Kiwanda cha biskuti za bangi chagunduliwa Kawe

Kiwanda cha biskuti za bangi chagunduliwa Kawe

Pfizer

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2021
Posts
590
Reaction score
807
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya imekamata kilogramu 423.54 za bangi iliyosindikwa maarufu kama skanka katika operesheni maalum zilizofanyika kwenye mipaka na fukwe za Bahari ya Hindi.

20231108_142030.jpg

Kilogramu 158.54 zilikamatwa eneo la Kigamboni na Kawe jijini Dar es salaam zikiwa zimehifadhiwa ndani ya mabegi ya nguo tayari kwa kusafirishwa, kilogramu 265 zilikamatwa katika matukio tofauti mikoa ya nyanda za juu kusini zikiwa zimefichwa ndani ya magan kwa kuchanganywa na bidhaa nyingine ikiwemo maboksi yenye matunda aina ya apples zikisafirishwa kuelekea jijini Dar es salaam.

Aidha, Mamlaka imekamata watu wanaojihusisha na utengenezaji wa biskuti kwa kuchanganya na skanka katika eneo la Kawe jijini Dar es salaam. Katika tukio hilo, watuhumiwa walikutwa wakiendelea na uzalishaji wa biskuti hizo kwa kutumia mtambo mdogo wa kusaga skanka na vifaa vya kutengeneza biskuti za bangi.
 
Snapinsta.app_400020149_644204371259766_5087984446709835252_n_1080.jpg

WhatsApp Image 2023-11-08 at 15.15.56.jpeg
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (DCEA) imekamata watu wanaojihusisha na shughuli za utengenezaji wa biskuti kwa kuchanganya na bangi aina ya skanka katika eneo la Kawe Jijini Dar es Salaam.

Kamishna Jenerali wa DCEA Aretas James Lyimo amesema watuhumiwa hao wamekutwa wakiendelea na uzalishaji wa biskuti hizo kwa kutumia mtambo mdogo wa kusaga skanka na vifaa vya kutengenezea biskuti hizo za bangi ya skanka.

Kutokana na operersheni hiyo watu 16 wamekamatwa na Kilogramu 423.54 za bangi iliyosindikwa ya skanka yenye kiwango kikubwa cha sumu ya TetraHydroCannabinol THC ambapo asilimia 75 ikizalishwa kutokana na bangi aina ya Sativa na asilimia 45 bangi ya Indica ikiwa na sumu zaidi ya asilimia 45 ikilinganishwa na asilimia 3 hadi 10 zilizo katika bangi ya kawaida.

Chanzo: Clouds TV
 
Hata pombe ilikuwa haramu kama bangi ila ikaruhusiwa miaka ya 1930s

Wazungu wametukuta na vilevi vyetu kwanini tufuate sheria zao za vilevi ?

Pombe na Sigara zinaua watu lakini zinaruhusiwa, bangi haijawai kuua na ni dawa ya kansa kwanini inakatazwa ?
 
M
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (DCEA) imekamata watu wanaojihusisha na shughuli za utengenezaji wa biskuti kwa kuchanganya na bangi aina ya skanka katika eneo la Kawe Jijini Dar es Salaam.

Kamishna Jenerali wa DCEA Aretas James Lyimo amesema watuhumiwa hao wamekutwa wakiendelea na uzalishaji wa biskuti hizo kwa kutumia mtambo mdogo wa kusaga skanka na vifaa vya kutengenezea biskuti hizo za bangi ya skanka.

Kutokana na operersheni hiyo watu 16 wamekamatwa na Kilogramu 423.54 za bangi iliyosindikwa ya skanka yenye kiwango kikubwa cha sumu ya TetraHydroCannabinol THC ambapo asilimia 75 ikizalishwa kutokana na bangi aina ya Sativa na asilimia 45 bangi ya Indica ikiwa na sumu zaidi ya asilimia 45 ikilinganishwa na asilimia 3 hadi 10 zilizo katika bangi ya kawaida.
Mkuu,samahani.
Ikikupendeza tupia ka picha ka aina hiyo ya biskuti ama kasha lake ili iwe rahisi kuzitambua.
Naziweka shukurani zangu kwako hapa chini.
 
Back
Top Bottom