Smt016
JF-Expert Member
- Jan 11, 2016
- 3,012
- 4,300
Hilo mkuu lipo wazi tu walishasema kabla ya msimu kuanza kwamba lengo la msimu huu ni kuingia top 4 ili waweze kupata nafasi ya kucheza champions league ndipo waingie kwenye kinyang'anyiro cha ushindani wa kusajili wachezaji wenye majina makubwa. Ushawishi ni kucheza champions league + nguvu ya pesa. Kilichowaangusha ac milan kwa miaka yote 10 ni ukata. Berllusconi hakuwa na ela ya kusajili kocha na wachezaji wa maana zaidi ya kuchukua wachezaji wanaopigwa benchi kwenye timu zao na ukizingatia mwaka 2007 karibia robo tatu ya timu walifikia kikomo chao cha kucheza mpira. Kufukuzwa kwa montella ni sahihi sana ila kumpa nafasi Gattuso ni kamari kubwa zaidi wamechezaUwekezaji mkubwa Unahusisha pia ushawishi wa wachezaji kuja hapo San siro hilo ni jambo jema sana sasa ushawishi sio wa pesa tu hata namna club imepanga nini ndani ya muda gani ili wavutike watu kuja hapo