Kiungulia wakati wa Ujauzito

Kiungulia wakati wa Ujauzito

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Mabadiliko makubwa ya mfumo wa homoni pamoja na kasi ya ukuaji wa mtoto ambayo huleta mgandamizo kwenye tumbo la chakula ni mambo mawili yanayosababisha kutokea kwa tatizo la kiungulia kwa wanawake wajawazito.

77953052-DABC-4484-9F2A-F8A42DAB807D.jpeg


Jambo hili siyo la ajabu, linaweza kutokea kwa mwanamke yeyote.

Ili kuzuia, kukabiliana pamoja na kupunguza changamoto zinazoambatana na tatizo hili, mambo yafuatayo yanashauriwa-
  • Kupunguza ulaji wa vyakula na vinywaji vinavyoongeza uzalishwaji wa asidi tumboni mfano pilipili, energy drinks na vyakula vyenye mafuta mengi.
  • Kutokutumia kabisa pombe na sigara
  • Kuepuka ulaji wa chakula kingi kwa mkupuo mmoja, badala yake kula chakula kidogo kila mara kwa kadri unavyoweza
  • Kunywa maji mengi kila mara
  • Epuka ulaji wa chakula cha usiku muda mchache kabla ya kwenda kulala, unashauriwa kula walau saa 2-3 kabla ya muda sahihi wa kulala
  • Inua kidogo kitanda chako usawa wa kifua kwa kutumia mto au kitu chochote kile ili kuruhusu kifua kuwa juu zaidi kuliko sehemu ya chini ya mwili.
Mara nyingi tatizo hili huwa halihitaji dawa, lakini mtaalamu wa afya anaweza kushauri matumizi ya dawa za kudhibiti uzalishwaji wa asidi tumboni kama vile Omeprazole, Pantoprazole au Compound Magnesium Trisilicate ikiwa ataona kuna sababu za msingi za kufanya hivyo.

Chanzo: STG NEMLIT 2021
 
Mabadiliko makubwa ya mfumo wa homoni pamoja na kasi ya ukuaji wa mtoto ambayo huleta mgandamizo kwenye tumbo ni mambo mawili yanayosababisha kutokea kwa tatizo la kiungulia kwa wanawake wajawazito.

Jambo hili siyo ya ajabu, linaweza kutokea kwa mwanamke yoyote.

Ili kuzuia, kukabiliana pamoja na kupunguza changamoto zinazoambatana na tatizo hili, mambo yafuatayo yanashauriwa-
  • Kupunguza ulaji wa vyakula na vinywaji vinavyoongeza uzalishwaji wa asidi tumboni
  • Kutokutumia kabisa pombe na sigara
  • Kuepuka ulaji wa chakula kingi kwa mkupuo mmoja, badala yake kula chakula kidogo kila mara kwa kadri unavyoweza
  • Kunywa maji mengi kila mara
  • Epuka ulaji wa chakula cha usiku muda mchache kabla ya kwenda kulala, unashauriwa kula walau saa 2-3 kabla ya muda sahihi wa kulala
  • Inua kidogo kitanda chako kwenye usawa wa kifua kwa kutumia mto au kitu chochote kile kuruhusu kifua kuwa juu zaidi kuliko sehemu ya chini ya mwili
Mara nyingi tatizo hili huwa halihitaji dawa, lakini mtaalamu wa afya anaweza kushauri matumizi ya dawa za kudhibiti uzalishwaji wa asidi tumboni kama vile Omeprazole, Pantoprazole au Compound Magnesium Trisilicate ikiwa ataona kuna sababu za msingi za kufanya hivyo.

Chanzo: STG NEMLIT 2021
Dawa ya kiungulia wakati wa ujauzito ni tangawizi imenywe maganda Alf inawekwa mdomoni inamumunywa kama pipi
 
Dawa ya kiungulia wakati wa ujauzito ni tangawizi imenywe maganda Alf inawekwa mdomoni inamumunywa kama pipi

Tena akifanya asubuhi hata morning sickness inasaidia pia
 
Back
Top Bottom