Kituko cha utotoni ambacho sitakisahau

Yaani nahisi hicho kipaji sina,halafu aligumia kwa maumivu sana ndio kilinifanya nicheke sana
lakini kicheko chako kilimsahaulisha maumivu na kuanza kukutimua
 
Dingi si aliwahi kunidaka na mikanda ya X pornograph darasa la tano kipindi hicho VHS nikala kichapo cha kolabo mama baba na broo na mikanda yote ikavunjwa vunjwa

Balaa sasa yule jamaa niliyemuomba mikanda alinidai karibu mwaka mzima na kila akinidaka nlikua nakula makonzi tu sina pakushtaki
 
Kumbe hiki kioaji chako umeanza nacho tangu utotoni eehh[emoji15]
 
Nikiwa darasa la tatu nilikuwa na kijipu vile vidogo kwenye makalio. Sasa niliogopa kusema maana watu waliokuwa wananizunguka walikiwa wababe nilihisi watanikamua bila huruma, nikauchuna.

Asubuhi naenda shule sijapewa hela nikaamua kuiba, hela za mboga zilikuwa zinakaa juu ya vile vikabati vya zamani vyembamba virefu. Nikapanda stuli nikafikisha mkono kwenye hela bahati mbaya ikasogea mbele kidogo ikabidi nijirefushe zaidi kumbe nimeshaharibu stepu pale kwenye stuli ikateguka!!! Niliporomoka nikatulia tako lile lile lenye jipu, nilipata uchungu flani amaizing kabisa hadi wakubwa wakanikuta hapo na siri zote zikafichuka
 
Mimi nilijipaka utomvu wa majani flani kule kwetu mamndenyi kwenye uume - wakaka wakubwa walitudanganya inaongeza ukubwa wa uume - niliumwaaaaaaaaaaa...lakini ilisaidia nilitahiriwa kabla ya kufikia umri wa kutahiriwa (kwa mila zetu).
 
[emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12]
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Mimi nilijipaka utomvu wa majani flani kule kwetu mamndenyi kwenye uume - wakaka wakubwa walitudanganya inaongeza ukubwa wa uume - niliumwaaaaaaaaaaa...lakini ilisaidia nilitahiriwa kabla ya kufikia umri wa kutahiriwa (kwa mila zetu).

Ila kuna utomvu fulani unafanya hiyo kazi ila uvumilie maumivu na kuwashwa
 
ha ha haha
 
Nilihifadhi uyoga kwenye kabati la nguo, nikasema namuekea baba mpaka akija nimpatie zawadi kwani nilikua nampenda baba yangu mnooo ,na baba alikua anaishi mkoa mwingine na mimi mwingine, ule uyoga uliozea kabatini nililia sana,huwa nikikumbuka nachekaga utoto raha sana
 
Yaaan mpaka leo hata nikimuuliza mwenyewe hajui na mm sijui tatizo lilikuwa nn
 
Hahahahahah
 
Dahh.....
Hii ilinitokea ukubwani aiseeee....
Tukiwa chuo flani Jijini Dar, tulikua tukilala kwa room yetu na usiku tuliamka kujisomea.
Pembeni ya room yetu alikua jamaa na mpenziwake wapo kwa room moja na room mate wengine.
Kumbe jamaa walikua wakianza kufanya mambo yao, hawa too mate wangu walikua wakienda wanapanga viti then wanaanza kula chabo kwa kubadilishana (kwazam).
Sikuhiyo katika kula chabo, jamaa mmoja alianguka kutoka juu viti walivyo vipanga na ule mshtuko ulifanya kelele ambayo ilipelekea jamaa wote kukimbia na kujificha sehem tofauti na room kwetu.
Jamaa mwenye mpenzi alitoka kwa hasira na kuja moja kwa moja room kwetu na alinikuta pekeangu nikiwa najisomea Dahh......[emoji134], jamaa alini maindi sana na aliamini kwamba mimi ndie nilikua nikimla chabo na nika dondoka na kiti.
Kuanzia skuhiyo jamaa alinichukia sanaaaa..... hapo ilikua mwaka 1999.
Cha ajabu nilikuja kuitwa kwenye usahili wa kazi sehemu mwaka 2008, nilimkuta na yeye akiwa kati ya walio ni sahili. Jamaa alini recommend vizuri na nilipata kazi na Hakuwahi kuniuliza tukio lile
 
mbavu sina mumie!!!!!!!!!!!
mie sitasahau nilikuwa mgonjwa nikapelekwa hosp na mama. enzi hizo sindano ni zile za ppf tena zinachemshwa kwenye stove ndo unadungwa, manake zilikuwa za kushea.
sasa nikiwa na maza nilicho fresh japo iliuma balaa afu si unajua vituo vya afya vya msing vilivyokuwa? manake havikuwaga na vitanda vya kuchomea sindano kama siku hizi so unasimama kisha unatupiwa mkuki wako.

kesho yake nikaambiwa niende alone kuchoma sindano manake dozi ilikuwaga ni sindano 5 miaka iyo. nilipofika njian nikajionea tabu si nikautana na rafiki zangu tukaenda kubembea? mbembea zenyewe si hizi za siku izi, kijijini ilikuwa karibu na mto kuna mti, na huo mti umeotea mti wa kutambaa ule ambao huwaga unaota kwa kupata sapoti ya mti mwingine sasa miziz yake ule unaotambaa ndio unaushika kwa mikono miwili unabembea nao. wenzako ndo wanakusukuma. asa mie kule kuumwa, mwili uko weak si nikajishika ili nibembee, ile nasukumwa tu nikenda mara ya kwanza ile narudi mara ya pili nguvu zikaisha nikadondoka kwenye jiwe. Jmani niliumwa acha tu. ikabidi sasa nijipeleke mwenyewe hosp manake nilijua nikifika home maza asingejali mkono umevunjia ama nini ningelemba mboko afu ndo nipelekwe hosp.
 
Nakumbuka kipindi nasoma primary huko,kuna mzeee mmoja alikuwa na mkewe wakafungua sehemu ya kuuza vitafunwa,sasa kama unavyojua sehemu za vijijin,mtu anaungaunga tayari sehemu ya biashara,sas huyu mzee alikuwa biashara yake ni karimati 25,mihogo ya kukaaanga,mashelisheli kipindi hicho,sasa kama hujuavyo wanafunzi likatengenezwa bomu,kwamba tunatinga pale zaid ya 40,harafu c wajua biashara zetu mtu katandaza kwenye meza tu isipokuwa kagawa partition hapa karimati,mbele mihogo,mbele tena ndizi,ikifika saa nne,tunakimbilia kwa huyo mzeeee,aise kinachotokea hapo mzee kupigwa tu,maaana vurugu tupu,huyu anadai chenji,huyu anadai maji huyu hela akutoa adai chenji,huyu katoa shiling 50 maana unapata viwili lakini tokea afike mtu anatafuna baki anasisitizia bado kimoja bado kimoja,kumbe mtu kapiga zaidi ya saba,abadae mzee na mkewe wanalia:O,ni shida
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…