Kitu gani kwenye usafiri huwa unafanya Kisha baadaye ukimbuka unacheka/una huzunika.

Kitu gani kwenye usafiri huwa unafanya Kisha baadaye ukimbuka unacheka/una huzunika.

Masinki

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2014
Posts
709
Reaction score
478
Ni Jumamosi tulivu Sana ya mwaka 2020 wabongo wanaita Njaanuari hii,,imani yangu mpo in good spirits ingawa mifukoni kunaweza kusiwe POA.
Wengi wetu hizi forum/mitandao ya kijamii ndio inatupa ahueni ya mawazo,yaaap acha nijielekeze kwenye mada yangu ya leo.
Kuna Mambo mengi yanayofurahisha Sana pindi tuwapo kwenye usafiri haswa wa umma na mengine yanatia huzuni ukiyatazama ama kuyafikiria,basi Kila mmoja kwa nafasi yake anaweza kutoa ya moyoni hapa aliyokutana nayo kwenye usafiri.
Mimi binafsi ninayo mengi lakini nikushirikishe kwa haya machache ,siku moja natokea wilayani kuelekea mkoani ikizingatiwa barabara zetu za vumbi usafiri huwa ni shida kidogo,kilikuwa na kipindi Cha kumalizika kwa sikukuu za krismas yaani trh 27.
Tukiwa njiani walipanda watu wengi sana,wengine watu wazima wananizidi umri hatujuani,wengine nawajua/wananijua ni Kama jamaa kwangu.
Balaa likaja bus ilianza kujaa viti vyote vikawa level seats,na bado Kuna wasafiri wengi nahisi na kwasababu ya sikukuu wengi walirudi majumbani kwao,basi bana kufika vijiji vya Kati akapanda Baba mdogo umri 50's nilimuona na kumsikia akilalamika lakini baharia nilitulia Kama sio mm vile nikajifanya nasinzia licha ya kwamba huwa silali kwenye gari kabisa,na Tena niliziba masikio nisimsikie anavyolalamika,nilijiambia kimoyo moyo sitaki kusimama mm licha ya tamaduni zetu kutoruhusu lakini nilikaza.
Kila nikitaka kufumbua hata jicho nimuone inakuja,,inakataaa ,kiukweli waliosimama walikuwa wengi kuliko waliokaa na baharia nikasema hata iweje huyu mzee sitampisha ilihali afya yake ni imara sikuweza Hadi pale nilipoona Kuna gari jingine likaja Wakafaulishwa ndio amani yangu ilirejea.
Anyway sijakutana nae Hadi Sasa nimsikie kujua je aliniona?ni kitu ambacho Kila nikifikria nabaki kucheka na huruma juu.
Kingine ni siku moja katika safari Dada mmoja kushikwa na tumbo la kuhara hahahahaha sitasahau hilo.nisiwachoshe Sana.
 
1. Kuna siku nilikuwa natokea Bukoba to Mwanza. Nimetulia zangu kwenye seat. Ile tumefika Muleba Akapanda Mzee mmoja ( Siyo mzee sana ). Seat zimeshajaa

Basi limetembea, baada ya muda mzee uzalendo ukamshinda, akaning'oneza - kijana chukua Tsh 1,000 uniachie seat nikae.

Nikamtizama, Nikamhurumia Nikamwambia Mzee Kaa Tu Usijali. Nikampisha.

Tulipofika Busisi ( Kuna Kivuko ) akanitafuta akitaka kunilipia, nikamwambia ninayo pesa wala asijali sana.

2. Siku moja nimepanda daladala za G/Mboto - Mbagala, Kwenye Seat nikakuta kuna kinada kimekaa kina furushi la bag na mtoto kama wa 3 years. Chenyewe Kimepakata Furushi hata mtoto kimekaliza kwenye seat. Tukawa Kama Tumekaa Watatu, Nimekaa Kwa Shida Kweli. Nikakiambia Chukua Bag Lako Weka juu ya Carrier Halafu Pakata Mtoto Tukae Vizuri. Kikakaa Kimya. Nikarudia Tena. Kimya. Nikamwambia Konda, Ile Anakiuliza Kikawa Kikali Kinaongea Kwa Sauti Kubwa Gari Zima Wanasikia Eti Nimekitongoza.
Nilivyoona Kimezidi "Nikakichapa Mabanzi Mawili Ya Uso" Halafu Nikahama Seat
 
Kukata uzi kwa sauti huku umevaa Headphone huku ukidhani abiria wenzako hawakusikii.

dodge
 
Back
Top Bottom