Kitabu cha Mungu kinapokuwa kimbilio la wanasiasa wakati wa matatizo

Kitabu cha Mungu kinapokuwa kimbilio la wanasiasa wakati wa matatizo

MakinikiA

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2017
Posts
5,104
Reaction score
6,827
Rais Trump na kanisa
Rais Trump alikosolewa kwa kupiga picha akiwa amebeba biblia

Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionRais Trump alikosolewa kwa kupiga picha akiwa amebeba biblia

Rais Trump hana kanisa maalum analohusishwa nalo lakini uhudhuria ibada ya kanisa mara moja moja kukiwa na hafla maalum.

Amekuwa akitumia ishara na matamshi ya kidini kuwavutia wapiga kura wa Kikristo

Zaidi ya asilimia 75 ya Wainjilisti wazungu walimpigia kura Trump katika uchaguzi wa mwaka 2016, kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na kite cha Pew, ikilinganishwa na asilimia tatu tu ya Wamarekani weusi ambao ni wa dhehebu la kiprotestanti.

Kuna baadhi ya wale wanaohisi hali ya Jumatatu ya rais kuzuru kanisa la St John's ni juhudi za rais kuwavutia Wainjilisti wazungu kabla kuelekea uchaguzi mkuu.

Lakini hata wafuasi wa Rais Trump, kama vile mchungaji Burns, wanaounga mkono hatua ya kupiga picha ilikuwa ya kuimarisha msimamo wake wa kisiasa''

"Rais angesifika ikiwa angelitumia nafasi hiyo kuwaomba watu kufanya [maandamano ya amani] na kuwaambia kuwa "Niko na nyinyi, Nitaandamana pamoja na nyinyi, Naelewa kwanini mna ghadhabu."

Hata hivyo Rais Trump ametetea uamuzi weke kwenye Twitter, kwa kuandika: "Mumenielewa vibaya! Ikiwa maandamano ni ya amani, kwanini waandamanaji walichoma Kanisa usiku uliotangulia? Watu walipendezwa na hatua yangu."

Viongozi wengine wa kidini duniani wanasemaje?
Hatua ya Rais Trump kushikilia Bibilia mbele ya kanisa la St John's Episcopal limekosolewa na viongozi tofauti duniani.

Padre Antonio Spadaro, ambaye ametajwa kuwa mwandani wa karibu wa Papa Francis, aliandika katika Twitter "Wale wanaotumia Bibilia kwa maslahi yao ya kidunia nyakati za majanga wanakosea."

Kwa mujibu wa Askofu Mkuu wa Cape Town Thabo Makgoba, "Kupiga picha kwa kutumia Bibilia ni kinyume na kile kilichoandikwa ndani yake na maana ya ujumbe uliopo ndani yake, na sote tunajua hilo linamaanisha nini Afrika Kusini."

"Nilizaliwa enzi za ubaguzi wa rangi na kukulia katika mazingira hayo. Ni miaka michache iliyopita ya maisha yangu [ndio nimeishi katika mazingira ya kidemokrasia]," alisema.

Nchini Afrika kusini, dini ilitumiwa kama njia ya kuwabagua kwa misingi ya rangi enzi ya utawala wa kibaguzi.

"Inasikitisha sana wakati wanasiasa wanapotumia kanisa ama kutumia Bibilia kwa maslahi yao binafsi," Askofu huyo Mkuu aliendelea kusema.

Nchini Uingereza, Askofu wa Liverpool, Paul Bayes, aliweka kwenye Twitter picha ya Rais Trump akishikilia Bibilia na kuambatanisha na maneno:

"Hiki ni Kitabu kizuri. Akiashiria maandiko matakatifu kuhusu: 'Upendo wa Mungu .' 'Wapende maadui zako'. Nakuomba awahukumu watu wako kwa haki, Na maskini wako kwa haki. Waokoe na kuwatetea watu masikini #BlackLivesMatter '
 
Hii ni kwa St John’s tu au hata pale St. Peter’s.?
 
Back
Top Bottom