Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
KITENDAWILI CHA PICHA YA WAASISI WA TANU 7 JULAI, 1954: "NOW YOU SEE HIM NOW YOU DONT"
Nimepokea ujumbe huo hapo chini:
Asalam Aleikum Warahmatullah Wabarkatuh,
Poleni kwa msiba, wanasema hiyo picha ya waanzilishi wa TANU imewekwa CCM kama ulivyoshauri, ni kweli, imewekwa wapi, Chamwino au Lumumba?
***
Waleikum Salaam Warahmatullah Wabarakatuh.
Tushapoa ndugu yangu.
Mwaka 1987 nilikwenda Maktaba ya CCM Dodoma wakati huo nafanya utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes.
Nilikuta picha ya Waasisi wa TANU imetundikwa.
Sina taarifa ni hii picha uliyoniletea.
Nakushukuru sana.
Lakini ningependa kukufahamisha kuwa picha hii uliyoniletea si ile picha halisi yenyewe.
Picha hii ina kasoro kubwa ya kutiwa mkono na kubandikwa ndani picha ya Kasella Bantu ambae hayumo kwenye picha iliyopigwa pale ofisi ya TAA New Street tarehe 7 Julai 1954.
Wengine ambao hawamo katika picha ya Waasisi wa TANU ni Tewa Said Tewa na Ally Sykes.
Hawa watatu walikaa pembeni kwa kuwa walikuwa watumishi wa serikali na sheria ilikuwa inawakataza kujihusisha na siasa.
Nimepokea ujumbe huo hapo chini:
Asalam Aleikum Warahmatullah Wabarkatuh,
Poleni kwa msiba, wanasema hiyo picha ya waanzilishi wa TANU imewekwa CCM kama ulivyoshauri, ni kweli, imewekwa wapi, Chamwino au Lumumba?
***
Waleikum Salaam Warahmatullah Wabarakatuh.
Tushapoa ndugu yangu.
Mwaka 1987 nilikwenda Maktaba ya CCM Dodoma wakati huo nafanya utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes.
Nilikuta picha ya Waasisi wa TANU imetundikwa.
Sina taarifa ni hii picha uliyoniletea.
Nakushukuru sana.
Lakini ningependa kukufahamisha kuwa picha hii uliyoniletea si ile picha halisi yenyewe.
Picha hii ina kasoro kubwa ya kutiwa mkono na kubandikwa ndani picha ya Kasella Bantu ambae hayumo kwenye picha iliyopigwa pale ofisi ya TAA New Street tarehe 7 Julai 1954.
Wengine ambao hawamo katika picha ya Waasisi wa TANU ni Tewa Said Tewa na Ally Sykes.
Hawa watatu walikaa pembeni kwa kuwa walikuwa watumishi wa serikali na sheria ilikuwa inawakataza kujihusisha na siasa.