Kitu gani unachokumbuka ambacho mama yako alikuonya ukiwa mtoto na mpaka leo hukisahau?

Hapa alimaanisha usipende kuwaeleza watu udhaifu/shida zako?
hapana nilikua nasumbuliwa na kitu
nikawa sielewi moyo wangu unataka nini, kwanini niwe vile, je nifanye nini niepukane na hali ile
sasa mama akawa amenishauri sana na watu lakini sikushaurika
ndo akaamua kuniambia hivo kuwa niseme na moyo wangu
nijue unataka nini na wapi nakosea na nini nifanye kuepukana na hali hio
 
Kuchelewa kurud nyumbani, alikuwa anafinya masikio, Ni nani.... alikwambia... urudi usiku nyumbani.? Tabia ni kama ngozi aisee siku hiz nipo Huru ghetto narud usiku mshale unasoma AM. Night kali.

Kiukwel kutembea usiku sana sio jambo jema, hasa kama una drive Kuna mengi sana yana happen njiani. Assume umepata brake down. Au unakuta na na walio kazin.
 
Ni kweli aisee!

Ndo ujirekebishe sasa, rudi home muda ambao ni reasonable!
 
Hahahahahaha sisi boarding kwetu tulikuwa tunaita 'kufaitia' meaning 'fighting' for food [emoji23][emoji23][emoji23]
Hahaaa kule kama umeenda na ustaarabu wako lazima utauacha tu
 
1. Mwanamke anaekula njiani haolewi wanaume hawataki mwanamke anaekula hovyo

2. Usipende kunusa chakula utakatika pua.

3. Usikubali kubadili dini kwa sababu ya mwanaume

4. Soma sana uje kunisaidia mama yako.

Mama yangu ni zaidi ya mama kwangu kwani anaplay na role ya baba. Mpaka Leo naogopa kunusa chakula na nilisoma kwa bidii ili nisimdisappoint mama.
 
Mwanangu usipende kulala sana...usingizi ni adui wa maendeleo

Mwanangu kwenye nyumba yk usikanyage mchanga..na usikae sehem chafu

Usimtegemee mwanaume kwa kika kitu

Jishushe haitakupunguzia kitu ila itakuongezea heshima..usiwe mwepesi wa kudakia vitu na usiwe mjuaji

Nakupa kila kitu usome uje uishi vizur

Ukiustiri mwili wako utaheshimika

Usipende kutembea usiku..giza lina mengi mabaya

Sijui nimpe nini mama yang..amenifundisha sa kuish na watu..nampenda mno..tuwapende sana mama zetu na polen kwa waliotangulia mbele za haki
 
"Mwanangu ktk maisha ya ndoa ambayo ndiyo hatua kuu unayoielekea miaka mitano sita hivi inayokuja OGOPA KUWA CHANZO KWA MWANAMKE KUTOKA MACHOZI kwa sababu yoyote ile, USIMUUMIZE MTOTO WA MTU KWENYE ndoa mtakayounganishwa na Mungu, sitaki kuona mwanamke anakuja analia kwangu kisa wewe".
Machozi yetu wanawake kwa wanaume huzuia mafanikio, yana laana, hayafai. "Usisahau mwanangu"(2006)

Shkamoo mama,
Rest in eternal Peace
 
Kitu ambacho sikisahau tangu nikiwa mdogo nijinsi mama anavyo umia nikipata tatizo na kulifanya tatizo langu ni lake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…