Kiwanda cha magari tanzania

Kiwanda cha magari tanzania

MMhm...Hiyo site yao imefanana na magari wanayounda. Wizi Mtupu! Yaani ni kugawana umaskini...!

Nimekusoma mzee.

Hiyo website yao ka daftari la report ya mtendaji wa kijiji yaani sisi wtz cjui tushalogwa au vp yaani sielewi hata kidogo kwa nini tuko nmna hii,
Yaani kweli hamna hata mtu wa ku update site waweke hata picha za viongozi wanaowatembelea vifaa wanavyo unda au hata kuunga tu hiyo pia itawa saidia kujitangaza hata kuvutia msukumo wa biashara.
Lakini ndo hivo tena.
 
si nlisema mie?. gari baaaaaaaaya!
 
si nlisema mie?. gari baaaaaaaaya!

Aisee kweli.
Yaani mchuma ni mbaya kinyama, anyway ndo huo sasa wataalamu wa dezain habu wapeni wajaribu hata bodi tu waanze. Hata kama kona itakuwa mpaka aloshiba ndo anyonge wasidieni.
 
Tz tungeweka nguvu sehemu chache sasa angalia kuna Nyumbu, TRIDO n.k na wote hawa wanatumia pesa ya kodi!

Kwa nini tusiwe na one Center of Excellence of Industrial Innovation aand Production? Ndo maana quality of output Nyumbu iko chini as we dont prioritise on how we invest in research!

Tunatamani kila kitu wakati mmoja..at the end we achieve nothing!
 
Tatizo letu watanzania ni kutokuwa na uzalendo wa kujenga nchi yetu...mambo yafuatatayo yanaonyesha tuko hivyo
1. Walimu hususani wa shule za msingi na sekondari za serikali kuchelewa kufika kazini na kutoa visingizio mbalimbali... ohoo usafiri mgumu n.k. Pia hawafundushi kwa moyo
2. Wafanyakazi wa idara zote za serikali kudai rushwa au kutengeneza mazingira ya rushwa ndipo kazi ifanyike. mfano upatikanaji wa leseni mbalimbali, matibabu hospitali za serikali, usalama barabarani, vituo vya polisi n.k
3. Wafanyakazi wa maofisini (asilimia kubwa) hawafanyi kazi kwa kujituma... muda mwingi wa kazi (valuable time) huutumia kupiga soga.. na wakati mwingine huingia kwenye mitandao na kufanya surfing. hii ni quality time, mtu yapaswa azalishe. Inakuwa vizuri kama umetimize lengo lako la siku ndio upige domo (kama kuna performance management system) au upoteze muda kwenye surfing
4. Viongozi wote wapo kwa maslahi binafsi na si kwa maslahi ya wananchi wao.Wengi ni wala rushwa, mafisadi na wana uchoyo ulio kithiri. Wakielezwa ukweli wanatoa vitisho. Mfano Chiligati na Mkapa enzi zake.
5.Hatupendi kujishughulisha na kuwa na mbinu mbadala za kujiongezea kipato au kusaidia kuboresha maisha ya wengine. Mfano, toka umemaliza shule (labda university) umewahi ku impart knowledge yako kwa mtu mwingine (academic knowledge)?
6.Tukitoka kazini ni kuendekeza starehe tu, kama vile kwenda club, baa, grocery, uzinzi au kujishughulisha na masuala yasiyo kipaumbele kwa maisha yetu. Eti tumechoka kwa kufanya surfing na kupiga soga!!!! Lol
7.Sio wabunifu at all. mfano, viongozi especially hata Rais anatumia nguvu na ubabe kuwaambia watu wa bandarini waharakishe upakuaji na upakiaji wa makontena ili kuondoa msongamano... Hana solution! hiyo kazi itafanyika vipi? Tatizo pale ni kipato... pay the godamns workers (loaders/offloaders) well. Hakika hautaona kontena pale. Maskini wale ndio the least paid employees!! Ndio maana wanaiba power windows za magari. Kule Holland (Roterdam), wafanyakazi wa Bandari wanalipwa kuliko wa sekta nyingine. Hakuna kulala pale. Hebu Mr. President aende akapate somo pale.. then akienda bandarini ataenda na solution
8. Mkulima analima mazao ya kumtosha kwa miezi minne au mitano tu ya mwaka.. na wakati ana shamba kubwa ameacha majani tu yanaota. Miezi mingine yote anakuwa omba omba. Nimesikia Tanzania tunalima asilimia 1% tu ya arable land...what a shame!

Kwa maisha haya tunayoishi, hakika hatutatoka kwenye umaskini na hatuwezi kuwa wabunifu hata kidogo.

Nyumbu limevumbuliwa toka enzi za marehemu sokoine ... toka kipindi kile hadi leo hakuna version mpya ya magari hayo... at least sasa hivi tungekuwa na sungura basi.
 
Back
Top Bottom