Fantastic Beast
Member
- Feb 18, 2019
- 53
- 539
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar una mambo ya SEBULENI na ya CHUMBANI.
Mojawapo ya mambo ya chumbani ni kwamba Rais wa JMT hawezi akatokea Visiwani moja kwa moja. Na kamwe haitokaa itokee Rais wa SMZ akatokea Bara.
Rais Mwinyi na Samia walipata ngekewa za kuwa Marais wa JMT wakati tu wa VIPINDI VYA MPITO.
Mwinyi aliupata Urais wa JMT wakati Nyerere alipoamua kung'atuka madarakani kwa hiari yake. Kilikuwa na kipindi cha mpito kwani nchi ilikuwa inaondokana na mfumo wa Ujamaa kwenda kwenye Soko Huria.
Rais Samia ameupata Urais kipindi cha mpito baada ya kufariki kwa Hayati JPM. Hakuupata kwenye sanduku la kura, bado tupo kwenye kipindi cha mpito cha nngwe ya mwisho ya JPM.
Hata ikitokea Rais wa JMT akatokea Visiwani, basi huwa inapaswa kuongoza kwa tahadhari kubwa sana kosa dogo tu linaweza kuchochea dhana ya "Uzanzibari" au "Utanganyika".
Kwa nyakati tulizopo sasa, inaonekana wale WAPISHI wa mambo ya CHUMBANI wameanza kutoa mapishi yasiyoiva, wanatoa maboko. Wameshindwa kuhakikisha miiko haivunjwi, wameshindwa kuhakikisha yale ya CHUMBANI hayafiki SEBULENI.
Ikiwa wapishi wa CHUMBANI wataamua kuvunja miiko na kumuweka mgombea wa JMT kutokea Visiwani, basi tunaweza kushuhudia SHIFT OF THE REGIME isiyotarajiwa kwa sababu tu ya uoga wa wapishi wa CHUMBANI.
Mojawapo ya mambo ya chumbani ni kwamba Rais wa JMT hawezi akatokea Visiwani moja kwa moja. Na kamwe haitokaa itokee Rais wa SMZ akatokea Bara.
Rais Mwinyi na Samia walipata ngekewa za kuwa Marais wa JMT wakati tu wa VIPINDI VYA MPITO.
Mwinyi aliupata Urais wa JMT wakati Nyerere alipoamua kung'atuka madarakani kwa hiari yake. Kilikuwa na kipindi cha mpito kwani nchi ilikuwa inaondokana na mfumo wa Ujamaa kwenda kwenye Soko Huria.
Rais Samia ameupata Urais kipindi cha mpito baada ya kufariki kwa Hayati JPM. Hakuupata kwenye sanduku la kura, bado tupo kwenye kipindi cha mpito cha nngwe ya mwisho ya JPM.
Hata ikitokea Rais wa JMT akatokea Visiwani, basi huwa inapaswa kuongoza kwa tahadhari kubwa sana kosa dogo tu linaweza kuchochea dhana ya "Uzanzibari" au "Utanganyika".
Kwa nyakati tulizopo sasa, inaonekana wale WAPISHI wa mambo ya CHUMBANI wameanza kutoa mapishi yasiyoiva, wanatoa maboko. Wameshindwa kuhakikisha miiko haivunjwi, wameshindwa kuhakikisha yale ya CHUMBANI hayafiki SEBULENI.
Ikiwa wapishi wa CHUMBANI wataamua kuvunja miiko na kumuweka mgombea wa JMT kutokea Visiwani, basi tunaweza kushuhudia SHIFT OF THE REGIME isiyotarajiwa kwa sababu tu ya uoga wa wapishi wa CHUMBANI.