Kitendo cha Kanisa kufungisha ndoa ya Joti huku akiwa amenyoa mtindo wa kihuni ni sahihi?

KWA MIMI NINAVYOFAHAMU NI KWAMBA KANISANI NI MAHALI PATAKATIFU KULIKO SEMU ZOTE NA NDIO MANA WATU WOTE TUNAPAHESHIMU. NA TUINGIAPO KANISANI TUNAJUA TUMEINGIA MAHALI AKAAPO MUNGU MTAKATIFU. SASA KAMA KANISA KATOLIKI WAMESHAFIKA HUKU HADI KURUHUSU VIDUKU MADHABAHUNI BASI HAPO INABIDI TUTAFAKARI TUMETOKA WAP NA TUNAENDA WAPI KWANI BWANA WETU YESU KRISTO AMBAYE NDIYE KIONGOZI WETU MKUU WA WOKOVU WETU NA NDIYE TUNAYEMFUATA ALITUAMBIA TUYAONAPO HAYO CHANGAMKENI. TUMWOMBE MUNGU SANA ATUFUNULIE KWAMBA NI NYAKATI GANI TULIZO NAZO.
 
weka andiko kiBiblia kuthibitisha huo mtindo wa kihuni! Hayo ni mapokeo tu ndugu. Kwa USA na jamaica unaweza kukutana na pastor amesuka dread lakini kwa Tanzania ni ishara ya uhuni, sasa mfano kama huu una uhusiano wowote na andiko la biblia?
.....Vitabu vitakatifu vinasema, yoyote anyoaye denge amelaaniwa
 
Msihukumu msije mkahukumiwa

Waabuduo halisi ni wale watamwabudu Bwana katika roho na kweli
 
Kwani Joti ni Mlawi?? That gospel was for the Leviticus and not for Lucas Mhaville.BTW do you know who were the Leviticus?
 
Wamekosea sana ukizingatia kuna mabango ya mavazi yasiyo ruhusiwa hapo nje
Sasa nywele ni mavazi??? Chunga sana msikuwa km mafarisayo, waosha mikono na kunawa miguu huku moyoni wakiwa wachafu hatari.

Kumbuka story ya makaburi yanayo ng'ara kumbe ndani ni mifupa tupu, kuna watu wanavaa vyema ila ni waovu ajabu...!
 
Kwa kanisa katoliki,hiyo sio inshu,kwani hushangai hata.
1.kashfa ya ulawiti kwa watoto unaofanywa na mapadri.
2.kashfa ya wizi katika benki ya Vatican.
3.Mauaji yaliofanywa na kanisa hili karne nyingi zilizopita,angalia kwenye internet,"SPANISH INQUISITION"ambapo watu takribani 100,000,000 waliuwa.
 
Lesbians and gays ni kama ulemavu mwingine... Hatuwezi kuwatupa walemavu wetu, cha msingi tuendelee kuishinao kwa upendo wakweli. Nao waweza Pona nakuwa raia wema
Na huwa wanaenda kanisani pia...!! Sasa kama mnyoo tu inakuwa shida, hao lesbians na gays inakuwaje?

Usihukumu....
 
Kwani Joti ni Mlawi?? That gospel was for the Leviticus and not for Lucas Mhaville.BTW do you know who were the Leviticus?
Usomaji wa maandiko Matakatifu lazima utofautiane na usomaji wa maandiko mengine. Kwa uelewa wako unadhani kitabu cha Esta, Ruth, Hosea, Yoeli, Ezekiel, n.k hivyo navyo kwa mantiki yako vitakuwa vinazungumza juu ya hao watu tu bila kufundisha wengine?
Kwa ufupi kitabu cha walawi kilikuwa kinawahusu walawi na maonyo kwa watu wengine juu ya kuenenda vyema mbele za Mungu wao.
Wao ndio walikuwa wanasimamia usafi wa kanisa kiroho, ikiwa ni pamoja na kutoa makatazo kwa mambo yanayomchkiza Mungu.
Endelea kushupaza shingo, ninachojua, katika mambo ya kiroho mtu ashikiwi bakora ili apelekwe ktk ukweli wa neno bali hiyo ni kazi ya ROHO MTAKATIFU.
 
I ain't no a damn believer.I just challenged what you believe dude.
 
Pamoja na kuwa mimi ni shabiki mkubwa wa JOTI...
Ila nashangaa JOTI Akiwa anaigiza tangazo la jaza ujazwe...alionekana amevaa Suti kali na Tai..kumaanisha heshima labda wazunge wale wenye kampuni ya tigo wa hungary walimlazimisha kuvaa ile suti ingawa alipendeza mno...kwa lile TANGAZO.ILA Kuja kwenye harusi tuuu kwasababu yeye ndo mchaguzi na huru kachagua kuwa na kiduku na mavazi ya sio suti...kwenye harusi ila kwenye matangazo ya tigo kwakuwa analipwa na inabidi apendeze lazima avae suti ili alipwe....Sasa kwenye harusi avae suti na asiwe na kiduku kwani Nani anamlipa?
Hahahaha Joti bwana...basi sawa....
 
weka andiko kiBiblia kuthibitisha huo mtindo wa kihuni! Hayo ni mapokeo tu ndugu. Kwa USA na jamaica unaweza kukutana na pastor amesuka dread lakini kwa Tanzania ni ishara ya uhuni, sasa mfano kama huu una uhusiano wowote na andiko la biblia?
Biblia imekataza kunyoa Denge.
 
Lesbians and gays ni kama ulemavu mwingine... Hatuwezi kuwatupa walemavu wetu, cha msingi tuendelee kuishinao kwa upendo wakweli. Nao waweza Pona nakuwa raia wema
Mkuu ni wakati huu wa Neema tunaendelea kuwaonya wabadili tabia zao lakini watambue wasipobadilika wataingia ktk jehanum ya moto.
 
Mkuu KANISA hata UFUNGE NDOA NA DUME / JIKE wakiwa JINSIA MOJA UKRISTO haukatai...sio kosa mkuu hilo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…