, uchawi, unajimu, urembo kama kupaka makeup. Kitabu kinaeleza kuwa MALAIKA walioasi wakawafundisha mambo meñgi sana àmbayo Kwa Sasa ndîo tunaita Teknolojia na utandawazi.

Jambo lililonishangaza NI kuona mpaka masuala ya Teknolojia ya kutumia Dawa Fulani ili Wanawake wasibebe mimba ili kutoharibu urembo wao. Hii ilifanya Baadhi ya Wanawake waliotumia Teknolojia ya Kuzuia mimba baadaye kushindwa kupata Watoto. Enock anaeleza hayo.

6. Demigods yàani wale machotara wa Malaika na binadamu ambao Kwa uelewa wàngu ndîo nahisi wanaitwa Majini. Wakawa wanakula kupita kiasi Jambo ambalo mama zào(Wanawake wa kibinadamu) walishindwa kuwalisha, wale Demigods wakaanza Kunywa damu za watu, kisha nyama zào, kisha wakawa wanakula ndege, wanyama na samaki wa baharini. Kipindi hicho nafikiri wanyama kama Godzilla waliishia kuliwa na hawa demigods.

Urefu wao(hao Demigods) ulikuwa Mita thelasini kwenda juu na walikuwa na uwezo mchangayiko yàani uwezo WA kibinadamu na kimalaika.

7. Wanadamu wakawa wanalia kutokana na kuuawa na hawa Watoto chotara(demigods au wanefili).
Kilio Chao kilitokana na dhulma ya uhai, kuchukuliwa Wake zào, kuteswa n.k.

8. Kilio Kikafika Mbingu ya Tano Huko alikuwepo MALAIKA Mikael, Gabriel, Rafael na Uriel. Malaika hao nao cheo chao NI kikuu. Wakaweka kikao huku wakilalamika wao Kwa wao Kwa matendo yanayofanywa na kina Samzaiya na Azazel na wenzao.

Mikael akiwa Kiongozi wa Malaika AMBAO hawakuasi akamuita Baba yao(Mungu). Mungu akawauliza kûna nini mbona kuniita. Wanasema(akina Mikael), tazama Samzaiya na Azazel wanachokifanya Huko Duniani. Wameiba Siri za MBINGUNI Ambazo Mwanadamu hakupaswa kuzijua lakini waô wamewapa. Wamewafunisha siri zetu, Kisha wakazaa nao Watoto. Ndio maana unasikia kilio Huko Duniani. Umwagaji WA damu umekuwa Mkubwa.

9. Mungu akatoa Amri akina Samzaiya na wenzake wakamatwe Kisha wafungwe katika maeneo mbalimbali mpaka Siku ya hukumu.

10. Kuhusu Demigods Mungu akawaambia atafutilia mbali Watoto na kizazi cha demigods na Wanadamu walioasi (walioungana na demigods) Kwa kutumia Gharika.

11. Basi kulikuwa na vita Kali Baina ya Malaika walioasi na MALAIKA waaminifu. Upande WA waliasi ukiongozwa na Samzaiya na Azazel huku upande WA MALAIKA waaminifu ukiongozwa na Mikael, Gabriel, Rafael na Uriel.
Mungu akamteua Malaika WA Mbingu ya Tano Aitwaye Samael kuhakikisha Haki inatendeka katika vita hiyo. Samael maana yake sumu y Mûngu, Malaika wa Kifo àmbayo majukumu yake yalikuwa mosi, kuhakikisha Haki inatendeka, pili, kushawishi na kujaribu viumbe Wengine Mpaka Malaika wènyewe,

12. Samael ndiye aliyeuweka MTU WA ujuzi WA Wema na ubaya pale Bustani ya Edeni na kumtumia nyoka kumdanganya Eva.

13. Samael ndiye aliyemtuma Ammado yàani Malaika wa ukahaba kumlaghai Adamu Kisha adamu akalala na Ammado na kuzaa naye Mtoto

14. Samael alikuja kuanguka baàda ya kumchukua Lilith kuwa Mkewe na kwenda naye kwèñye Mbingu ya Tano

15. Samael ndiye aliyepigana na Yakobo usiku ule ambao Yakobo alikuwa anaenda Kwa Labani Mjomba wake.
Samael ndiye prosecutor na ndiye aliyemletea majanga Ayoub katika kupima Haki na ukamilifu wa Ayoub

16. Ingawaje Watu wengi wanamhusisha Lucifer kuwa ndiye aliyemdanganya Eva lakini Samael ndiye aliyefanya Jambo hilo.

17. Nuhu hakuwa Mtoto WA kawaida. Jambo lililopelekea babaake Aitwaye Lameki kutaka kumkana Kwa kuona amebambikiwa, Methuselah babaye Lameki akapeleka habari hizô Kwa Enoch(Babu yake Lameki)
Nuhu tofauti na Watoto Wengine wanapozaliwa kwa Wakati huo. Alikuwa amezaliwa akiwa mweupe kupitiliza mwenye nywele kama za dhahabu. Kwa Sasa ungemuita albino. Lakini kama hiyo haitoshi, macho yake yalikuwa yakiwaka kama taa na kujuza mwanga chumbani
Jambo hilo lilimfanya Baba yake, Lameki kuona huenda Mkewe alilala na demigod au Moja ya wale Malaika walioasi.

18. Enoch ndiye aliyemwambia Methuselah Mwanaye kuwa asihofu kuhusu Mtoto wa Lameck kwani NI wake, na ndiye atakuwa mkombozi wa Wanadamu na amepewa jukumu la kujenga Safina àmbayo Watu nane tuu ndîo watakaookoka Wakati huo ûkifika. Enoch akamuita kitukuu chake hicho jina Nuhu.

19. Samael ndiye aliyemlaghai Eva na kuzaliwa Kaini.

20. Gharika ikaja kufuta na kuangamiza Watu wôte waovu na wale Demigods ingawaje wàpo ambao waliescape

21. Nuhu alipata nafasi ya kuingia na nguo ya Adamu Ile aliyovikwa na Mungu kipindi kile walichoasi.
Baàda ya gharika Hamu Mwanaye Nuhu aliiba Ile Nguo àmbayo ilikuwa na maajabu. Kisha Nimrodi Mjukuu wa Hamu naye akaiiba. Yeye akaweza kûitumia katika shughuli zake za Kúpiga upinde. Baadaye akawa Mfalme.

22. Ibrahim alizaliwa Nuhu bado akiwa hai. Nuhu alikufa Ibrahim akiwa na Miaka 55
Hivyo hadithi zote za tangu Adamu Ibrahim alizipata Kwa Babu yake, Nuhu.

Kwa Leo tuishie Hapa.

Ijumaa Kareem

Robert Heriel
Taikon WA Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam
Visa vya Anunaki hivyo.
 
Uko sawa kabisaa. Lakini naona hivyo vitabu vya Luka na wengine uliowataja pamoja vimeandikwa na watu tofauti lakini vina coherence maana yake kuna uvuvio wa ROHO mtakatifu katika uandishi.
Even a Fabricated Story can Form Coherence Mkuu...
NA ndo maana kuna kipimo maalumu cha Kupima Story kabla ya kuiamini..

Kipindi Nilipokuwa nasoma Bible Textual Analysis sanaa sana kwenye OT [Old testaments] (Textual Critiq)

Kuna maandishi mengi yana Ideas Sawa na yana maana Sawa na Ni hadithi za zamani zimeandikwa na watu tofauti ila zinakosa ubora wa Kuwa Za ukweli na Walishindwa kuyaweka kwenye Biblia Kwa sababu kwanza ni uongo pili vinakosa Analytical Truth..

ntakuandikia kimoja kama sio viwili tu..
Uthibitishwaji wa Nyakati (Nyakati inapimwa kwa Vitu Vingi kama Lugha iliyotumika Muda huo, Aina ya Uandishi, Miji ya Mda huo Na hata majina ya Miji)..

Kwa mfano..

Baba Yako alikuandikia Barua ya maelezo kabla ya yeye Kufariki mwaka 2001 akakuambia..

"Mwanangu Nimekuachia Mali nyingi sana ila mali hizo niliamua Kuzigawa katika sehemu mbali mbali Zingine zipo Mkoa wa Manyara na zingine zipo Mkoa wa Geita Mwanangu tumia Hizo mali vizuri, Kwani ni mali pekee Zenye utajiri wa Nafsi kuliko Utawala wote wa Rais Obama"

ukiisoma Kwa haraka haraka Habari hii kwa mwaka 2012 mpaka mwaka 2024 Unaweza ukaona Ni sawa na haina Shida ila kama ukituma critical Thinking and analysis utaona shida nyingi sna..

Kwanza mwaka 2001 hakukuwa na Mkoa unaitwa Manyara wala Mkoa wa Geita na wala Mwaka 2001 hakukuwa na rais anaiyeitwa Obama..

So obvious its fabticated story iliyotungwa Kwenye miaka Ya 2010 mpaka mwaka 2018 hivi..

Kwahyo ulifanya Textual analysis ya Maandiko ndani ya Biblia Yanafail kuendana na authentification na Autharitative Regulation..

Umesema Luka Ilikuwa na Uvuvio wa Roho mtakatifu, samahani kwa kusema hivi "I doubt that"..

Luka(Alikuwa ni Daktari wa Binadamu) mwenyewe anasema Ukisoma Luka 1:1-4..

Kuwa ametafuta Kwa kufanya Research na kuuliza wazee walioishi miaka hiyo na baada ya kuwauliza akaandika.. kwahyo unamaanisha Research pia Zina uvuvio??

na Elewa neno alilotumia Luka Kutunga

Kutunga Ni kubuni Jambo ambalo hapo kabla halikuwepo.. (Kama BAKITA wanavyitafsiri)
Screenshot_20240715_112717_Biblia Takatifu.jpg
 
Back
Top Bottom