Kitu gani uliwahi ona au kushuhudia ukacheka sana?

Kuna uzi huku wa siku nyingi kweli ilikua kuhusu kuongea kilugha. Sasa kuna Mnyakyusa akaelezea story yake kiwa shuleni kwao waliwekewa bango la speak Swahili ukiongea Kinyakyusa tu unavalishwa bango. Akapatwa na chafya kalii akaipiga ile ejooooo kwa bahati mbaya. Yani nikikumbukaga ile comment nacheka tu.

Napendaga kucheka sana nikiwa na rafiki zangu hasa nikiwa nakunywa. Yani rafiki yangu anaweza akawa ananisema mimi nakufa kwa kicheko inabidi na yeye aahirishe aanze kucheka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] kuna nyuzi humu zinachekesha mnoo siku hizi hata hazipo sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna siku binti yangu alitembelewa na ndugu zake toka kijijini. Walishangaa kumkuta ana nywele ndefu had mgongoni (alikuwa ameshonea weaving). Wakashangaa sana. Wakasema he! Kumbe mjini kuna raha hivi! Had nywele zinabadilika! Umekuwa kama mzungu. Mmoja wao akasema "sirudi tena kijijini. Nataka nibaki mjini ili niwe na nywele ndefu kama zako!". Walikuwa wakiongea hivi huku wanazishika shika. Nilicheka sana (japo nilijifanya sihusiki kwenye mazungumzo yao). Sikufikiria kama kizazi hiki kuna ambae hajui kuhusu mawigi na weaving
 
Mi kuna siku ninatoka na mshua tunaenda church!
Ilinyesha mvua sasa kukawa na matope ile navuka mtaro nikateleza nikajikuta nimeka chini kwenye tope!!
Mzee akaniambia rudi nyumbani ukabadili suruali!!
Ile narudi home nikasikia kishindoo tiiiiii!
Mzee naye aliteleza kwa kweli nilishindwa kuvumilia kicheko!😁
Mzee naye alicheka balaa tunarudi home bi Mkubwa anadhani tulivamiwa
 
Msalimie Binti yako Mkuu.
 
Umetunga ama?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
niliwahi kumwambia dereva mwenzangu usipak gari hapo panatitia na kuna upepo mkali unakatiza, ilikuwa isaka, akanijibu kamfundishe baba yako nimeanza kuendesha we unanyonya,, dakika mbili nyingi chombo ikabetuliwa na upepo yaani inaanguka taratibu slow motion huku jamaa kashika kichwa anaangalia semi inamfuata mpaka tukamuwah kumvuta, aisee baada ya kumuokoa nilicheka mpaka tumbo iliuma siku nzima, hasa majibu aliyonijibu dakika kadhaa zilizozipita na jinsi alivyokoga vumbi baada ya chombo kupinduka.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lazima ucheke aisee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahahahaaaaa hii hata Mimi nimecheka

Sent from my TECNO-C5 using Tapatalk
 
Nimecheka hapa nimeimagine ambavyo mnachekana na mzee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku moja nakumbuka nimeingia kwenye mgahawa mmoja hivi , aseeeh nilikutana na bomba la kunawia ambalo sijui hata linafunguliwaje. Nilihangaika sana bila mafanikio na nikawa naona aibu kuuliza , niliganda pale pale nikawa najifanya nakunja shati huku nikisubiri mtu aje ili nione wanavyofungua. Basi, ikapita kama dakika moja hivi mdada akaja kunawa.
mdada: Kaka za sahizi?
Mimi: salama Dada
Mdada: vip kaka,maji yameisha nn mana nimekuona upo umesimama hapa muda mrefu?
Mimi: maji yapo, ila kuna mtu tu namsubir hapa[emoji4]
Mdada: anhaa, si ungeket tu kweny kiti kaka angu?
Mimi: kimoyo kimoyo nikawa najisemea huyu Dada katumwa nn[emoji1] ?


Basi alivyomaliza tu kunawa na mimi nikaenda kunawa, kumbe ili maji yatoke unatakiwa ubonyeze kibatan ambacho kipo pale pale juu ya bomba then ukimaliza we unasepa zako, bomba linajifunga lenyewe bila kuguswa[emoji1] [emoji1] [emoji1] , mi nilikuwa nahangaika kuzungusha Tu. Dah huwa nacheka sana nikiifikiria hii siku

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…