Kitendawili cha wasiojulikana hatimaye kimeteguliwa na Spika Tulia?

Kitendawili cha wasiojulikana hatimaye kimeteguliwa na Spika Tulia?

Wasio julikana ni sisi, njooni mtukamate tuka jitetee Mahakamani?? ….tumewachooka sasa!! mbona tunajisema kila siku??? au mna tatizo la msingi nyie mbwa!!..sisi tulifanya kwa sababu tulilipwa au mlitaka tufe njaa!!

Mbona nyie mnakula rushwa bakshishi za chama, sasa kwa nini sisi tusile ili kutimiza mauaji kwa wanoko! mtupe basi ajira hamtaki kwa hiyo tufe na njaa nyie mkaropoke kwenye majukwa huko siyo!!

tukipewa hela sie tuna wafyeka tu!!...kwani hamjui kuwa Maisha ni vita unazubaa na tonge mdomoni wkt na mie nalitaka mwee!! thubutuu……. mmeshindwa kutuweka nguvuni nyamazeni kimyaaa!

mkibisha tunalianzisha tena make uzoefu tunao! tumeachiwa huo urithi!! halafu tunazurura weee mitaani na magari yetu tuliyo nunuliwa wala hamtujui sijui!...….ivo mlitaka sisi tufe na njaa nyau nyie!

Mauaji ni ajira kam DRs/Nurses anavo toa mimba ni mauaji pia, mbona hamuwasemi hao kina Mama/dada wanao toa mimba zenu nyie wanaume?? tena utakuta lingine limetoa mimba weee!! mpaka kizazi kimedata halizai tena!

hilo hilo nalo ! eti lina lilia kifo cha Beni saanane! eti kaonewa mwee! hiyo ni dhihaka!...….Drs Nurses mtulie yenu tunayajua!!….limke lililo toa Mimba bila huruma kuwa nalo makini sana!...litakuumiza tu! usicheke nalo!

Mengine manaume yanatoa hela wake zao wakatoe mimba! na yenyewe yameshiriki...lkn eti mnatuona sisi tulio wakung'uta Risasi wana fiki tuna makossa...si watulie tuu! waone!

sasa mjadala huu ufungwe vinginevyo tutakuja live km majamba wazi, hapo ulipo si mbali! subiri uone sarakasi tamu! mmoja baada ya mwingine nyau kabisa!
 
Utata wa kauli ndilo tatizo kwasababu wapo wanaotafsiri ni kuua, wapo wanaosema ni kupoteza na mleta mada kasema 'wasiojulikana' wengine wana tafsiri hakuna shida

Hawa wanaosema hakuna tatizo si habari kwasababu hakuna tatizo. Tatizo ni hawa wanaotfasiri kwa mtazamo mwingine hasa ukizingatia miaka 6 iliyopita ilivyokuwa. Watu wanakumbu kumbu za akina Kenan Kihongosi na Heri james, wanakumbuka akina Sabaya , wanakumbuka viroba na maiti kutoka south Africa mto Ruvu.
TL alifuatiliwa na gari wakasema hakuna tatizo leo tunajua kilichomkuta

Ikiwa basi kauli hiyo sivyo ilivyo kwanini
CCM hawatoki na kuitetea kwamba haina tatizo wakijua imetolewa na mjumbe wa kamati kuu tena iliyokaa hivi karibuni?
Kwanini Msajili asitoke na kufafanua kama haina utata ? Je angeitoa mwana CDM leo ingaliwakuwaje?
Kwanini IGP asijitokeze na kuwahakilishia watu kuwa kauli hiyo ni safi tu haina shida

Kauli ya Spika inahamasisha vurugu nchini! Alipaswa awe amejiuzulu
Kwanza tukubaliane hao wote wenye tafsiri tofauti wana haki sawa, asitokee mmoja au kundi moja likajiona lina haki zaidi ya wengine.

Pili, unazungumzia matukio ya miaka sita iliyopita, kwamba ndio yanakupa hofu kuamini hii kauli itaturudisha zama zile, hii hofu yako na wenzako, ni haki yenu, naiheshimu.

Lakini usiitumie hofu yenu kuipandikiza kwa wengine, waache nao wabaki na mawazo yao, ukweli ni kwamba miaka sita iliyopita sio leo, kwani wakati ule alikuwepo mtawala tofauti na aliyepo sasa, na hata habari za kutekana/kuuana hazipo kwa wingi kama wakati ule.

Kusisitiza kutaka kauli ya IGP kwenye ile tungo tata naona unaenda mbali sana, kwanini kwanza usitake "clarification" toka kwa yule aliyeitoa? naamini baada ya kupata "clarification" toka kwake ndio itaonekana kama anatakiwa kujiuzulu, au vinginevyo.

Lakini tusimlazimishe mtu ajiuzulu kwasababu ya hofu yetu isiyo na uthibitisho usioacha shaka, au niseme kwasababu zetu za kihisia kutokana na ile kauli aliyoitoa.
 
Mimi nimemsikia kwa video clip akisema "Nyooka nae" hiyo ya ashughulikiwe sijaiona, kama unayo tuwekee hapa tumalize utata.

Naona mnatumia matukio yaliyopita kuhukumu yaliyopo, ndipo mnapokosea.
Hivi ngoja nikuulize swali (direct question).

Hivi wewe unaelewa nini mtu akisema maneno "Nyooka Naye", katika maudhui (context) ya sehemu yalipotamkwa maneno hayo na kuya'qualify' kuhusu viongozi wanaoshambuliwa na hao wanaotakiwa "kunyooshwa", na kundi siyo la wazee, ila vijana ambao damu zinachemka wakisikia maneno ya namna hiyo yakisemwa na kiongozi mkuu ndani ya nchi yakilenga kuwawekea kinga viongozi wenzake na yeye mwenyewe dhidi ya wanaolengwa kunyooshwa.

Wale jamaa wa Rwanda waliokuwa wakiwaita wenzao "Mende" waliolengwa kuondolewa kati binaadam, bila shaka nao ungewaona kuwa hawakuwa na tatizo lolote kabisa kuwafananisha wenzao na wadudu wasiotakiwa kuwa miongoni mwa binaadam!
 
Hivi ngoja nikuulize swali (direct question).

Hivi wewe unaelewa nini mtu akisema maneno "Nyooka Naye", katika maudhui (context) ya sehemu yalipotamkwa maneno hayo na kuya'qualify' kuhusu viongozi wanaoshambuliwa na hao wanaotakiwa "kunyooshwa", na kundi siyo la wazee, ila vijana ambao damu zinachemka wakisikia maneno ya namna hiyo yakisemwa na kiongozi mkuu ndani ya nchi yakilenga kuwawekea kinga viongozi wenzake na yeye mwenyewe dhidi ya wanaolengwa kunyooshwa.

Wale jamaa wa Rwanda waliokuwa wakiwaita wenzao "Mende" waliolengwa kuondolewa kati binaadam, bila shaka nao ungewaona kuwa hawakuwa na tatizo lolote kabisa kuwafananisha wenzao na wadudu wasiotakiwa kuwa miongoni mwa binaadam!
Maana yangu nimeshaiandika huko juu, hili suala mnalichukulia kwa hisia zaidi ya uhalisia, na wewe kuielewa maana tofauti nami ni jambo la kawaida, kwasababu lugha iliyotumika haikuwa direct, ndio maana kila mmoja anaitafsiri yake.

Huo mfano wa Rwanda uliotoa haufanani kabisa na hoja tunayoizungumzia hapa, "mende" anajulikana kwa wote ni mdudu wa aina gani, hilo sio la kubishana, usilazimishe kuingia kwenye kichwa changu, nawaona mmetawaliwa na hisia zilizochanganyika na hasira kwenye reasoning yenu, hamko neutral.
 
Maana yangu nimeshaiandika huko juu, hili suala mnalichukulia kwa hisia zaidi ya uhalisia, na wewe kuielewa maana tofauti nami ni jambo la kawaida, kwasababu lugha iliyotumika haikuwa direct, ndio maana kila mmoja anaitafsiri yake.

Huo mfano wa Rwanda uliotoa haufanani kabisa na hoja tunayoizungumzia hapa, "mende" anajulikana kwa wote ni mdudu wa aina gani, hilo sio la kubishana, usilazimishe kuingia kwenye kichwa changu, nawaona mmetawaliwa na hisia zilizochanganyika na hasira kwenye reasoning yenu, hamko neutral.
Sikiliza tena aliyosema huyo Tulia mwanzoni kabisa. Hayo ya ‘nyoosha’ ameanza kuyatumia katika sentensi zilizofuatia.
 
kwasababu lugha iliyotumika haikuwa direct, ndio maana kila mmoja anaitafsiri yake.
Mtu anakwambia:"Niakunyoosha", wakati mtu huyo unajuwa wazi kwamba unayofanya wewe ni kinyume cha maslahi yake, bado utasema maana ya maneno yake haiko 'direct', na kwamba kutakuwa na tafsiri nyingine anayodhamiria uipate!
usilazimishe kuingia kwenye kichwa changu, nawaona mmetawaliwa na hisia zilizochanganyika na hasira kwenye reasoning yenu, hamko neutral.
Ni dhahiri kabisa hapa ni nani anayelazimisha anayofikiri yeye ndiyo yawe sahihi, wakati yanayozungumziwa yana tafsiri halisi isiyo na utata.
 
Back
Top Bottom