Semistocles
JF-Expert Member
- Jul 2, 2016
- 1,932
- 1,126
[emoji23]me wakati mdogo nilikua nachelewa kutoka shule coz nilikua tukiruhusiwa tu kurudi home natafuta viboko naanza kuchapa majani na miti njiani huku naisemesha km wanafunzi...kufika home late
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Ebwana mie nilikuwa nimebanwa na haja kubwa halafu sehemu niliyokuwepo ni mbali na nyumbani,jamaa akanichuza et niweke mawe kwenye mifuko ya bukta ndiyo yatapungua. Kilichofuata ni kujinyea na niliporudi nyumbani chupi nikaitupa chini ya uvungu wa kitanda.
Ulikuwa kichaaaaa[emoji23] [emoji23] [emoji23]Pia nakumbuka kua nikiingia bafun kuoga naingia ndan ya karai lemye maji.ya moto.ambayo yshapoozwa kwaio.naingia ndan ya karai nauchapa usingiz tena saio.na kile kibarid cha.asubuh na yale maji ya moto aise acha tu ..bada ya muda nashtuka.nimeanza kugongew mlango wa bafuni hahahhh
ha ha ha ha haNiliwasha moto nyuma ya nyumba ya jirani nilipojaribu kuuzima ukanishinda,nikaamua kutoka nduki mpaka home na kujificha kwenye uvungu wa kitanda.Kuuzima moto ule ilibidi mtaa mzima ukusanyike.Baadae nikadakwa raia wakanisamehe kwa kua nilikua mdogo sana.
[emoji23][emoji23][emoji23]Ulikuwa kichaaaaa[emoji23] [emoji23] [emoji23]
Hahahaaa kama sio Ustadhi Yasin Abdallah basi wewe utakuwa J Msangimimi ndio nilikuwa refa wa ngumi,yaani muda wa kutoka shule wanafunzi wenzangu walikuwa wanakuja kuniuliza kama kuna pambano.Yaani walikuwa wakitibuana tu,wanakuja kwangu kutoa taarifa nami nawaingiza kwenye ratiba.Wakati mwingine nilikuwa naratibu mapambano mpaka matatu kwa siku.Sheria ilikuwa ukitoka damu basi pambano limeisha na wewe uliyetoka damu ndio umeshapigwa.Kimbembe ni siku siri ilipovuja kwa walimu baada ya mtoto mmoja kula kichapo mpaka jino likatoka na mzazi akaja kesho yake shule.Yaani nilipomuona tu kijana yuko na mzazi wake wanaenda ofisi ya mwalimu mkuu,nilikula kona na sikutokea shule wiki nzima.Nilikua nikitoka nyumbani naaga naenda shule kumbe naishi porini.Bahati mbaya kuna siku dogo mmoja aliniona nimebana miembeni,daaah akaenda kumtonya ticha.Asikuambie mtu,darasa zima lilitumwa kunikamata,kuna watu wana mbio sio mchezo.Nilichezea fimbo sana siku hiyo na ndio nikastaafu rasmi urefa na kuratibu ndondi.
hahaaaaaaaa,walitakiwa walimu wavumbue kipaji na sio kunilamba fimbo na kusitisha ndoto zangu za kuwa refa wa ndondi bora dunianiHahahaaa kama sio Ustadhi Yasin Abdallah basi wewe utakuwa J Msangi
[emoji28] [emoji28] [emoji28] [emoji28] [emoji23]hahaaaaaaaa,walitakiwa walimu wavumbue kipaji na sio kunilamba fimbo na kusitisha ndoto zangu za kuwa refa wa ndondi bora duniani
kwa saikolojia ya haraka haraka ni kwamba umetoa ya moyoni kwa namna nyingine,kwamba wewe ulikuwa ukitenda hayo.Very brave of uMbona humu sijaona mtu anaandika kwamba alikuwa kikojozi wa kuozesha magodoro ya pamba kila kukicha? Wengine humu mlikuwa mnajisaidia haja kubwa kitandani usiku wa manane mkiwa mnaota ndoto, kwamba mpo msalani. Mbona hayo yote hamsemi? Au mmeyasahau? Kama mmeamua kusema mambo yenu ya utotoni hadharani basi semeni yote tuujue ukweli. Msitubabaishe hapa.
[emoji23] [emoji23] [emoji23]Mie nilimcharanga shoka kuku aliekua anaataga na kupasua mayai yake yote baada ya kuanza kunipigia kelele nikiwa natengeneza gari languu la mbaoo.... Nilikua sipendagi ujinga mimi nikiwa kwenye kazi zangu
OK tuanze na wewe.Mbona humu sijaona mtu anaandika kwamba alikuwa kikojozi wa kuozesha magodoro ya pamba kila kukicha? Wengine humu mlikuwa mnajisaidia haja kubwa kitandani usiku wa manane mkiwa mnaota ndoto, kwamba mpo msalani. Mbona hayo yote hamsemi? Au mmeyasahau? Kama mmeamua kusema mambo yenu ya utotoni hadharani basi semeni yote tuujue ukweli. Msitubabaishe hapa.