Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,307
- 25,932
Katika miaka ya karibuni, Simba SC imekuwa ni klabu ambayo ilikuwa ikiwakilisha taifa letu kwenye michuano ya kimataifa-ngazi ya klabu bingwa Afrika. Pamoja na kuwa rekodi nzuri katika uwanja wa Mkapa hapa Dar inapowakaribisha wapinzani wao wageni, Simba imekuwa ikiliaibisha taifa hili kwa vipigo vya paka mwizi huko ugenini.
Kwa kumbukumbu za miaka ya karibuni Simba walichezea kichapo cha 5-0 na Al Ahly ya Misri; 5-0 na AS Vita Club ya DRC; 4-1 na TP Mazembe ya DRC na 4-0 na Kaizer Chiefs ya Afrika ya Kusini. Simba wafahamu kuwa wanapocheza ugenini wanabeba taswira na heshima ya nchi yetu. Kupigwa mabao mengi ni kuliaibisha taifa.
Hata kama Simba inapata ushindi kwa Mkapa, iache mara moja kutuaibisha ugenini. Tumechoka!
Kwa kumbukumbu za miaka ya karibuni Simba walichezea kichapo cha 5-0 na Al Ahly ya Misri; 5-0 na AS Vita Club ya DRC; 4-1 na TP Mazembe ya DRC na 4-0 na Kaizer Chiefs ya Afrika ya Kusini. Simba wafahamu kuwa wanapocheza ugenini wanabeba taswira na heshima ya nchi yetu. Kupigwa mabao mengi ni kuliaibisha taifa.
Hata kama Simba inapata ushindi kwa Mkapa, iache mara moja kutuaibisha ugenini. Tumechoka!