Kitendawili cha BAKWATA na Serikali BAKWATA na Waislam 1968 - 2024

Kitendawili cha BAKWATA na Serikali BAKWATA na Waislam 1968 - 2024

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Baada ya uhuru mwaka wa 1961 palizuka hofu kubwa sana ya kuogopa Uislam na Waislam Tanganyika.

Mwaka wa 1963 ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu ya TANU Ukumbi wa Karimjee palizuka ugomvi kati ya Bibi Titi Mohamed na Julius Nyerere kuhusu EAMWS.

Haukupita muda mrefu Baraza la Wazee wa TANU chini ya Mwenyekiti Iddi Tulio likavunjwa kwa shutuma za kuchanganya dini na siasa.

Mwaka huo huo wa 1963 pakaenea uvumi kuwa serikali inataka kuivunja EAMWS.

Uvumi huu ulimalizwa na mkutano wa pili wa Muslim Congress mwaka wa 1963 chini ya EAMWS uliofanyika Aga Khan Girls School pale Bilali Rehani Waikela alipotoa risala kali kwa Mwalimu Nyerere akionya kujitokeza kwa chokochoko za chinichini dhidi ya Waislam.

Juu ya haya yote serikali iliivunja EAMWS na kuunda BAKWATA mwaka wa 1968.

Soma hapo chini historia hii ya BAKWATA na Augustino Mrema:

"Baada ya miaka mingi ya Waislam kuisusia BAKWATA ikafika mahali ikawa inashindwa hata kufanya mikutano ya uchaguzi wa viongozi kwa mujibu wa katiba yake.

Kwa hali kama hiyo ilikuwa kwa Msajili wa Vyama kuivunja BAKWATA.

Serikali ilipoona imekabiliwa na hali hiyo ikachukua jukumu la kutayarisha mkutano ili kuihuisha BAKWATA.

Tarehe 28 Aprili 1993 Waziri wa Mambo ya Ndani na Makamo Waziri Mkuu Augustine Mrema aliitisha mkutano kati ya Waislam na Wakristo katika Ukumbi wa Diamond Jubilee Hall, Dar es Salaam.

Mkutano ulikuwa hauna agenda.

Kanisa lilipeleka ujumbe wa hali ya juu kabisa.

Waislam hawakutokea isipokuwa BAKWATA.

Katika mkutano ule Mrema alieleza kuwa uchaguzi katika BAKWATA umechelewa sana kwa kukosa fedha.

Kanisa paleplale lilijitolea fedha kuipa BAKWATA ili ifanye uchaguzi wake.

Halikadhalika Mrema alisaidia kukusanya fedha kutoka kwa wafanyabiashara kwa ajili ya uchaguzi wa BAKWATA.

Mkutano ulifanyika Dodoma tarehe 10th -12th Mei.

Badala ya kufanya uchaguzi BAKWATA ilirekebisha katiba yake ili iweze kumpa ruhusa Sheikh Mkuu wa BAKWATA haki ya kufukuza na kumweka katika uongozi au kumtoa mtu yeyote bila ya kipingamizi."

(Kutoka kitabu, "Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes (1924 - 1968...").
 
KITENDAWILI CHA BAKWATA NA SERIKALI BAKWATA NA WAISLAM 1968 - 2024

Baada ya uhuru mwaka wa 1961 palizuka hofu kubwa sana ya kuogopa Uislam na Waislam Tanganyika.

Matokeo yake ndiyo hii BAKWATA.

Soma historia hii ya BAKWATA na Augustino Mrema:

"Baada ya miaka mingi ya Waislam kuisusia BAKWATA ikafika mahali ikawa inashindwa hata kufanya mikutano ya uchaguzi wa viongozi kwa mujibu wa katiba yake.

Kwa hali kama hiyo ilikuwa kwa Msajili wa Vyama kuivunja BAKWATA.

Serikali ilipoona imekabiliwa na hali hiyo ikachukua jukumu la kutayarisha mkutano ili kuihuisha BAKWATA.

Tarehe 28 Aprili 1993 Waziri wa Mambo ya Ndani na Makamo Waziri Mkuu Augustine Mrema aliitisha mkutano kati ya Waislam na Wakristo katika Ukumbi wa Diamond Jubilee Hall, Dar es Salaam.

Mkutano ulikuwa hauna agenda.

Kanisa lilipeleka ujumbe wa hali ya juu kabisa.

Waislam hawakutokea isipokuwa BAKWATA.

Katika mkutano ule Mrema alieleza kuwa uchaguzi katika BAKWATA umechelewa sana kwa kukosa fedha.

Kanisa paleplale lilijitolea fedha kuipa BAKWATA ili ifanye uchaguzi wake.

Halikadhalika Mrema alisaidia kukusanya fedha kutoka kwa wafanyabiashara kwa ajili ya uchaguzi wa BAKWATA.

Mkutano ulifanyika Dodoma tarehe 10th -12th Mei.

Badala ya kufanya uchaguzi BAKWATA ilirekebisha katiba yake ili iweze kumpa ruhusa Sheikh Mkuu wa BAKWATA haki ya kufukuza na kumweka katika uongozi au kumtoa mtu yeyote bila ya kipingamizi."

(Kutoka kitabu, "Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes (1924 - 1968...").
"Kanisa paleplale lilijitolea fedha kuipa BAKWATA ili ifanye uchaguzi wake"

......kanisa ilikua na masirahi gani katika uchaguzi wa bakwata?
 
It's time to move on Mzee wangu. Uislamu ni mkubwa kupita BAKWATA. Naamini mkiwa na mambo yenu hasa ya kimaendeleo mnayaweza kuyatekeleza vizuri bila msaada wa Serikali.

Wakatoliki walipoteza vingi sana wakati wa sera za ujamaa. Lakini wakakaa chini wameanza upya leo wako mbali tena.

BAKWATA haina uwezo wa kuwazuia Waislamu wakiamua jambo lao.
 
It's time to move on Mzee wangu. Uislamu ni mkubwa kupita BAKWATA. Naamini mkiwa na mambo yenu hasa ya kimaendeleo mnayaweza kuyatekeleza vizuri bila msaada wa Serikali.

Wakatoliki walipoteza vingi sana wakati wa sera za ujamaa. Lakini wakakaa chini wameanza upya leo wako mbali tena.

BAKWATA haina uwezo wa kuwazuia Waislamu wakiamua jambo lao.
Mag...
BAKWATA ina nguvu kubwa.

Waislam hawawezi kujenga shule bila ya BAKWATA kuridhia kwa kuieleza serikali kutoa kibali cha ujenzi.

Wakikataa basi ndiyo mwisho.

Serikali haiendi kinyume na matakwa ya BAKWATA.
 
Mag...
BAKWATA ina nguvu kubwa.

Waislam hawawezi kujenga shule bila ya BAKWATA kuridhia kwa kuieleza serikali kutoa kibali cha ujenzi.

Wakikataa basi ndiyo mwisho.

Serikali haiendi kinyume na matakwa ya BAKWATA.
Duh, Mzee Mohamed Said, ufafanuzi tafadhali: Waislamu ni nani na BAKWATA ni nani?
 
Duh, Mzee Mohamed Said, ufafanuzi tafadhali: Waislamu ni nani na BAKWATA ni nani?
Emacha,
Wote ni Waislam.

Inapokuja suala la BAKWATA inakuwa BAKWATA upande mmoja na majority Waislam upande mwingine.
 
Baada ya uhuru mwaka wa 1961 palizuka hofu kubwa sana ya kuogopa Uislam na Waislam Tanganyika.

Mwaka wa 1963 ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu ya TANU Ukumbi wa Karimjee palizuka ugomvi kati ya Bibi Titi Mohamed na Julius Nyerere kuhusu EAMWS.

Haukupita muda mrefu Baraza la Wazee wa TANU chini ya Mwenyekiti Iddi Tulio likavunjwa kwa shutuma za kuchanganya dini na siasa.

Mwaka huo huo wa 1963 pakaenea uvumi kuwa serikali inataka kuivunja EAMWS.

Uvumi huu ulimalizwa na mkutano wa pili wa Muslim Congress mwaka wa 1963 chini ya EAMWS uliofanyika Aga Khan Girls School pale Bilali Rehani Waikela alipotoa risala kali kwa Mwalimu Nyerere akionya kujitokeza kwa chokochoko za chinichini dhidi ya Waislam.

Juu ya haya yote serikali iliivunja EAMWS na kuunda BAKWATA mwaka wa 1968.

Soma hapo chini historia hii ya BAKWATA na Augustino Mrema:

"Baada ya miaka mingi ya Waislam kuisusia BAKWATA ikafika mahali ikawa inashindwa hata kufanya mikutano ya uchaguzi wa viongozi kwa mujibu wa katiba yake.

Kwa hali kama hiyo ilikuwa kwa Msajili wa Vyama kuivunja BAKWATA.

Serikali ilipoona imekabiliwa na hali hiyo ikachukua jukumu la kutayarisha mkutano ili kuihuisha BAKWATA.

Tarehe 28 Aprili 1993 Waziri wa Mambo ya Ndani na Makamo Waziri Mkuu Augustine Mrema aliitisha mkutano kati ya Waislam na Wakristo katika Ukumbi wa Diamond Jubilee Hall, Dar es Salaam.

Mkutano ulikuwa hauna agenda.

Kanisa lilipeleka ujumbe wa hali ya juu kabisa.

Waislam hawakutokea isipokuwa BAKWATA.

Katika mkutano ule Mrema alieleza kuwa uchaguzi katika BAKWATA umechelewa sana kwa kukosa fedha.

Kanisa paleplale lilijitolea fedha kuipa BAKWATA ili ifanye uchaguzi wake.

Halikadhalika Mrema alisaidia kukusanya fedha kutoka kwa wafanyabiashara kwa ajili ya uchaguzi wa BAKWATA.

Mkutano ulifanyika Dodoma tarehe 10th -12th Mei.

Badala ya kufanya uchaguzi BAKWATA ilirekebisha katiba yake ili iweze kumpa ruhusa Sheikh Mkuu wa BAKWATA haki ya kufukuza na kumweka katika uongozi au kumtoa mtu yeyote bila ya kipingamizi."

(Kutoka kitabu, "Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes (1924 - 1968...").
We udini utakuuwa..!!
 
Wewe mzee tulia na wajukuu. Unachokitaka kiwe hakitatokea. Watu wanakupuuza.
 
kila kitu kuanzia mwaka 1961 ni NYERERE na kumwogopa Sykes ...tumechoka habari zake ndo nchi imedumaa
 
Kanisa lilipeleka ujumbe wa hali ya juu kabisa.

Waislam hawakutokea isipokuwa BAKWATA.
Mzee wangu Mohamed Said nina maswali mawili kutoka ktk kipande hiki
1. unaposema KANISA unamanisha nini?
2. "Waislamu hawakurokea isipokuwa BAKWATA"
Hapa swali kwani Bakwata sio WAISLAMU?
 
Duniani kuna watu na viatu sasa kuna mtu yeye aliamua kuwa kiatu,huyo mtu kwa Tanzania hii anaabudiwa kuliko muumba wa hii dunia na viumbe wake.
 
"Kanisa paleplale lilijitolea fedha kuipa BAKWATA ili ifanye uchaguzi wake"

......kanisa ilikua na masirahi gani katika uchaguzi wa bakwata?
Hivi anaposema "kanisa" huwa anaongelea nini? Na neno lipo too general..
 
Back
Top Bottom