Kitambulisho cha NIDA ni muhimu sana, nenda kachukue kitambulisho chako

Kitambulisho cha NIDA ni muhimu sana, nenda kachukue kitambulisho chako

RIGHT MARKER

Senior Member
Joined
Apr 30, 2018
Posts
129
Reaction score
473
📖Mhadhara (72)✍️
Ni siku nyingi sana sikutembelea ofisi ya NHIF. Lakini jana nilikwenda kwenye ofisi ya NHIF kuchukua kadi ya Bima ya afya ya mtegemezi, nikaambiwa kuwa sasahivi mambo yamebadilika. Kwa sasa mtu mzima hapewi kadi ya Bima ya afya bali atatumia NIDA (NAMBA YA NIDA) kutibiwa hospitalini.

Kwa ufafanuzi zaidi ni kwamba ukiomba Bima ya afya na ikishahidhinishwa hupewi kadi, bali ukienda hospitalini utatumia NIDA (NAMBA YA NIDA). Kadi za Bima ya afya zinatolewa kwa watoto pekee.

Hongera sana kwa ofisi ya NHIF kwa hii hatua nzuri, na idara nyingine ambazo zinafanya kwa mtindo huo kwani inamsaidia mtu kutokutembea na mzigo mkubwa wa vitambulisho kwenye pochi yake.

Kupitia uzi huu napenda kuwashauri wananchi wenzangu waende kuchukua vitambulisho vyao vya NIDA kwenye ofisi walizojiandikisha kwasababu kitambulisho cha NIDA ni muhimu sana kwenye mambo mbalimbali.

Vitambulisho vya NIDA vya Wananchi wengi vimetoka na vimepelekwa maeneo husika lakini wananchi hawaendi kuchukua vitambulisho vyao. Ukienda kwenye ofisi za maafisa watendaji wa mtaa/kata utakuta vitambulisho ni vingi sana vimekaa muda mrefu mpaka vinachakaa, nendeni mkachukue vitambulisho vyenu vya NIDA.

RIGHT MARKER,
DAR ES SALAAM.
 

Attachments

  • images (5).jpeg
    images (5).jpeg
    36 KB · Views: 5
Ni ubunifu mzuri pia. Tuwapongeze mara moja moja na kuwakosoa pia..
 
Hicho kitambulisho cha Samia ni feki?
Amezaliwa mwaka 1234 mwezi wa 56 tarehe 8 🤣🤣🤣

Hao walotengeneza hicho kitambulisho Wana kesi ya kujibu
 
Vipi kwa wageni wa nchi nyingine wakihitaji kujiunga na hiyo Bima inakuaje mkuu...?
 
Wangefanya pia kikawa kikatumika kama kadi ya benk. Yaani kwa kifupi wako integrate kwenye social services. Kingeleta maana Sana.
 
📖Mhadhara (72)✍️
Ni siku nyingi sana sikutembelea ofisi ya NHIF. Lakini jana nilikwenda kwenye ofisi ya NHIF kuchukua kadi ya Bima ya afya ya mtegemezi, nikaambiwa kuwa sasahivi mambo yamebadilika. Kwa sasa mtu mzima hapewi kadi ya Bima ya afya bali atatumia NIDA (NAMBA YA NIDA) kutibiwa hospitalini.

Kwa ufafanuzi zaidi ni kwamba ukiomba Bima ya afya na ikishahidhinishwa hupewi kadi, bali ukienda hospitalini utatumia NIDA (NAMBA YA NIDA). Kadi za Bima ya afya zinatolewa kwa watoto pekee.

Hongera sana kwa ofisi ya NHIF kwa hii hatua nzuri, na idara nyingine ambazo zinafanya kwa mtindo huo kwani inamsaidia mtu kutokutembea na mzigo mkubwa wa vitambulisho kwenye pochi yake.

Kupitia uzi huu napenda kuwashauri wananchi wenzangu waende kuchukua vitambulisho vyao vya NIDA kwenye ofisi walizojiandikisha kwasababu kitambulisho cha NIDA ni muhimu sana kwenye mambo mbalimbali.

Vitambulisho vya NIDA vya Wananchi wengi vimetoka na vimepelekwa maeneo husika lakini wananchi hawaendi kuchukua vitambulisho vyao. Ukienda kwenye ofisi za maafisa watendaji wa mtaa/kata utakuta vitambulisho ni vingi sana vimekaa muda mrefu mpaka vinachakaa, nendeni mkachukue vitambulisho vyenu vya NIDA.

RIGHT MARKER,
DAR ES SALAAM.

Ni hatua nzuri, nimeona PSSSF nao pia hawatoi tena kadi bali NIDA card tu ndiyo itatumika kwa wanachama wao wapya.

Hata hivyo kuna changamoto kwa sababu hizi kadi mpya za NIDA, hasa hizi ambazo hazina muda wa kuisha (expiry date) zinafutika maandishi mapema sana. Sasa vikiwa na matumizi mengi hivyo itabaki kadi tu bila maandishi yeyote.

Sijui NIDA wametoa kadi hizo zenye ubora duni makusudi ili zifutike mapema ili watu wakalipie kupatiwa kadi mpya?
Yaani haziko imara ukilinganisha na zile kadi za mpiga kura.
 
Kweli wametupa vitambulisho feki, changu kimeshafutika namba ndani ya miezi sita.. Waliopata mwanzo enzi za Magu ndio vilikuwa vina ubora. Bora wasingetupa sihesabu kama nna kitmbulisho.


Ni kweli kabisa zile za mwanzo kabisa ziko vizuri lakini zenyewe zilikuwa na ukomo (expiry date), baada ya muda utatakiwa ulipie upewe mpya.

Kwenye hizi NIDA cards mpya baada ya kuondoa tarehe ya ukomo (expiry date) ubora wake ni duni, yaani kadi haitumiki mara kwa mara lakini maandishi yanafutika yenyewe tu tena ndani ya miezi mitano tu ukilinganisha na kile cha mpiga kura mpaka sasa kina miaka mitano (5) lakini kiko vizuri.

Nafikiri wamefanya hivyo makusudi ili waendelee kupata hela kwa watu kuomba kadi mpya kila baada ya muda fulani.
 
Back
Top Bottom