Kituo cha sheria na haki waelezea uchaguzi ndani CHADEMA na CCM

Kituo cha sheria na haki waelezea uchaguzi ndani CHADEMA na CCM

Mashamba Makubwa Nalima

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2024
Posts
4,978
Reaction score
2,411
Mkurugenzi Mtendaji Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dkt. Anna Henga amesema Uchaguzi wa ndani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) umefanyika kwa Haki na Uwazi, kinyume na matarajio ya wengi kutokana na mnyukano uliokuwepo mitandaoni kabla ya siku ya Uchaguzi wenyewe na iwe hivyo kwenye Uchaguzi Mkuu.

"Tumefuatilia chaguzi ambazo zilizokuwa zinaendelea kwenye vyama, Chama tawala pamoja na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), nakuona jinsi chaguzi zimeendeshwa, jinsi tulivyoona sisi kama waangalizi wa masuala ya demokrasia nchini. Kwanza kabisa huo utaratibu wa kuchagua ndani ya vyama unatambulika kidemokrasia na chaguzi ndani ya vyama huwa ni ishara ya Uchaguzi mkuu utakuwaje kwahiyo kama ndani kuna amani na uchaguzi mkuu mara nyingi unakuwa na amani."

"Tukianza na uchaguzi wa CHADEMA ambao ndio wa hivi karibuni zaidi, uchaguzi ule ulianza kwa heka heka nyingi za mitandaoni tukasema itakuwa hatari sana huu uchaguzi, wanagombana huyu kamtupia neno huyu ikatia wasiwasi sana watanzania kama utakuwa uchaguzi wa amani lakini kinyume na matarajio ya wengi tumeona kwamba uchaguzi umefanyika kwa amani, umefanyika kwa uwazi na hakuna aliyezulika, hakuna aliyeumia, hakuna vurugu yoyote iliyotokea. Kwenye demokrasia Haki ya kuchagua kwa usalama pia ni haki ya binadamu, ni haki ya kidemokrasia, pia tumependa ambavyo Uchaguzi umekuwa wazi aliyeshindwa ameona kabisa ameshindwa na aliyeshinda ameona kabisa ameshinda, hiyo ni zuri sana tunaweza kujifunza hata kwa uchaguzi mkuu kuwe na uwazi kwasababu demokrasia inataka uwazi"
 
Toka maktaba:
21 January 2025

MKURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk. Anna Henga, amesema kinachoendelea katika Chama ...

1737623649139.jpeg


16 January 2025
Mnyukano CHADEMA waishtua LHRC

1737624261776.jpeg

KURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk. Anna Henga, amesema kinachoendelea katika Chama cha Demokrasia na Maendeelo (CHADEMA), ni ishara tosha kwamba demokrasia bado ina shida nchini.

Amesema tatizo hilo pia haliko kwa chama hicho pekee bali hata Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye baadhi ya uchaguzi wake wa ndani huwa kunaibuka mijadala inayofafania na kinachoendelea CHADEMA.

Alisema hayo jana jijini Dar es Salaam alipozungumza na Nipashe, akieleza kuwa tuhuma za rushwa ndani ya CHADEMA zinaweza kuwa za kweli au zina nia ya kumchafua mtu. Ukweli wake unaweza kuthibitika mahakamani.

"Mchakato wa kidemokrasia hapa nchini una shida, si tu kwa CCM wala CHADEMA, angalau kidogo kwa Chama cha ACT-Wazalendo huwa wanajitahidi kujiepusha na kama huwa yanatokea wana namna ya kudhibiti," alisema Dk. Anna ambaye kitaaluma ni mwanasheria.


Alisema demokrasia nchini bado ni changa na hakuna mipango ya kuifanya ikomae, huku akisisitiza suluhu ya yote hayo ni Katiba mpya.

"Tungeweza kuwa na Katiba mpya ambayo inatoa mwongozo wa kidemokrasia, Tume Huru ya Taifa Uchaguzi (INEC), ingekuwa na mwongozo ambao na wengine wangefuata. Ninadhani ingekuwa suluhu kwa ukuzaji wa demokrasia nchini.

"Ukiona mzazi ana changamoto basi hata watoto lazima watakuwa nayo, pia katika uchaguzi wa CHADEMA, nimeona wanaume wengi wamechaguliwa katika nafasi mbalimbali. Hii inaonesha nafasi ya wanawake ndani ya chama hicho bado ni ndogo," alisema Dk. Anna.

Alishauri kuwe na mabadiliko makubwa ya kisheria ili kuwa na demokrasia katika uchaguzi japo ni ngumu kwa sasa kwa sababu vitu vingi vimo katika Katiba
 
23 January 2025
Dar es Salaam, Tanzania

CHADEMA YAONESHA UKOMAVU WA KIDEMOKRASIA

1737623905319.jpeg

Picha maktaba : Dk. Hellen Kijo-Bisima

Mmoja wa wanaharakati waliopongeza hatua hiyo ni Mkurugenzi Mtendaji mstaafu wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk. Hellen Kijo-Bisima, aliyesema hatua iliyofikia CHADEMA katika uchaguzi huo ni ukomavu wa siasa kwa kuwa umekuwa wa amani. Zaidi ya hayo, amesema mshindi amepatikana na aliyeshindwa amekubali kushindwa na hiyo ndiyo maana halisi ya demokrasia
 
Mkurugenzi Mtendaji Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dkt. Anna Henga amesema Uchaguzi wa ndani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) umefanyika kwa Haki na Uwazi, kinyume na matarajio ya wengi kutokana na mnyukano uliokuwepo mitandaoni kabla ya siku ya Uchaguzi wenyewe na iwe hivyo kwenye Uchaguzi Mkuu.

"Tumefuatilia chaguzi ambazo zilizokuwa zinaendelea kwenye vyama, Chama tawala pamoja na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), nakuona jinsi chaguzi zimeendeshwa, jinsi tulivyoona sisi kama waangalizi wa masuala ya demokrasia nchini. Kwanza kabisa huo utaratibu wa kuchagua ndani ya vyama unatambulika kidemokrasia na chaguzi ndani ya vyama huwa ni ishara ya Uchaguzi mkuu utakuwaje kwahiyo kama ndani kuna amani na uchaguzi mkuu mara nyingi unakuwa na amani."

"Tukianza na uchaguzi wa CHADEMA ambao ndio wa hivi karibuni zaidi, uchaguzi ule ulianza kwa heka heka nyingi za mitandaoni tukasema itakuwa hatari sana huu uchaguzi, wanagombana huyu kamtupia neno huyu ikatia wasiwasi sana watanzania kama utakuwa uchaguzi wa amani lakini kinyume na matarajio ya wengi tumeona kwamba uchaguzi umefanyika kwa amani, umefanyika kwa uwazi na hakuna aliyezulika, hakuna aliyeumia, hakuna vurugu yoyote iliyotokea. Kwenye demokrasia Haki ya kuchagua kwa usalama pia ni haki ya binadamu, ni haki ya kidemokrasia, pia tumependa ambavyo Uchaguzi umekuwa wazi aliyeshindwa ameona kabisa ameshindwa na aliyeshinda ameona kabisa ameshinda, hiyo ni zuri sana tunaweza kujifunza hata kwa uchaguzi mkuu kuwe na uwazi kwasababu demokrasia inataka uwazi"
👏🏻👏🏻
 
Back
Top Bottom