Kitunguu swaumu; Kinga ya saratani, malaria

Kitunguu swaumu kinazuia influenza!






Kitunguu swaumu tangu kale kimekuwa kikijulikana kama 'dawa ya kushangaza' na kutumiwa na watu wengi katika kutibu mafua na influenza. Miongoni mwa faida za kitunguu swaumu ni kuzuia kupatwa na magonjwa mbalimbali na

maambukizo ya virusi. Hivyo kitunguu swaumu hujulikana kama antibiotiki ya asilia. Uchunguzi umeonyesha kwamba kula kitunguu swaumu kunapunguza kushadidi ugonjwa wa influenza na hata kuzuia kupatwa na ugonjwa

huo. Vilevile kula kila mara kitunguu swaumu, huzuia kupatwa na magonjwa ya moyo, kwani kitunguu swaumu huzuia damu isigande kwenye mishipa ya damu.

Halikadhalika kitunguu swaumu ambacho pia ni kiungo muhimu cha chakula kina potassium, na hivyo watu wenye ugonjwa wa shinikizo la damu wanashauriwa kula vyakula vilivyopikwa kwa kitunguu swaumu.

Si vibaya kujua kuwa katika uchunguzi uliochapishwa mwaka 2001, imeelezwa kwamba, kitunguu swaumu kina athari kubwa na nzuri pale kinapochanganywa na baadhi ya dawa nyinginezo katika kutibu Ukimwi au HIV.

Haya shime jamani… kuanzia leo vyakula visikose kuungwa na kitunguu thomu, iwapo unaogopa kupatwa na influenza kama mimi!
 
Nina tatizo la kutopata choo kikubwa kikamilifu.....!!

Naomba msaada
 
Haya ya kitunguu swaumu yananikumbusha lile sakata la mdada aliyekuwa mwanachama humu akatafuna kitunguu swaumu ili apambane na chunusi usoni kwake na kuishia kuharibu mimba yake changa. Alisikitisha sana yule hasa ile kauli yake, "Nilikuwa namhitaji sana huyu kiumbe mtarajiwa azaliwe salama salmini"
 
Samahani kwa kuliingizia hili kwani lipo nje ya maada husika, ila nimefanya hivi ili nipate msaada kwa ukaribu zaidi
Kuna ndugu yangu amepoteza sense( fahamu) kuanzia kiunoni kushuka chini miguuni,miguu yake wala hajapoa ni yamoto kama kawaida
Tatizo lilianza ghafla alipokuwa anatibiwa malaria ghafla alisikia maumivu makali sana ya mgongo hadi kufikia hatua ya kupoteza fahamu,baada ya fahamu kurudi ndio hilo tatizo likaibuka!
Madaktari wengine wanasema huenda kuna budging ya spinal disc ingawa MRI haikuonyesha hivo, wengine walisema huenda kwasababu alikua na tb ya mapafu basi huenda ikawa pia alikuwa na spinal tb.Na mpaka sasa ameshamaliza dozi ya tb lakini hizo sense hazijarudi....
Na ukimgusa mguu unajivuta kama ni yeye anauvuta kumbe unafanya hivo automatically
Naomba msaada wako
 
Me nikitafuna vitunguu swaumu kabla sijalala napata usingizi mzuri sana. Au nikitaka kwenda mazoez lazima nitadune vitungu swaumu huwa natoka jasho sana.
 
hivi vitunguu saumu vya misri vinapatikana wapi kwa hapa dar?
 
Pole zake

Mwanamke mjamzito hatakiwi kula kula tu vitu hovyo
 
Reactions: BAK
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…