Kitu usichokijua kuhusu ‘juisi ya boksi’

Kitu usichokijua kuhusu ‘juisi ya boksi’

Ndio mzizi mkavu,kumbuka yafuatayo,
1.matunda hukamuliwa na kuifadhiwa kwa njia za kienyeji na kisasa preservative inayotumika mara nyingi ni sodium benzoate inayokubalika kama food grade..kuifadhi na kusindika matunda ni vizuri kiuchumi kwa kuyaongezea thamani na pia matunda ya aina moja hayapatikani kipindi chote cha mwaka hivyo huifadhiwa ili kuokoa hasara ya kupoteza matunda wakati wa msimu,TAnzania tunaitaji hii ili kusaidia wakulima na walaji, usiwatishe wadau.
2.kufanana kwa ladha ya matunda ni selection anayoweza kuifanya msindikaji au inategemea na wingi wa matunda katika nchi husika, takwimu kutoka association of mango growers in tanzania kuna zaidi ya aina 50 za maembe yanayolimwa kwa sasa east and central Africa eg. Pwani utapata bolibo na apple kwa wingi india utapata totapuri unategemea msindikaji wa eneo hilo ataprefer aina ipi?ikizingatiwa na aina ya embe lililozoeleka kwa walaji?
3.Hata matunda unayopata sasa mengi sio organic kwa hiyo usibabaike.
4.Kwa wadau wa chakula tunajua kila kitu kina impact toa article kuhusu coke uone ni wangapi wataichagua dhidi ya juice ya box.

Mwiso napenda kutoa wito kwa wadau kupanda matunda na kuwekeza katika viwanda vya matunda ili kukuza uchumi wa Taifa letu.
 
Hii ni hatari kwa jamii yetu asante kwa kutujuza
 
FAIDA YA UBUYU.

attachment.php




UBUYU WENYEWE

Unga wa ubuyu unaelezwa kuwa na vitamini na madini mengi kuliko matunda mengine. Inaelezwa

kuwa unga wa ubuyu una Vitamin C nyingi kuliko hata machungwa na ina kiwango kingi cha madini

ya kashiamu (Calcium) kuliko hata maziwa ya ng’ombe.

Aidha, unga wa ubuyu ni chanzo kikubwa cha madini mengine aina ya chuma (iron), Potasiamu

(Pottasium) na manganizi (magnesium). Inaelezwa kuwa kiwangao cha Potasiamu kilichomo kwenye

unga wa ubuyu ni mara sita zaidi ya kile kinachopatikana kwenye ndizi. Ubuyu ni muhimu sana kwa

watu wenye matatizo ya figo.

Vile vile unga wa ubuyu una uwezo mkubwa wa kuongeza kinga ya mwili (antioxidant) kutokana na

kuwa na kiwango kikubwa cha virutubisho vya kuongeza kinga mwilini dhidi ya magonjwa

nyemelezi. Kiwango chake kinazidi hata kile kinachotolewa na matunda mengine kama vile Krenberi,

bluberi na blakberi. Ili upate faida za unga wa ubuyu zinazoelezwa hapa, lazima ule ubuyu halisi

usiochanganywa na kitu kingine cha kuongeza ladha



UNGA WA UBUYU :


* Hutumika kutengeneza juisi. ( Juisi ya ubuyu ina vitamnini C nyingi kuliko tunda lingine lolote duniani.


*Husaidia kuongeza kumbukumbu.


SABUNI YA UBUYU :


* Huondoa mabaka, mmba, chunusi , madoadoa na mwasho wa ngozi


* Hulainisha ngozi na kuifanya yenye mvuto daima.
* Hutibu fangasi na huwasaidia walio haribiwa ngozi na vipodozi.
* Huwasaidia wenye ulemavu wa ngozi.

FAIDA ZA JUISI YA UKWAJU.



[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Tunda la Ukwaju.[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Tunda la ukwaju ni tunda lenye faida nyingi sana kwa afya ya mwanadamu. Tunda hili huweza kutumika kutengeneza juisi ambayo matumizi yake yana faida kubwa sana katika afya ya mwili wa mwanadamu.





[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Juisi ya Ukwaju.[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

NAMNA YA KUTENGENEZA JUISI YA UKWAJU.

Nunua ukwaju wako, ukwaju unapatikana kwa wingi sana masokoni na kwenye supermarkets

  • andaa maji kwenye dishi na uoshe kidogo tuu
  • baada ya kuuosha chukua ukwaju wako weka kwenye sufuria yenye maji ya saizi na injika jikoni
  • uache uchemke kwa dakika 10/15 ili uuwe vijidudu
  • ipua ukwaju wako jikoni na uache kwa muda upoe
  • andaa maji yako masafi na chujio ili uweze kuchuja juice yako kwa uangalifu zaidi ili upate juice yenyewe
  • weka sukari kwa kiasi unachopendelea
  • pia ili kupunguza ukali unaweza ukaweka hiliki au vanila ili kupata taste
  • weka juice yako kwenye fridge ili ipoe tayari kwa kunywa

FAIDA YA JUISI YA UKWAJU.


  1. Chanzo kizuri cha viuasumu mwilini 'antioxidants' ambavyo huzuia Saratani (cancer)
  2. Chanzo cha Vitamini B na C vile vile "carotentes"
  3. Hushusha joto la mwili na kuondosha homa, hasa homa ya malaria na homa ya matumbo
  4. Huulinda mwili dhidi ya mafua na kero za mafua kooni
  5. Husaidia myeyusho na mmengenyo wa chakula na kuondosha kuvimbiwa
  6. Husaidia kutibu matatizo ya nyongo (bile disorders)
  7. Husaidia kurahisisha choo (laxative)
  8. Husaidia kupunguza wingi wa lehemu (cholesterol) na hivyo kuimarisha moyo
  9. Husaidia ngozi kuwa nyororo, vile vile husaidia ngozi inayopona baada ya kuungua au yenye vidonda
  10. Husaidia kuua minyoo tumboni (kwa watoto wadogo)

NB: Ikiwa ukwaju na asali havikudhuru, basi changanya hivyo viwili ili kupata faida maradufu!




Nashukuru sana MziziMkavu
 
Last edited by a moderator:
Daah kaka mkubwa kila kitu ukishatoa demerits huwa nakinote, nasubiri siku ukija na madhara ya kuoa/kuolewa na mke/mume mzuri!
 
Back
Top Bottom