G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,795
- 36,704
Jeshi la Polisi linafanya upuuzi kukamata viongozi na wafuasi wa vyama vya upinzani na kuacha wale wa chama tawala na mawakala wao.
Kitendo hiki kinadhihirisha jinsi vyombo vya dola vinavyotumika kwa maslahi ya kuhakikisha chama tawala kinapata kwa ukamilifu kile kinachokitaka kwa nguvu. Kwenye nchi inayojinasibu kuwa ya kidemokrasia na inayofuata mfumo wa uchaguzi huru na wa haki kuwapata viongozi wa wananchi, kufanya hivi ni upuuzi mtupu kwa vyombo vya dola. Aidha ni dalili ya ukomavu duni wa vyombo hivyo.
Huwezi kujitapa hadharani kuwa demokrasia itatamalaki kwenye uchaguzi mkuu huku mafichoni vyombo vinavyoshughulikia hayo vikionyesha udhaifu mkubwa kiutendaji na kwenye matokeo.
Tumuombe na tumpe rai Rais Magufuli kuwa haya yanayotokea yana dhamana juu ya mikono yake. Hii ni nchi yenye watu wa kada mbalimbali kisiasa. Nimkumbushe tu kuwa kilichoharibu ustawi wa nchi nyingi duniani ni mwenendo mbovu wa shughuli za kisiasa ndani ya mataifa hayo huku chama tawala kikijipa ufalme mbele ya kada nyingine za kisiasa.
Kitendo hiki kinadhihirisha jinsi vyombo vya dola vinavyotumika kwa maslahi ya kuhakikisha chama tawala kinapata kwa ukamilifu kile kinachokitaka kwa nguvu. Kwenye nchi inayojinasibu kuwa ya kidemokrasia na inayofuata mfumo wa uchaguzi huru na wa haki kuwapata viongozi wa wananchi, kufanya hivi ni upuuzi mtupu kwa vyombo vya dola. Aidha ni dalili ya ukomavu duni wa vyombo hivyo.
Huwezi kujitapa hadharani kuwa demokrasia itatamalaki kwenye uchaguzi mkuu huku mafichoni vyombo vinavyoshughulikia hayo vikionyesha udhaifu mkubwa kiutendaji na kwenye matokeo.
Tumuombe na tumpe rai Rais Magufuli kuwa haya yanayotokea yana dhamana juu ya mikono yake. Hii ni nchi yenye watu wa kada mbalimbali kisiasa. Nimkumbushe tu kuwa kilichoharibu ustawi wa nchi nyingi duniani ni mwenendo mbovu wa shughuli za kisiasa ndani ya mataifa hayo huku chama tawala kikijipa ufalme mbele ya kada nyingine za kisiasa.