Kituko cha utotoni ambacho sitakisahau

Kituko cha utotoni ambacho sitakisahau

Teh teh teeeeh! Ukataka kumbikiri sister! Ila sijui kuna nguvu gani kwenye maneno mabaya, watoto huwa rahisi sana kuyadaka.
Teh teh..Ukisikia kitu kipya unakidaka fasta...
 
Nakumbuka nilikua na mchezo wa kudandia magali kwa nyuna bila dereva kujua..bas siku moja nilidandia trector nikashindwa kushuka trector lilikua linafata mawe polini mbali kidogo...nlivoona naji yamenizidi ilibidi nijisalimishe tu kwa dereva...dereva akanambie twende wore mpaka anakochukua mawe tutarudi wot,kufika kule alinigonga bakora za kutosha.
Mda wa kurudi trector likaalibika ijabidi tulale ukouko..uku home nako natafutwa sana Aaah keshi yake nilivorudi nlikura njiti za kutosha..
Nimecheka sana! Hiyo tabia alikuwa nayo rafiki yangu, kuna siku alidandia kwenye tela la tractor, kumbe ule mlango haukuwa na lock, sasa kakimbizia weee hadi akalifikia, ile kushika tu ule mlango ukashuka na kutua kichwani! Alilazwa hospitali wiki za kutosha!
 
Teh teh..Ukisikia kitu kipya unakidaka fasta...
Nakumbuka watoto wa my sister wanefuatana wa kike na wa kiume(wa kiume ndio mkubwa)

Kuna siku vilikwenda kucheza hivyo vikachelewa kuoga, mama yao akawachapa kisha akawaogesha usiku sebuleni saa2 wakati tukiwa tunakula.

Akaanza kuogeshwa mdogo wa kike alivyamaliza akaenda kumwaga maji na kuweka mengine sasa yule mdogo akachukua maji kidogo ya baridi akammwagia kaka yale kidogo mgongoni kaka mtu akastuka na kwa hasira akamtusi mdogo wake "nitaku*fira" aisee tulistuka dada kidogo azimie, sijui alilisikia wapi tusi hilo, alikula makofi hadi tukamtetea.
 
Nakumbuka watoto wa my sister wanefuatana wa kike na wa kiume(wa kiume ndio mkubwa)

Kuna siku vilikwenda kucheza hivyo vikachelewa kuoga, mama yao akawachapa kisha akawaogesha usiku sebuleni saa2 wakati tukiwa tunakula.

Akaanza kuogeshwa mdogo wa kike alivyamaliza akaenda kumwaga maji na kuweka mengine sasa yule mdogo akachukua maji kidogo ya baridi akammwagia kaka yale kidogo mgongoni kaka mtu akastuka na kwa hasira akamtusi mdogo wake "nitaku*fira" aisee tulistuka dada kidogo azimie, sijui alilisikia wapi tusi hilo, alikula makofi hadi tukamtetea.
Teh teh..Hiyo kali aisee...Maskini ya Mungu utakuta hapo hata hakajui kanamaanisha nn...Pata picha ndo anasema hivyo mbele za wageni
 
Ha haa unakuta maza mnoko kuliko mzee,afu akianza kumpampu mzee utatamani ukimbilie hata barabarani aise
Yaani mie baba hakuwahi hata kunifinya na nilikuwa kipenzi chake, ila mama daaaah!! Yaani nikikumbuka vipigo na nilivyokuwaga chautundu hata havihesabiki, unakula stiki hadi unajiuliza "huyu kweli mama yangu"
 
Nakumbuka watoto wa my sister wanefuatana wa kike na wa kiume(wa kiume ndio mkubwa)

Kuna siku vilikwenda kucheza hivyo vikachelewa kuoga, mama yao akawachapa kisha akawaogesha usiku sebuleni saa2 wakati tukiwa tunakula.

Akaanza kuogeshwa mdogo wa kike alivyamaliza akaenda kumwaga maji na kuweka mengine sasa yule mdogo akachukua maji kidogo ya baridi akammwagia kaka yale kidogo mgongoni kaka mtu akastuka na kwa hasira akamtusi mdogo wake "nitaku*fira" aisee tulistuka dada kidogo azimie, sijui alilisikia wapi tusi hilo, alikula makofi hadi tukamtetea.
ha ha ha ha ha...
duh hii kali
 
Teh teh..Hiyo kali aisee...Maskini ya Mungu utakuta hapo hata hakajui kanamaanisha nn...Pata picha ndo anasema hivyo mbele za wageni
Unadhani hata maana kalikuwa kanajua basi, kalijiropokea tu sijui alilisikia wapi nae akalidaka, duuuuh yaani tulibaki kimyaaa tunatoa macho tu.
 
Hahaha mtoto ni mtoto tu. My lil sis yeye alikuwa anaonja kitu chochote mbele yake. Yani kila anachokiona anabugia tu fasta. Tushapata kesi kibao na yeye kwa mzee maana mara leo anywe mafuta ya taa, kesho kabugia mseto dawa, mara atake kuonja mafuta ya betri yani ni heka heka tu. Si unawajua wazee mlivyo, nyie mnaona tu kama sisi hatupo makini na mtoto, wazembe

Siku ya siku, bi mkubwa alihisi kuna panya kaingia ndani. So akamtegea dawa, kosa ni kwamba alichukua kipande cha samaki kizuri tu kwa matumizi ya binadamu, akapaka dawa akategesha kwenye kisosi. Ameingia bafuni kuoga, anatoka kipande cha samaki hakipo. Mmh machale kumcheza haiwezekani dk chache panya awe ashabeba samaki wote yule, kamuita dogo, kumuuliza uliingia chumbani dogo kagoma. Maza kampa kofi takatifu ikabidi kaseme kenyewe ndo kamechukua samaki Hahaha. Mama presha Tafuta maziwa fasta, kumpigia simu mzee fasta (ilikuwa weekend uzuri) wakamuwahisha hospital. Kufika hospital ikaonekana dawa haina nguvu kihivyo so wakampa tu nini sijui

Tatizo sasa mzee wangu ni anapenda utani, me sioni ndani. Ile hospital aloenda ndo huwa tunatibiwa hapo mara nyingi so doctors tumezoeana nao. Dr mmoja akaanza kumzingua mzee " eti daah ila mshkaji hiki si kiashiria kizuri, haiwezekani mtoto achukue hadi samaki wa panya, home lazima kuna uhaba wa nyama nyama. uwe unawanunulia nyama watoto bana", mzee akaishia tu kucheka.
Usiku tumekaa mzee akaanza kuniambia "daah ila watoto wanatiaga aibu jamani, huyu dogo kanifedhehesha leo, utadhani nyama halagi, kumbe anakula hadi basi", nilichekaje


Hahahah...mkuu nimependa sana kisa chako!

Ila zaidi ya yote nimependa uandishi wako mwandiko umezingatia hatua zote za kiuandishi muundo na maana nukta, koma na kila herufi umeiumba ipasavyo.

Kama ungekua mwalimu ungebarikiwa zaidi kwa kuwasaidia wengi miandiko yao humu na huko ulipo.
 
Hahahah...mkuu nimependa sana kisa chako!

Ila zaidi ya yote nimependa uandishi wako mwandiko umezingatia hatua zote za kiuandishi muundo na maana nukta, koma na kila herufi umeiumba ipasavyo.

Kama ungekua mwalimu ungebarikiwa zaidi kwa kuwasaidia wengi miandiko yao humu na huko ulipo.
Ahsante mfilipino mwenzangu teh.
 
Nikiwa mdogo niliwahi kuiba hirizi iliyokuwa inapumua ya mzee mmoja mchawi aliyekuwa anaogopeka sana pale kijijini. .kwenda kuipasua nilikuta kinyonga aliyekatwa mkia alitweta kwa kukosa pumzi vizuri
Lile tukio lilikuwa kubwa na baya pale kijijini mpaka ikibidi nihamishwe

Hirizi hiyo alikua anaitundika nyumbani? Nawaza uliibaje.
 
Hahaha...ushaanza kunifanya nasmile smile hapaa...

Ile ya mishumaa kwenye mvua huitaki tena eeeh...
Hahaha basi usismile bana

Teh ile idea wengi watakuwa washacopy bana, nitafutie kitu kingine cha uhakika bana
 
Yaani mie baba hakuwahi hata kunifinya na nilikuwa kipenzi chake, ila mama daaaah!! Yaani nikikumbuka vipigo na nilivyokuwaga chautundu hata havihesabiki, unakula stiki hadi unajiuliza "huyu kweli mama yangu"
He hee mama ni anapiga mpaka unaomba poo. Nilikua naangusha kilio cha nguvu nalia weee kama nusu saa hivi mpaka anakuja kunibembeleza mwenyewe ndio nanyamaza.

Kwenye hii michezo ya kujipikilisha nilichezea vifinyo na vichapo mana kila siku nilikua naiba vitu ndani tunaenda kujipikilisha kwenye njeka.
 
Ngoja nisome zoooote. Huenda nikakuta aliefanya kituko kama nilichofanya.
 
Mie navituko vingi sanaa maana utotoni nilikua mtundu kupindukia
1. Nikiwa na pacha wangu tunatengeneza magari ya mbao gafla bandani kulikua na kuku kaatamia akaanza kupiga kelele tukamcharanga na majembe na kupasua mayai yake ila baba alivyorudi toka kazini akaishia kupigwa na butwaa tu hatukuchezea kichapo.
2. Nikiwa kwa bibi angu, kuna baba angu mdogo alikuja na coins kibao kwa ajili ya biashara zake akaziweka chumban kwa bibi ambako mie nilikua nalala. Nikawa naiba zile coins nanua mapulizo na watu pale mtaani wakawa wananituma naenda nawachukulia maana nilikua hamna nachoelewa ila kuna siku akanifuma nilichezea bakora za kutosha.
3.nikiwa darasa la kwanza la pili nilikua sipendi shule..nikawa nasumbua sana ila darasani nilikua vzuri coz nilikua sipendi kua kilaza...sasa io siku nilichelewa namba nikagoma kwenda shule mama akanitolea uvivu akanibeba msobe msobe na fimbo mkononi dah nikatupa viatu njiani sweta begi ila mama hakuniacha hadi kwa head teacher wakaitwa vijana wa darasa la saba wakanishika mikono na miguu nikachezea bakora za kutosha dah ila nashukuru mungu nilimalza salama had kufika hapa nilipo
 
Hahaha basi usismile bana

Teh ile idea wengi watakuwa washacopy bana, nitafutie kitu kingine cha uhakika bana


Hahah...kweli ile itakua imeshaibwa

Mfilipino vuta subira niwaze tupate amazing nyingine tena kwa valentine day inabidi iwe ni amazing plus
 
Back
Top Bottom