Kitendo cha kukamatwa viongozi WACHADEMA kwa kutaka kuandamana kwa amani kimeleta taswira ambayo si nzuri serikali ya Awamu ya Sita

Kitendo cha kukamatwa viongozi WACHADEMA kwa kutaka kuandamana kwa amani kimeleta taswira ambayo si nzuri serikali ya Awamu ya Sita

fazili

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
16,427
Reaction score
22,418
Kiongozi wa CHADEMA Freeman Mbowe ameonekana kwenye video akikamatwa wakati anaongea na waandishi wa habari. Hapo ni kabla ya kufanya maandamano ambayo hata kama angeyafanya katiba ya Jamhuri ya Muungano haimkatazi. Mheshimiwa Mbowe amekamatwa pamoja na viongozi wengine wa CHADEMA akiwepo mkamu mwenyekiti Tundu Lissu na mwenyekitii wa CHADEMA kanda ya kaskazini Godbless Lema.

Jambo hili limezidi kuichafua serikali ya Tanzania mbele ya macho ya wananchi na jumuiya ya kimataifa. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaruhusu maandamano lakini cha kushangaza Jeshi la Polisi mwishoni mwa wiki iliyopita lilitoa amri ya kukataza maandamano ya CHADEMA. Hii sio mara ya kwanza kwa serikali ya awamu ya 6 chini ya uongozi wa Samia Suluhu Hassani kuzuia maandamano ya vyama vya upinzani hususan CHADEMA.

Ni vyema serikali ikaheshimu katiba na uhuru wa kujieleza kama inavyoelezwa kwenye katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Soma Pia: Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe ajitokeza Magomeni, akamatwa na Polisi
 
20240923_105848.jpg
 
Inamaana maandamano hayajafanyika? Mbowe si alisema hata akikamatwa msirudi nyuma?
 
Inamaana maandamano hayajafanyika? Mbowe si alisema hata akikamatwa msirudi nyuma?
Mnakuwa wajinga nyie watu kwa kufikiri Mbowe anapigania mambo yake na ninafikiri kwasababu akili zenu ni mbovu na hamuoni kwamba hata ni vibaya mauaji yanayoendelea ambayo Mbowe na wengine wanataka serikali iyazuie. Ujinga wako mkubwa sana.
 
Hawajakamatwa kwa kosa la kuandamana wamekamatwa kwa makosa ya uhaini kosa ambalo halina dhamana na hukumu yake ni kifo
 
Back
Top Bottom