Kitendawili cha BAKWATA na Serikali BAKWATA na Waislam 1968 - 2024

Kitendawili cha BAKWATA na Serikali BAKWATA na Waislam 1968 - 2024

Wewe mzee tulia na wajukuu. Unachokitaka kiwe hakitatokea. Watu wanakupuuza.
Mama Samia...
Sijapata kupuuzwa katika maisha yangu.

Jumapili iliyopita nimetunukiwa tuzo hiyo hapo chini katika ukumbi wa Julius Nyerere International Conference Centre:

1731770665291.png
 
We udini utakuuwa..!!
Nga...
Kuandika na kuzungumza mambo yenye kuongeza elimu katika jamii na ulimwengu hakuui mtu.

Ingekuwa kunatoa uhai mimi ningeshakuwa marehemu miaka mingi iliyopita.

Zaidi kalamu yangu imenipa manufaa makubwa maishani.

Leo nikiweka video ya somo lolote lile ''viewers'' wanafika 80K.

Vyombo vya habari binafsi na umma vinapishana kizingitini kwangu kutaka mahojiano na mimi.

Vijana wadogo waandishi ambao ndiyo wanaanza kazi wamekuwa wapenzi wangu wakubwa na huchekeshana sana katika mahojiano.

Namuuliza ushasoma DOT Command.
Blank face.

Hajui nazungumza kitu gani.
Ananiuliza mchango wa Bibi Titi katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Jibu langu nampa swali.
''Umepata kumsoma Schneider Plantan katika historia ya uhuru?''

''Mjerumani huyu?''
Ananiuliza kwa mshangao.

''Hapana Mzulu huyu jina lake Schneider Abdillah Plantan.''
Tukimaliza ananiambia, ''Mzee Mohamed una madini sana.''

Tunacheka sote.
''Nikuoneshe picha zangu za ujana?''

Sasa vicheko vinaongozeka mpiga picha kesha maliza kazi yuko ''relaxed'' na yeye sasa anaingia katika mazungumzo anacheka.
 
Mag...
BAKWATA ina nguvu kubwa.

Waislam hawawezi kujenga shule bila ya BAKWATA kuridhia kwa kuieleza serikali kutoa kibali cha ujenzi.

Wakikataa basi ndiyo mwisho.

Serikali haiendi kinyume na matakwa ya BAKWATA.
Waislamu kwa jinsi ninavyofahamu kuna madhehebu mbalimbali, Je, hiyo BAKWATA ina nguvu katika madhehebu yote ya kiislamu?
Waislamu ambao hawaungi mkono BAKWATA, kwa nini wanashindwa kuunda taasisi yao binafsi ili kuipunguza nguvu BAKWATA ambayo wanaona hawakubaliani nayo? Wanashindwa Nini kufanya hivyo?
Mbona kwenye madhehebu ya kikristo wameweza ?
 
Tuzo ya kiislamu. Mdini mkubwa wewe.
Mama...
Umepandisha ghadhabu.

Naam ninazo sasa tuzo mfano wa hii tatu nimetunukiwa.
Halikadhalika nina tuzo mbili nimetunukiwa JF.

Una la kusema?

1731789668219.jpeg

2021

1731789759254.png

2022
1731789840700.jpeg

Mexence Melo​
 
Mzee wangu MS..
Naomba nijibu maswali yangu kwenye post #17 na #18 tafaadhali.
 
Mzee wangu Mohamed Said hicho ni kifungo cha milele,

Hakuna kiongozi ambae hatapenda kufanya kazi na Bakwata...
Wale viongozi wanapewa VIP treatment na maamuzi ya haki ya juu kabisa kuhusu Waislamu na Uislam Tanzania..

I can guarantee you will never make it..
Labda mjiunge nao .
 
Nani aliyekuwa anaogopa?! Na kwanini aogope?
Inside10,
Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa na ilm kubwa sana.
Lakini hakuwa anajibu kila swali aliloulizwa.

Akiwa hataki kujibu swali aliloulizwa alikuwa akimwambia muulizaji asome hilo somo linalomtatiza atapata jibu.

Nami jibu langu ni hilo.
Soma niandikayo kwa utulivu kila kitu kitakuwa wazi kwako.
 
Mzee wangu Mohamed Said hicho ni kifungo cha milele,

Hakuna kiongozi ambae hatapenda kufanya kazi na Bakwata...
Wale viongozi wanapewa VIP treatment na maamuzi ya haki ya juu kabisa kuhusu Waislamu na Uislam Tanzania..

I can guarantee you will never make it..
Labda mjiunge nao .
Fortilo,
Hayo usemayo hakuna binadamu anaeweza kuyajua ila Mwenyezi Mungu.
Yeye ndiye mwenye ilm ya ghaibu yaani kuyafahamu yajayo.
 
kila kitu kuanzia mwaka 1961 ni NYERERE na kumwogopa Sykes ...tumechoka habari zake ndo nchi imedumaa
Kina...
Ukichoka unajipumzisha kusoma niandikayo wala huna haja ya kujichosha zaidi kwa kuandika hapa kueleza hali uliyonayo ya uchovu.
 
Waislamu kwa jinsi ninavyofahamu kuna madhehebu mbalimbali, Je, hiyo BAKWATA ina nguvu katika madhehebu yote ya kiislamu?
Waislamu ambao hawaungi mkono BAKWATA, kwa nini wanashindwa kuunda taasisi yao binafsi ili kuipunguza nguvu BAKWATA ambayo wanaona hawakubaliani nayo? Wanashindwa Nini kufanya hivyo?
Mbona kwenye madhehebu ya kikristo wameweza ?
John...
Umeuliza swali zuri.

BAKWATA imeundwa na serikali baada ya serikali kuipiga marufuku EAMWS mwaka wa 1968.

Hakuna taasisi ya Kikristo iliyoundwa na serikali.
 
Nga...
Kuandika na kuzungumza mambo yenye kuongeza elimu katika jamii na ulimwengu hakuui mtu.

Ingekuwa kunatoa uhai mimi ningeshakuwa marehemu miaka mingi iliyopita.

Zaidi kalamu yangu imenipa manufaa makubwa maishani.

Leo nikiweka video ya somo lolote lile ''viewers'' wanafika 80K.

Vyombo vya habari binafsi na umma vinapishana kizingitini kwangu kutaka mahojiano na mimi.

Vijana wadogo waandishi ambao ndiyo wanaanza kazi wamekuwa wapenzi wangu wakubwa na huchekeshana sana katika mahojiano.

Namuuliza ushasoma DOT Command.
Blank face.

Hajui nazungumza kitu gani.
Ananiuliza mchango wa Bibi Titi katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Jibu langu nampa swali.
''Umepata kumsoma Schneider Plantan katika historia ya uhuru?''

''Mjerumani huyu?''
Ananiuliza kwa mshangao.

''Hapana Mzulu huyu jina lake Schneider Abdillah Plantan.''
Tukimaliza ananiambia, ''Mzee Mohamed una madini sana.''

Tunacheka sote.
''Nikuoneshe picha zangu za ujana?''

Sasa vicheko vinaongozeka mpiga picha kesha maliza kazi yuko ''relaxed'' na yeye sasa anaingia katika mazungumzo anacheka.
Tatizo kubwa ulilonalo, ni kwamba kila mada unayoiandika, inalenga kuonyesha yafuatayo;
1. Waislamu wanaonewa kila siku na kwenye kila jambo
2. Waislamu wapo juu kuliko wengine wote ila tu wanakandamizwa

Kitendo cha kutoona waislamu nao huwa wanakosea, waislamu wanaonewa kila siku ndo ninapopingana na wewe. Ki
 
Tatizo kubwa ulilonalo, ni kwamba kila mada unayoiandika, inalenga kuonyesha yafuatayo;
1. Waislamu wanaonewa kila siku na kwenye kila jambo
2. Waislamu wapo juu kuliko wengine wote ila tu wanakandamizwa

Kitendo cha kutoona waislamu nao huwa wanakosea, waislamu wanaonewa kila siku ndo ninapopingana na wewe. Ki
Ndugu zetu yaani hawataki kukosolewa kabisa, yaani kuna masuala mengine hata yakijadiliwa kwa akili za haraka haraka tu they make a lot of sense lakini ndio hivyo sasa; ni sawa na kupigia mbuzi guitar
 
Wala sio wewe unachosha

Huyu aitwae NYERERE
Kina...
Maktaba yangu ni kati ya maktaba tatu zilizosheheni taarifa nyingi za Julius Nyerere.

Maktaba ya kwanza ni ya Dr Salim Ahmed Salim, Mohamed Said na Brig.General Hashim Mbita.

Ndiyo sababu unaona wengi wanakuja kwangu kwa mahojiano.

Lakini mengi niliyonayo nimeyapata kutoka Nyaraka za Sykes.

Haya yapo katika kitabu cha maisha ya Julius Nyerere (Nyerere Biography).
 
Tatizo kubwa ulilonalo, ni kwamba kila mada unayoiandika, inalenga kuonyesha yafuatayo;
1. Waislamu wanaonewa kila siku na kwenye kila jambo
2. Waislamu wapo juu kuliko wengine wote ila tu wanakandamizwa

Kitendo cha kutoona waislamu nao huwa wanakosea, waislamu wanaonewa kila siku ndo ninapopingana na wewe. Ki
Nga...
Hakuna tatizo.
Endelea kupinga na mimi nitakuwa nakupa majibu.
 
Back
Top Bottom