Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,413
- 23,592
Nimetulia namsikiliza kwa makini Spika Tulia akiwataka vijana wanaosadikiwa ni wa CCM kuwashughulikia wanaowakosoa viongozi wa chama na serikali. Moja kwa moja nikamkumbuka kijana machachari Ben Saanane kwa jinsi alivyokuwa anahoji sifa za Rais na Mwenyekiti wa CCM, John Pombe Magufuli (RIP).
Sina hakika na kilichompata kijana huyo lakini hadi leo hajulikani yuko wapi na kama yuko hai au la. Hivyo hivyo hali kama hiyo ikawatokea wengi hadi maiti zikaanza kuokotwa kwenye viroba. Kwa mara ya kwanza katika historia ya taifa hili, kumkosoa kiongozi wa chama na serikali kukawa ni kujitafutia makuu.
Pamoja na kuwa na vyombo vya ulinzi na usalama, wananchi waliendelea kuishi kwa hofu bila maelezo ya kutosheleza. Waliopotelewa na ndugu zao walipewa majibu ya mkato kwamba wahusika hawajulikani. Basi neno wasiojulikana likawa wimbo kila akipotezwa mtu huku raia wakizidi kutekwa na kupotezwa.
Kuna wakati utaupenda ukweli na kuna wakati utauchukia ukweli. Kama ni mtenda maovu lazima utauchukia ukweli kwani kila utakapotaka kuuzikao hautakubli. Lakini kama ni mtenda wema utaupenda na kuulinda wabaya wasije wakapata nafasi ya kuuzika hata kama ni kwa muda mfupi tu kabla ya kujitokeza tena.
Nimemsikia Spika Tulia...je alichoagiza kinatoa kamwanga kadogo kwa kitendawili cha wasiojulikana? Nikitazama sura za wale vijana wanaoamrishwa kuwashughulikia wakosoaji wa viongozi wa chama na serikali napata woga. Fikiria hawa wanikute nikimkosoa Spika Tulia, je nitapona? Je ndugu zangu wataniona tena?
Sina hakika na kilichompata kijana huyo lakini hadi leo hajulikani yuko wapi na kama yuko hai au la. Hivyo hivyo hali kama hiyo ikawatokea wengi hadi maiti zikaanza kuokotwa kwenye viroba. Kwa mara ya kwanza katika historia ya taifa hili, kumkosoa kiongozi wa chama na serikali kukawa ni kujitafutia makuu.
Pamoja na kuwa na vyombo vya ulinzi na usalama, wananchi waliendelea kuishi kwa hofu bila maelezo ya kutosheleza. Waliopotelewa na ndugu zao walipewa majibu ya mkato kwamba wahusika hawajulikani. Basi neno wasiojulikana likawa wimbo kila akipotezwa mtu huku raia wakizidi kutekwa na kupotezwa.
Kuna wakati utaupenda ukweli na kuna wakati utauchukia ukweli. Kama ni mtenda maovu lazima utauchukia ukweli kwani kila utakapotaka kuuzikao hautakubli. Lakini kama ni mtenda wema utaupenda na kuulinda wabaya wasije wakapata nafasi ya kuuzika hata kama ni kwa muda mfupi tu kabla ya kujitokeza tena.
Nimemsikia Spika Tulia...je alichoagiza kinatoa kamwanga kadogo kwa kitendawili cha wasiojulikana? Nikitazama sura za wale vijana wanaoamrishwa kuwashughulikia wakosoaji wa viongozi wa chama na serikali napata woga. Fikiria hawa wanikute nikimkosoa Spika Tulia, je nitapona? Je ndugu zangu wataniona tena?