Kiwanda kikubwa cha kuchakata gesi asilia kujengwa Lindi

Kiwanda kikubwa cha kuchakata gesi asilia kujengwa Lindi

Malaika Mkuu

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2014
Posts
902
Reaction score
909
Kampuni kubwa ya Nishati duniani, Shell, imeeleza kuwa imepiga hatua kubwa katika miezi ya karibuni kwenye majadiliano yake na serikali ya Tanzania kufanikisha ujenzi wa kiwanda kikubwa cha kuchakata gesi asilia (LNG) mkoani Lindi.

Hizo ni habari njema kwa Tanzania ambayo licha ya utajiri mkubwa wa nishati hiyo, haijakamilisha mipango ya ujenzi wa kiwanda hicho ambacho kinatarajiwa kugharimu mabilioni ya dola.

Mradi utafungua fursa za kibiashara, kukuza uchumi wa nchi na kutoa maelfu ya ajira kwa miaka mingi.

Afisa mwandamizi wa shell, Wael Sawan amerliza shirika la habari la Reuters kuwa serikali ya Tanzania na kampuni yake wamefika hatua kubwa ndani ya mwaka mmoja kuliko ilivyokuwa awali.

Sheli ina leseni ya kuendesha vitalu viwili (Block 1 na Block 4) vilivyoko bahari ya Hindi. Kwa pamoja vina futi za ujazo trilioni 16 ya gesi asilia inayoweza kuvunwa. Kampuni hiyo inakusudia kuwekeza kwenye mradi huo kwa kushirikiana na aquinor kutoka Norway.

IMG-20220222-WA0030.jpg
 
Serikali ya Dodoma ikifanikiwa katika hili, tutakuwa ni moja ya powerhouse wa gesi asilia Afrika...
 
Afisa mwandamizi wa shell, Wael Sawan amerliza shirika la habari la Reuters
Hizo ni habari njema kwa Tanzania ambayo licha ya utajiri mkubwa wa nishati hiyo, haijakamilisha mipango ya ujenzi wa kiwanda hicho ambacho kinatarajiwa kugharimu mabilioni ya dola.
1645514671013.png

Tulitarajia kumwona Afisa mwandamizi wa shell, Wael Sawan kwenye picha na siyo picha ya huyu, lengo la huu uzi si kutuhabarisha kuna agenda nyuma ya pazia kama ileeeeeeeeeeeeeeee ya Bwana yule aliyetuingiza chaka na gesi yetu miaka ileeeeeeeeee!!!
 
View attachment 2126978
Tulitarajia kumwona Afisa mwandamizi wa shell, Wael Sawan kwenye picha na siyo picha ya huyu, lengo la huu uzi si kutuhabarisha kuna agenda nyuma ya pazia kama ileeeeeeeeeeeeeeee ya Bwana yule aliyetuingiza chaka na gesi yetu miaka ileeeeeeeeee!!!
Wacha Kuzozaaaa
 
Kampuni kubwa ya Nishati duniani, Shell, imeeleza kuwa imepiga hatua kubwa katika miezi ya karibuni kwenye majadiliano yake na serikali ya Tanzania kufanikisha ujenzi wa kiwanda kikubwa cha kuchakata gesi asilia (LNG) mkoani Lindi.

Hizo ni habari njema kwa Tanzania ambayo licha ya utajiri mkubwa wa nishati hiyo, haijakamilisha mipango ya ujenzi wa kiwanda hicho ambacho kinatarajiwa kugharimu mabilioni ya dola.

Mradi utafungua fursa za kibiashara, kukuza uchumi wa nchi na kutoa maelfu ya ajira kwa miaka mingi.

Afisa mwandamizi wa shell, Wael Sawan amerliza shirika la habari la Reuters kuwa serikali ya Tanzania na kampuni yake wamefika hatua kubwa ndani ya mwaka mmoja kuliko ilivyokuwa awali.

Sheli ina leseni ya kuendesha vitalu viwili (Block 1 na Block 4) vilivyoko bahari ya Hindi. Kwa pamoja vina futi za ujazo trilioni 16 ya gesi asilia inayoweza kuvunwa. Kampuni hiyo inakusudia kuwekeza kwenye mradi huo kwa kushirikiana na aquinor kutoka Norway.

Tupe link sio maelezo yako
 
Back
Top Bottom