Teh teh..Ukisikia kitu kipya unakidaka fasta...Teh teh teeeeh! Ukataka kumbikiri sister! Ila sijui kuna nguvu gani kwenye maneno mabaya, watoto huwa rahisi sana kuyadaka.
Nimecheka sana! Hiyo tabia alikuwa nayo rafiki yangu, kuna siku alidandia kwenye tela la tractor, kumbe ule mlango haukuwa na lock, sasa kakimbizia weee hadi akalifikia, ile kushika tu ule mlango ukashuka na kutua kichwani! Alilazwa hospitali wiki za kutosha!Nakumbuka nilikua na mchezo wa kudandia magali kwa nyuna bila dereva kujua..bas siku moja nilidandia trector nikashindwa kushuka trector lilikua linafata mawe polini mbali kidogo...nlivoona naji yamenizidi ilibidi nijisalimishe tu kwa dereva...dereva akanambie twende wore mpaka anakochukua mawe tutarudi wot,kufika kule alinigonga bakora za kutosha.
Mda wa kurudi trector likaalibika ijabidi tulale ukouko..uku home nako natafutwa sana Aaah keshi yake nilivorudi nlikura njiti za kutosha..
Nakumbuka watoto wa my sister wanefuatana wa kike na wa kiume(wa kiume ndio mkubwa)Teh teh..Ukisikia kitu kipya unakidaka fasta...
Teh teh..Hiyo kali aisee...Maskini ya Mungu utakuta hapo hata hakajui kanamaanisha nn...Pata picha ndo anasema hivyo mbele za wageniNakumbuka watoto wa my sister wanefuatana wa kike na wa kiume(wa kiume ndio mkubwa)
Kuna siku vilikwenda kucheza hivyo vikachelewa kuoga, mama yao akawachapa kisha akawaogesha usiku sebuleni saa2 wakati tukiwa tunakula.
Akaanza kuogeshwa mdogo wa kike alivyamaliza akaenda kumwaga maji na kuweka mengine sasa yule mdogo akachukua maji kidogo ya baridi akammwagia kaka yale kidogo mgongoni kaka mtu akastuka na kwa hasira akamtusi mdogo wake "nitaku*fira" aisee tulistuka dada kidogo azimie, sijui alilisikia wapi tusi hilo, alikula makofi hadi tukamtetea.
Ha haa unakuta maza mnoko kuliko mzee,afu akianza kumpampu mzee utatamani ukimbilie hata barabarani aiseDaaaah kwa mjerumani(as we used to call our mom) hilo hatukuthubutu kufanya, maana unaweza ukasahau hata jina lako.
Yaani mie baba hakuwahi hata kunifinya na nilikuwa kipenzi chake, ila mama daaaah!! Yaani nikikumbuka vipigo na nilivyokuwaga chautundu hata havihesabiki, unakula stiki hadi unajiuliza "huyu kweli mama yangu"Ha haa unakuta maza mnoko kuliko mzee,afu akianza kumpampu mzee utatamani ukimbilie hata barabarani aise
ha ha ha ha ha...Nakumbuka watoto wa my sister wanefuatana wa kike na wa kiume(wa kiume ndio mkubwa)
Kuna siku vilikwenda kucheza hivyo vikachelewa kuoga, mama yao akawachapa kisha akawaogesha usiku sebuleni saa2 wakati tukiwa tunakula.
Akaanza kuogeshwa mdogo wa kike alivyamaliza akaenda kumwaga maji na kuweka mengine sasa yule mdogo akachukua maji kidogo ya baridi akammwagia kaka yale kidogo mgongoni kaka mtu akastuka na kwa hasira akamtusi mdogo wake "nitaku*fira" aisee tulistuka dada kidogo azimie, sijui alilisikia wapi tusi hilo, alikula makofi hadi tukamtetea.
Unadhani hata maana kalikuwa kanajua basi, kalijiropokea tu sijui alilisikia wapi nae akalidaka, duuuuh yaani tulibaki kimyaaa tunatoa macho tu.Teh teh..Hiyo kali aisee...Maskini ya Mungu utakuta hapo hata hakajui kanamaanisha nn...Pata picha ndo anasema hivyo mbele za wageni
Hahaha mtoto ni mtoto tu. My lil sis yeye alikuwa anaonja kitu chochote mbele yake. Yani kila anachokiona anabugia tu fasta. Tushapata kesi kibao na yeye kwa mzee maana mara leo anywe mafuta ya taa, kesho kabugia mseto dawa, mara atake kuonja mafuta ya betri yani ni heka heka tu. Si unawajua wazee mlivyo, nyie mnaona tu kama sisi hatupo makini na mtoto, wazembe
Siku ya siku, bi mkubwa alihisi kuna panya kaingia ndani. So akamtegea dawa, kosa ni kwamba alichukua kipande cha samaki kizuri tu kwa matumizi ya binadamu, akapaka dawa akategesha kwenye kisosi. Ameingia bafuni kuoga, anatoka kipande cha samaki hakipo. Mmh machale kumcheza haiwezekani dk chache panya awe ashabeba samaki wote yule, kamuita dogo, kumuuliza uliingia chumbani dogo kagoma. Maza kampa kofi takatifu ikabidi kaseme kenyewe ndo kamechukua samaki Hahaha. Mama presha Tafuta maziwa fasta, kumpigia simu mzee fasta (ilikuwa weekend uzuri) wakamuwahisha hospital. Kufika hospital ikaonekana dawa haina nguvu kihivyo so wakampa tu nini sijui
Tatizo sasa mzee wangu ni anapenda utani, me sioni ndani. Ile hospital aloenda ndo huwa tunatibiwa hapo mara nyingi so doctors tumezoeana nao. Dr mmoja akaanza kumzingua mzee " eti daah ila mshkaji hiki si kiashiria kizuri, haiwezekani mtoto achukue hadi samaki wa panya, home lazima kuna uhaba wa nyama nyama. uwe unawanunulia nyama watoto bana", mzee akaishia tu kucheka.
Usiku tumekaa mzee akaanza kuniambia "daah ila watoto wanatiaga aibu jamani, huyu dogo kanifedhehesha leo, utadhani nyama halagi, kumbe anakula hadi basi", nilichekaje
Ahsante mfilipino mwenzangu teh.Hahahah...mkuu nimependa sana kisa chako!
Ila zaidi ya yote nimependa uandishi wako mwandiko umezingatia hatua zote za kiuandishi muundo na maana nukta, koma na kila herufi umeiumba ipasavyo.
Kama ungekua mwalimu ungebarikiwa zaidi kwa kuwasaidia wengi miandiko yao humu na huko ulipo.
Ahsante mfilipino mwenzangu teh.
Hahaha itabidi nikutafute mfilipino mwenzangu unipe Idea fulani amazing kwa ajili ya valentineHahaa...mfilipino
Nimelipenda hili kwakweli!
Hahaha itabidi nikutafute mfilipino mwenzangu unipe Idea fulani amazing kwa ajili ya valentine
Nikiwa mdogo niliwahi kuiba hirizi iliyokuwa inapumua ya mzee mmoja mchawi aliyekuwa anaogopeka sana pale kijijini. .kwenda kuipasua nilikuta kinyonga aliyekatwa mkia alitweta kwa kukosa pumzi vizuri
Lile tukio lilikuwa kubwa na baya pale kijijini mpaka ikibidi nihamishwe
Hahaha basi usismile banaHahaha...ushaanza kunifanya nasmile smile hapaa...
Ile ya mishumaa kwenye mvua huitaki tena eeeh...
He hee mama ni anapiga mpaka unaomba poo. Nilikua naangusha kilio cha nguvu nalia weee kama nusu saa hivi mpaka anakuja kunibembeleza mwenyewe ndio nanyamaza.Yaani mie baba hakuwahi hata kunifinya na nilikuwa kipenzi chake, ila mama daaaah!! Yaani nikikumbuka vipigo na nilivyokuwaga chautundu hata havihesabiki, unakula stiki hadi unajiuliza "huyu kweli mama yangu"
Hahaha basi usismile bana
Teh ile idea wengi watakuwa washacopy bana, nitafutie kitu kingine cha uhakika bana
Poa poa, nakuaminia mfilipino mwenyeweHahah...kweli ile itakua imeshaibwa
Mfilipino vuta subira niwaze tupate amazing nyingine tena kwa valentine day inabidi iwe ni amazing plus