Kitabu kipya: Dola, Kanisa na Tatizo la Udini Tanzania

Kitabu kipya: Dola, Kanisa na Tatizo la Udini Tanzania

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074


1575131839958.png

Baada ya kifo cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (Rais wa Kwanza wa Tanganyika na pia Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) tarehe 14 Oktoba 1999 mengi yamesemwa na kuandikwa kuhusu msimamo wake na uadilifu kuhusu Uislam Tanzania.

Nia ya kitabu hiki ni kueleza jinsi Mwalimu Nyerere katika kipindi chake cha uongozi alivyoshughulikia suala la Uislam na Waislam wa Tanzania.

Hii ni historia ya uhusiano wa Mwalimu Nyerere na Waislam kwa kipindi cha takriban robo karne toka pale aliposhika madaraka ya nchi mwaka 1961 hadi alipoachia madaraka mwaka 1985.

Ni mategemeo ya mwandishi kuwa kitabu hiki kidogo kitaweka wazi yale ambayo hayafahamiki kwa wengi.

Kitabu kinapatikana Ibn Hazm Media Centre: Msikiti wa Manyema, Mtoro na Mtambani kwa bei ya Shs: Elfu Mbili.


 
Waelimishe waislamu wafanyeje ili kujikwamua hapa sasa hivi walipo, sio kuwajaza chuki kwa mambo yaliyopita ambayo hayarekebishiki, wewe ni mchochezi mkubwa wa chuki, kwa iyo unataka waislamu wabebe mapanga wawakate waliowadhulumu, kuwa na busara hata kidogo
 
Laki Si Pesa,
Laki...
Kitabu hiki kinatokana na baadhi ya sura katika kitabu cha Abdul Sykes ambacho kwa mara ya kwanza kilitoka mwaka wa 1998.

Kitabu hiki kinakwenda sasa toleo la nne katika miaka 21 ya kuwepo kwake na kinanunuliwa na kwisha na kuchapwa upya.

Hakuna Muislam aliyebeba hata wembe achilia mbali panga.

Kitabu kimerekebisha historia iliyokuwapo ya uhuru imehamasisha utafiti mpya wa kuandika historia ya uhuru wa Tanganyika.

Kazi hii inafanywa na jopo linaloongozwa na Prof. Issa Shivji na wamenihoji katika utafiti wao na nimewapa picha na baadhi ya nyaraka.

Pole sana naona umeghadhibika sana.
 
hofu ya nini, tufungue mioyo yetu na tuwe tayari kujifunza jambo jipya kila inapowezekana
Hayo siyo mafunzo mema maana hupandikiza chuki

Leo hii mnatengeneza taswira ya uislamu kudhurumiwa wakati mnayokutana nayo toka serikalini au kwenye jamii,hata dini nyingine yanakumbana nayo ila wapo kimya ifike muda mtambue inapofika muda unapofanyiwa jambo usilolipenda haimaanishi umefanyiwa sababu wewe ni muislamu lahasha

Bali unafanyiwa pasipo kuangalia wewe ni wa Imani,asili gani wala tabaka,epukeni kutengeneza nadharia za uongo,Tz bado haijawa na udini wala ukabila wa kuanza kubaguana @TudumisheUpendo #TzOneLove SISI-SOTE-NDUGU
 
Lako sio suala la chuki ndio ukweli wenyewe huo. Kwani huoni kila kukicha wanafunzi wa vyuo mbalimbali kutoka Tanzania Bara, wanajeshi na Taasisi mbalimbali huwa zinapelekwa Zanzibar kwenda kutiwa chuki za uwarabu pale mkunazini cathedral.?

Wanaelezwa kwamba wazee (bibi zao) walifagilishwa chini kwa kutumia matiti yao, hivi huyajuwi hayo au Waarabu walikuwa wakiwalawiti mababu zao. Mbona hukupiga kelele za kusomeshwa siasa za chuki. Mwache Mohammed Said atusomeshe bado angali hai maana hatutaweza kuyajuwa kama hakutuelezea.
 
Natumaini humo pia umeongelea udini mkubwa uliojitokeza ktk awamu ya 4 chini ya Jakaya Kikwete. La sivyo tuachane na masuala haya maana unafiki na kujipendelea ni kwingi sana.
 
Natumaini humo pia umeongelea udini mkubwa uliojitokeza ktk awamu ya 4 chini ya Jakaya Kikwete. La sivyo tuachane na masuala haya maana unafiki na kujipendelea ni kwingi sana.
Sooth,
Kitabu changu kinaeleza changamoto za uhuru na miaka 25 baada yake.

Ikiwa kuna dhulma kazifanya Rais Kikwete tafadhali zieleze hapa tuzifahamu.
 
Hauachi tu?
Kuna wajinga wachache wanaokuamini. Wengine wameishajua kuwa huna jipya, unapandikiza chuki tu huku ukisafiria nyota ya Nyerere. Unajifanya kumsema vibaya lakini ndiye anayefanya ngano zako zisomwe.
Nanren,
Nakuekeza kwa haki na ukweli.

Kitabu changu kimependwa kutokana na mimi kufungua Nyaraka za Sykes ambamo ndani yake zimewaleta watu katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika ambao hakuna aliyewajua.

Wewe ulikuwa unamjua Ali Mwinyi Tambwe, Iddi Faiz Mafungo na nduguye Iddi Tosiri, Bi. Tatu bint Mzee, Plantan Brothers, Erika Fiah, Sheikh Hassan bin Ameir kwa kuwataja wachache.

Sasa kwa kuunganisha historia za wazalendo hawa na Mwalimu Nyerere ndiko kulikowashangaza wengi na kukifanya kitabu changu kipendwe.
 
Bila shaka pia hako kakitabu kameelezea kwa undani sana udini uliopo visiwani ambapo Serikali yote ni Waislamu tupu, huku kukiwa hakuna Mkristo hata mmoja wakati visiwani kuna Wakristo.

Na pia, utakubali kwamba, Serikali ya Muungano inaundwa na Waislamu na Wakristo kwa hiyo haina udini kama Serikali ya visiwani.
 
Hayo siyo mafunzo mema maana hupandikiza chuki Leo hii mnatengeneza taswira ya uislamu kudhurumiwa wakati mnayokutana nayo toka serikalini au kwenye jamii,hata dini nyingine yanakumbana nayo ila wapo kimya ifike muda mtambue inapofika muda unapofanyiwa jambo usilolipenda haimaanishi umefanyiwa sababu wewe ni muislamu lahasha Bali unafanyiwa pasipo kuangalia wewe ni wa Imani,asili gani wala tabaka,epukeni kutengeneza nadharia za uongo,Tz bado haijawa na udini wala ukabila wa kuanza kubaguana @TudumisheUpendo #TzOneLove SISI-SOTE-NDUGU

Juzi nilikuwa nasikiliza hotuba za viongozi wa Kenya wakati wa kongamano la uzinduzi wa BBI wakiombea umoja wa kitaifa, na wanataka kuchukua mfano kutoka Tanzania lakini leo kuna hawa wababaishaji pumba akina Mohamed Said bado wanatafuta namna ya kugawa watanzania kwa misingi ya dini. Pumba tupu hapo.

Kama ukianza kusema waislamu walifanya hivi na wakristo walifanya hivi, ndipo unapoanza kuingia kwenye mlolongo wa wachagga walifanya hivi na wamatengo walifanya hivi hadi mwisho mnakuwa taifa la vipande vipande tena.

Anaposema Kanisa ana maana ya ukiristo, ila anasahau kuwa katika ukristo kuna madhehebu mengi sana mengine ambayo hata hayakubaliani na kabisa ni misingi ya ukatoliki wa Nyerere ambaye ndiye adui wake mkubwa.

Vile vile Tanzania kuna watu wengi ambao hawajipambanui na dini yoyote, kama hayati Kingunge na vile vile kuna dini ambazo siyo za kiislamu au za kikiristo.Mtu huyu leo hii kutuletea anachoita "kitabu kipya" cha udini ni mtu pumba kweli kweli kuliko hata nilivyokuwa naamini. Tunaingia 2020!!!
 
Kama siyo sensitization propaganda tu, hebu tuambie mapema una maana gani unaposema "kanisa" ili tusipoteze pesa zetu kununua kitabu ambacho hakina lolote la maana.
Kichuguu,
Baada ya uhuru mwaka wa 1961 mwaka wa 1962 palifanyika Muslim Congress iliyokusanya taasisi za Kiislam Tanganyika nzima na agenda ya mkusanyiko huu ilikuwa elimu.

Azimio kuu la mkutano huu ilikuwa kujenga shule na chuo kikuu ili kujikwamua na udhalili wa Waislam katika elimu uliosababishwa na ukoloni.

Kitabu kinaeleza yale yaliyotokea baada ya azimio hilo na kusababisha farka kubwa ndani ya jamii ya Kiislam iliyoishia kwa kupigwa marufuku East African Muslim Welfare Society (EAMWS) na kuundwa BAKWATA mwaka wa 1968.

Ndani ya kitabu hiki msomaji atasoma historia nzima ya nyakati zile na ataweza kuelewa kwa nini hali iko hivi hii leo.
 
Kichuguu,
Kichuguu,
Umeandika kwa ghadhabu.
Kenya tatizo lao ni ukabila.

Tanzania tatizo letu si sana katika ukabila bali dini ingawa tunajifanya hatuna tatizo hili na serikali kwa sababu za wazi inaogopa kujadili tatizo hili lakini viongozi wetu wanajua hili tatizo lipo na tunalo tokea uhuru.

Nia ya kitabu ni kuweka wazi haya ili kuwapa fursa viongozi wetu kuukabili ukweli huu na kutafuta dawa.

Umoja unapatikana pale ambapo kuna haki sawa kwa wote.

Lakini ikiwa wewe unaona mambo yote ni shwari hakuna tatizo unaweza ukaeleza fikra zako kiungwana tu bila ya kutukana.

1575194119887.png

Maandamano Waislam wanalalamika hujma katika elimu 2012
 
Mohamed Said,
Kenya tatizo siyo ukabila bali ni mgawanyiyiko wa wananchi kwa misingi ya imani fulani. Kwa kenya ulikuwa mgawanyiko wa kikabila, Rwanda ulikuwa mgawanyiko wa kiukoo, na Bosnia ulikuwa mgawanyiko wa kidini. Misingi yake yote ni ile ile unayopandikiza kwa wafuasi wako. Huu ni ubabaishaji sana wa kifikra leo hii 2020 kuambi watu kuwa umetoa kitabu kipya cha kuhubiri mgawanyiko wa kidini nchini.
 
Mohamed Said, Ukiona watu baada ya kutatua matatizo,kisayansi,wanaanza kuleta sababu,na kuhusisha dini,kabila na matatizo yaliyopo,basi ujue balaa limefika,

Kuna kipindi miaka hiyooo,Serikali baada ya kuona watoto kutoka shule za kagera wanafaulu sana kwenye mitiani,na kuchukua nafasi nyingi katika shule za serikali,iliamuliwa viwango vya kufaulu kwa mkoa was kagera vipandishwe!! Ili kudhibiti wingi wao!wala haikusaidia,wasomi nchi hii bado wanatoka kwa wingi mikoa ya Kagera,Mbeya,Kilimanjaro.

Sasa kama unatafuta kwanini mikoa ya Lindi na Mtwara,haina ufaulu wa kutosha,sabsbu sio ufaulu wa Kagera na mikoa mingine.

Nyerere hayupo tena,kuna mabaya alifsnya,je Mwinyi,Kikwete walishindwa kurekebisha!
Maana tukisema unajua sisi wa afrika,ni maskini,kwa sababu utumwa,ukoloni,na ukoloni mamboleo,umetuumiza sana,ndio maana hatuendeli kama wazungu,tutaendelea tu pale watakapo tuomba msamaha! What!!

Sasa kama ndio hivyo,Bakhresa,Mo,Dangote,Diamond,Ben Carson,Obama,walitoka wapi! Mbona wao ni wenzetu na wameendelea,?

There is no future in the past! Westage of time
 
Back
Top Bottom