macho_mdiliko
Platinum Member
- Mar 10, 2008
- 25,191
- 48,765
Swali la kwanza. Anabadilisha soksi? Soksi zinatakiwa zivaliwe mara moja tu halafu zinafuliwa. Siyo week nzima unavaa soksi hizo hizo. Pia kuna cream au powder inaitwa mycota, unapaka kati ya vidoleKwanini sasa niseme uongo wakati humu hatufahamiani?
Hapo Sawa sasa nimekuelewa vizuri MkuuUnasafisha miguu walau kila wiki mara moja au mbili baadae hiyo hali inaisha kabisa unakua poa lakini muhimu usafi, usafi uwe mara Kwa mara
Si ndio na mimi nakushangaa!Kwanini sasa niseme uongo wakati humu hatufahamiani?
Na soksi ziwe za Cotton sio PolyesterSwali la kwanza. Anabadilisha soksi? Soksi zinatakiwa zivaliwe mara moja tu halafu zinafuliwa. Siyo week nzima unavaa soksi hizo hizo.
Hapa sijaelewa Chumvi unaweza kuonja Wapi?Sasa hivi Ni mkavu hata chumvi unaweza kuonja.
Bakteria na fangasi zinazosababishwa na uchafu.Kuna rafiki yangu ana tatizo la miguu kutoa harufu kali, yani akivua viatu ni balaa, akinitembelea home huwa namwambia aingie na viatu, wapo waliomshauri aloweke miguu kwenye maji ya betri mwisho wa siku akaishia kuchubuka miguu lakini wapi, kwa kifupi amehangaika sana bila mafanikio.
Kwa yeyote ambaye amewahi kupitia changamoto kama hii na akafanikiwa kuitatua atujuze tafadhali.
Una mshauri akafanyaje ili tatizo limuishe?Bakteria na fangasi zinazosababishwa na uchafu.
Asante kwa ufafanuzi mkuukuna visababishi vingi sana vya miguu kutoa harufu
- Jasho na Bakteria au Soksi na Viatu ambavyo havipitishi hewa:
- Jasho: Miguu ina tezi nyingi za jasho. Wakati miguu inapokuwa kwenye viatu au soksi kwa muda mrefu, hali ya unyevu inatokea.
- Bakteria: Bakteria wanaishi kwenye ngozi na hula seli za ngozi zilizokufa na jasho. Wanapofanya hivyo, huzalisha kemikali zinazotoa harufu mbaya. Bakteria kama Brevibacteria ni maarufu kwa kutoa harufu hii.
- Soksi na viatu visivyo pitisha hewa huzuia mzunguko wa hewa, hali ambayo inachangia kuongezeka kwa jasho na unyevu, hivyo kuzalisha mazingira bora kwa bakteria.
- Usafi wa Miguu:
- Kutokuweka miguu safi inaweza kuongeza uwezekano wa seli za ngozi zilizokufa na jasho kuachwa miguu, hali inayowezesha bakteria kuzaliana zaidi na kutoa harufu mbaya.
- Matatizo ya Kiafya:
- Baadhi ya matatizo ya kiafya kama hyperhidrosis (hali ya kutoa jasho nyingi) yanaweza kusababisha miguu kutoa harufu kali zaidi ya kawaida.
- Maambukizi ya kuvu kwenye miguu kama vile athlete’s foot yanaweza pia kusababisha harufu mbaya.
- Lishe na Vinywaji:
- Vyakula fulani na vinywaji kama vile vitunguu, vitunguu saumu, na pombe vinaweza kuchangia harufu mbaya ya mwili, ikiwa ni pamoja na miguu.