Kiungo PSG akiri kuwa mwanamke

Kiungo PSG akiri kuwa mwanamke

samlaza

Member
Joined
Nov 20, 2014
Posts
9
Reaction score
7
Verratti.jpg

UKISTAAJABU Musa, utayaona ya Filauni! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya kiungo wa kimataifa wa Italia, anayekipiga Paris Saint-Germain (PSG),Marco Verratti kukiri kuwa yeye ni mwanamke.

Hiyo ni kafsha mpya ambayo italisumbua soka la Ufaransa. Kwa mujibu wa mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika jijini hapa hivi karibuni kwenye kambi ya des Loges, Marco Verratti aliweka wazi kuwa yeye ni mwanamke.

Jina lake kamili ni Marta, alitaka kuendelea kuificha siri hiyo akiwa na dhumuni la kutotaka kuhukumiwa kutokana na uwezo wake uwanjani ukilinganisha na jinsi yake:

"Nilitaka kuifisha kwa muda mrefu zaidi kwasababu ni vigumu kwa mwanamke kujihusisha na mambo kiume kama mpira. Ingawaje sikutaka nionekane kituko, zaidi kucheza mashindano ya wanawake,pasipo kumheshimu mtu yeyote. Nina matumaini mashabiki wangu wataendelea kuniona ni Marco na sio Marta,".

"Kwa sasa ninaondoka, si kazi rahisi kwangu,niaminini. Kunyoa nywele na kutojipamba huondoa uhalisia kwa mwanamke. Hivyo si vitu vya kawaida kwa mwanamke kwani wengi hupenda kutamaniwa. "

PSG wamuunga mkono Verratti.

Wachezaji walionywa kwa ufupi kabla ya mkutano huo. Kwa upande wa Zlatan Ibrahimovic, alisema ni mapinduzi ambayo hakuyatarajia:

"Tangu amekuja PSG, Marco hakuwahi kuoga kama wengine wanavyofanya. Nilifikiri labda anaogopa kwakuwa ana uume mdogo. Kisha anakuja kuweka wazi ni mwanamke licha ya mapambano yote mchezoni, nilifikiria tena labda atakuwa amejibadilisha.

Lakini huyo ni mmoja wa wachezaji katika kundi hilo hutokea mara moja, ni kitu kisichowezekana. Pamoja na hayo, Marco Marco ataendelea kubaki nasi.Labda atakuwa mwanamke wa kwanza kutwaa mpira wa dhahabu. "

Verratti ametokea wapi?

Amezaliwa Novemba 5, 1992 mjini Pescara, Italia akijaaliwa kipaji cha kucheza soka hasa kiungo mchezaji. Anasifika zaidi kwa uwezo wake wa kukokota mpira na kutoa pasi za mwisho.

Pia ni kiungo mwenye jicho la mwewe na uwezo wa kupiga mipira mirefu.Kutokana na uchezaji wake huo,amekuwa akifananisha na mkongwe, Andrea Pirlo kutokana na kiwango alichokionesha wakati wa fainali za Kombe la Dunia 2006 kwa kupewa nafasi licha ya umri wake kuwa mdogo.

Maisha ya awali

Alizaliwa mjini Pescara, lakini amekulia L'Aquila,Italia. Akiwa mtoto, alikuwa shabiki wa Juventus na alikuwa akimpenda zaidi Alessandro Del Piero.

Kipaji cha Verratti kilianza kuonekana akwa mdogo, amekuwa akipata ofa kutoka kwa vituo mbalimbali vya michezo Atalanta na Inter Milan, lakini aliamua kujiunga na timu ya Pescara kwa pauni 5,000.

Baada ya kuonesha kiwango cha juu akiwa na timu hiyo hasa ile ya U-16 iliyokuwa ikicheza dhidi ya AC Milan, timu ya Lombardy ilimsajili kwa pauni 300,000.

Wasifu wake

Jina Kamini: Marco Verratti
Kuzaliwa: Novemba 5, 1992 (age 23)
Mahali: Pescara, Italia
Urefu: Meta 1.6
Timu ya sasa: PSG

Timu ya Vijana

2000–2008- Pescara
Timu ya Wakubwa
2008–2012- Pescara
2012– hadi sasa PSG

Timu ya Taifa

2010–2011- Italia U-19
2011–2012- Italia U-20
2012–2013- Italia U-21
2012– hadi sasa Italia


Chanzo: JamboLeo
 
Japo umeandika kwa kiswahili sanifu bado naona mawenge siamini yule fundi ni sista duu......Dah! so? Anataka nini kwa kusema ni wa kike? Mbona hana chuchu???
 
Napata ukakasi. Picha tafadhali niweze kufanya mlinganyisho
 
Tupe chanzo chako cha habari hii tafadhali.
 
Weka picha bwana na sisi tumuangalie kwa jicho la tatu.
 
Mmmh....!
 

Attachments

  • 1431507015812.jpg
    1431507015812.jpg
    9.9 KB · Views: 782
Huyu mleta mada hii una akili au unatafuta kuwa Tia mkenge watu.
Hapo ndio utajua uwezo wa WaTanzania wa kufikiri wataichangia vip hii MADA.haya karibuni
 
Marco Verratti Ni mwanaume, Ana demu wake na wana mtoto mmoja aitwaye Tomasso. Ndio maana taarifa hii ya kizushi hujaiona ESPN, skysport, BBC, CNN na newsmedia nyngne zenye mashiko duniani
 
Marco Verrati
 

Attachments

  • 1431507307811.jpg
    1431507307811.jpg
    8.9 KB · Views: 570
  • 1431507321262.jpg
    1431507321262.jpg
    5.6 KB · Views: 607
  • 1431507335807.jpg
    1431507335807.jpg
    5.9 KB · Views: 606
  • 1431507350464.jpg
    1431507350464.jpg
    7.1 KB · Views: 1,338
  • 1431507360804.jpg
    1431507360804.jpg
    4.2 KB · Views: 1,351
Hahaaa, kweli hiyo ni zaidi ya maajabu.
 
Nimejaribu kumgoogle sijafanikiwa kuyapata hayo ya yeye kuwa "binti".
 
Back
Top Bottom