Kitabu kimpya: Mwanamke Mwanamapinduzi

Kitabu kimpya: Mwanamke Mwanamapinduzi

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
MWANAMKE MWANAMAPINDUZI

Hiki ni kitabu kinachohusu maisha ya Biubwa Amour Zahor kilichoandikwa na Zuhura Yunus.

Kitabu hiki kinahusu maisha yake Bi. Ubwa akiwa msichana mdogKio wa Kiarabu katika mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka wa 1964.

Nilipoanza kukisoma kitabu ghafla ikanijia filamu fupi niliyooana udogoni ya siku ‘’El Comandante,’’ Fidel Castro alipoingia Cuba baada ya kumuangusha Fulgencio Batista.

Pamoja na Castro ile filamu ilikuwa ikimuonyesha msichana kavaa unifomu za jeshi amebaba bunduki na kashika, ‘’megaphone,’’ anatoa matangazo akiwa juu kwenye gari lililojaa askari Wapinduzi (neno hili nimejifunza ndani ya kitabu hiki mwalimu wangu mwandishi wa kitabu Zuhura Yunus).

Kweli bint huyu kashuka kutoka Sierra Maestra na Fidel Castro na hakuna shaka ni mwanamke shujaa.

Lakini ushujaa wake haufikii hata robo ujasiri wa Biubwa.

Fikra zangu zikashuka kutoka kwa huyu bint zikenda Zanzibar katika hekaheka ya mapinduzi ndani ya kitabu hiki kuna picha ya Biubwa mwanamke pekee kisha wa Kiarabu katikati ya wanaume Wapinduzi ameshika bunduki kama vile kashika kikapu anaelekea Soko Muhogo.

Biubwa mwanachama wa ASP kashiriki katika mapinduzi ya kuiangusha serikali ya mseto wa ZNP na ZPPP.

Mapinduzi yaliyojaa umwagaji wa damu ambayo harufu ya damu ile haijapata kwisha.
Biubwa kafikaje hapa?

Lakini kitabu hiki cha maisha ya Bi. Ubwa Amour Zahor si kitabu utakishika na kukiacha.
Salama yako katika kitabu hiki ni wala usikiguse.

Ukikigusa ni sawa na ndege shorwa katua katika ulimbo.

Ndege huyu mdogo wa umbo akitua kwenye ulimbo hawezi kwamwe kujinasua mwenyewe.

Ukikigusa kitabu hiki ukakifungua na kuanza kusoma basi jua ushanasa.

Hiki si kitabu cha maskhara.

Shaaban Robert alipata kuandika kitabu, ‘’Ashiki Kitabu Hiki.’’

Mimi nakusihi na nakuambia maneno haya, ‘’Kisome kitabu hiki.’’

253193490_1056680308412680_5062274105457606070_n.jpg
 
Biubwa Amor Zahor azungumza

28 June 2016
Video: Women in Liberation Event



Embassy of Ireland in Tanzania hosted an exhibition and panel discussion on the theme of Women in Liberation Struggles. Irish academic, historian and expert on women in 1916, Mary McAuliffe, joined Tanzanian panellists to discuss the role of women in liberation in both Ireland and Tanzania.

Panellists were:
Biubwa Amour Zahor, Zanzibar political activist during the Independence period

Prof. Penina Mlama Mwalimu JK Nyerere Professorial Chair in Pan-African Studies, University of Dar es Salaam

Eda Sanga, first women journalist in Tanzania Broadcasting Corporation and Executive Director of Tanzania Media Women Association.

The discussion took place at the National Museum, Dar es Salaam, on 19th May, and was moderated by journalist and filmmaker Tulanana Bohela
Source : IrishForeignMinistry
 
Maalim wangu Mohamed Said unaweza kunipa darsa kidogo kwa nini wanamapinduzi wale wengi wao waliishia kusalitiana wenyewe kwa wenyewe na kuuana au kuwekana detainees?
 
Nimeona tu kwenye twitter, lakini tutakipata wapi sisi mashabiki wa kusoma vitabu?
 
Nimeona tu kwenye twitter, lakini tutakipata wapi sisi mashabiki wa kusoma vitabu?
Biti...

BOOKSHOP ZA TZ BARA
1.TPH BOOKSHOP LTD
2.APE NETWORK
3.MAK SOLUTIONS
4.DAR ES SALAAM BOOKSHOP.
5.A NOVEL IDEA
6.DODOMA BOOKSHOP,DODOMA
7.KASE STORES LTD, ARUSH
[02/11, 22:09] Zuhra Yunus: ZANZIBAR.
MASOMO BOOKSHOP
 
Maalim wangu Mohamed Said unaweza kunipa darsa kidogo kwa nini wanamapinduzi wale wengi wao waliishia kusalitiana wenyewe kwa wenyewe na kuuana au kuwekana detainees?
Na Mimi nasubiri majibu.

Maana historia ya Zanziba ni Kama imefanyiwa rebirth..
 
Biti...

BOOKSHOP ZA TZ BARA
1.TPH BOOKSHOP LTD
2.APE NETWORK
3.MAK SOLUTIONS
4.DAR ES SALAAM BOOKSHOP.
5.A NOVEL IDEA
6.DODOMA BOOKSHOP,DODOMA
7.KASE STORES LTD, ARUSH
[02/11, 22:09] Zuhra Yunus: ZANZIBAR.
MASOMO BOOKSHOP
Shukran Sheikh Mohammed
 
Back
Top Bottom