Ukanda wa SADC na Africa Mashariki umewahi kuwa na watawala nguli sana wa geopolitics na diplomasia mwaka 2015 kurudi nyuma.
Nyerere, Mandela, Thabo Mbeki, Mkapa, Chisano na Kikwete ambaye ni kama alifunga ukurasa huu walikuwa wanaweza hata kuitisha kikao cha pande zinazogombana, zinazopigana au kuzozana watu wakaitikia wito wakazungumza au wakakemea jambo walengwa wakaweka nidhamu kidogo.
Siku hizi ukirejea yanayoendelea Congo DRC ni kama kila mtu ameota sharubu, hakuna mtu mwenye sauti, hakuna anayesikiliza au anayeweza kutoa kauli ikatiliwa maanani.