Simara
JF-Expert Member
- Oct 1, 2014
- 7,512
- 23,925
Leo nimekumbuka vituko vya babu yangu, Babu yangu alikua anapenda sana kujifungia chumbani kwa hiyo muda mwingine unampelekea chakula huko huko ! Siku hiyo nimeenda nampelekea chakula naita babu babu kimya wakati namuona ndani kakaa nikaita tena babu akanijibu babuka yani nilicheka nusu nizimie sijui alikuwa na hasira gani hahahaha!!
Kuna siku kagoma kulala eti kilipo kitanda sio kila siku kinapokua so wamrudishie kinapokaa, sasa wanamuuliza huwa kinakaa wapi anaonyesha sehemu lilipo kabati la nguo. ha ha ha ha nilicheka ile siku maana aligoma kulala kama hawataki ni heri alale chini kesho arudi kijijini!! ikabidi kitanda kifunguliwe wasogeze kabati wakifunge tena.....wakina anko na mama walinunaa kwa hasira!!!
Share kituko chohote cha bibi/ babu yako unachokikumbuka
Kuna siku kagoma kulala eti kilipo kitanda sio kila siku kinapokua so wamrudishie kinapokaa, sasa wanamuuliza huwa kinakaa wapi anaonyesha sehemu lilipo kabati la nguo. ha ha ha ha nilicheka ile siku maana aligoma kulala kama hawataki ni heri alale chini kesho arudi kijijini!! ikabidi kitanda kifunguliwe wasogeze kabati wakifunge tena.....wakina anko na mama walinunaa kwa hasira!!!
Share kituko chohote cha bibi/ babu yako unachokikumbuka