Kizazi kilichokulia RFA na Kiss FM hakina ushamba kama hiki cha Clouds

Kizazi kilichokulia RFA na Kiss FM hakina ushamba kama hiki cha Clouds

Dance Macabre

Member
Joined
May 6, 2024
Posts
32
Reaction score
61
Enzi za RFA na Kiss FM, unasikiliza VOA, DW na BBC. Walikuwa na propaganda zao, lakini walihabarisha sana Watanzania juu ya dunia. Kijana mdogo anafahamu yanayoendelea huko Mosul, Iraq. RFA wenyewe walikuwa na vipindi vizuri kama Je Wajua. Kiss FM kwenye burudani, unasikiliza American Top 40, Weekend Top 30, n.k. Millenials wa Kitanzania walikuwa na exposure ya kihabari na burudani. Kiss FM na RFA walitufungulia dunia kihalisi.

Pengine zama za redio hizo na mtindo wao wa habari zimepitwa na wakati. Wamekuja hawa Clouds. Habari kubwa ni umbea wa mjini na michezo. Wachambuzi wao wa mambo hamna kitu, ni ujanja ujanja tu wa kuzungumza. Upande wa burudani ndiyo kabisa, utasikia wale wale wabana pua.

Zamani niliamini kuwa kizazi cha mbele kina kuwa na watu werevu na walioelimika kuliko kilichopita, kumbe si kweli. Kumbe inawezekana muda ukaenda mbele, lakini kizazi kikazidi kujaa ujinga na ushamba.
 
RFA 📻 yenyewe imekuwa ya udaku na kamali. Ukiondoa matangazo ya DW, BBC, na VoA vipindi vyote vilivyosalia Ni udaku mtupu. Kazi yao imebaki Ni uchawa Tu kwa ⏱️💯 na kuchezesha kamali wasikilizaji. Walevi ndiyo wanapewa vipindi waviendeshe.
Kuna bahadhi ya viredio vya wilayani vinajitahidi Sana katika kuleta vipindi vilivyojaa hoja kuntu, lakini haya maredio yenye brand Kubwa hamna Kitu kabisa.
 
Clouds fm ina 25yrs how iwe ya hovyo?

au unatak tusikilize wote sauti ya amerikaa ?

Biashara matangazo.....
 
Enzi hizo RFA masafa ya kati AM Redio mkoani inashi saa 7 mchana kujiunga na DW baada ya hapo inakata mpaka jioni wanajiunga na VOA (Mtangazaji mahiri Hadija Riami) baada ya hapo vipindi ni mwendo mdundo asee zamani raha sana.

Baadhi ya vipindi RFA👇🏻
1. Bolingo time (Tontoo Zuber Msabaha)
2. Je huu ni uungwana?
3. Je, Wajua? (Rebeca Muresi)
4. Michezo na RFA (Charles Mobea, Baruan Muhuza)
5. Sitasahau
6. Show Time (Skyworker & Glory Robson)
7. Usiku wa Mahaba
8. Lugha Gongana (Jumaa Ahmed Baragaza)

Endelea na wewe sasa😁😁😁

Watuma Salam maarufu kipindi hicho

1. Muhiri Obaleeeee
2. Lawena Nsonda Baba mzazi - mzee wa Makongorosi Chunya
3. Jumanne Sebarua Tingisha

Nk

Watoto wa 2000 hamtaelewa
 
Enzi za RFA na Kiss FM unasikiliza VOA, DW na BBC. Walikuwa na propaganda zao lakini walihabarisha sana watanzania juu ya dunia. Kijana mdogo anafahamu yanayoendelea huko Mosul Iraq RFA wenyewe walikuwa na vipindi vizuri kama je wajua. Kiss kwenye burudani unasikiliza American top 40, weekeend top 30 nk nk. Millenials wa kitanzania walikuwa wana exposure ya kihabari na burudani. Kiss FM na RFA walitufungulia dunia kihalisi

Pengine zama za redio hizo na mtindo wao wa habari ukapita. Wamekuja hawa clouds.Habari kubwa ni umbea wa mjini na michezo. Wachambuzi wao wa mambo hamna kitu, ni ujanja ujanja tu wa kuzungumza. Upande wa burudani ndiyo kabisa, utasikia wale wale wabana pua.

Zamani niliamini kuwa kizazi cha mbele kina kuwa na watu werevu na walioelimika kuliko kilichopita, kumbe si kweli. Kumbe inawezekana muda ukaenda mbele lakini kizazi kikazidi kujaa ujinga na ushamba.
Fact
 
Clouds media wamefanikiwa kukipotosha kizazi cha Gen-Z kuamini kua kupata taarifa za wasanii maarufu inatosha. Hizo international newz wawaachue wazee.
Kabisa. Imewaaminisha kuwa kuwajua wasanii na watu maarufu na masuala yao ndiyo ujanja. Ni kama magazeti ya Shigongo ila kwa audio.
 
Mwaka jana nilibahatika kupata kalikizo kafupi so muda mwingi nilikuwa nakaa nyumbani tu.

Nikasema ngoja nifanye kautafiti binafsi contents za vipindi vya radio hapa nchini.

Almost 85 wameigana, asubuhi ni magazeti na sports, inakuja discussion mbali mbali za mambo ya mitaani, muziki halafu michezo tena halafu usiku mzima muziki.

Katika wiki nzima ya research yangu nilikutana na kipindi kimoja tu katika radio ambacho kilikuwa very educative, kilihusu kampuni flani inayotoa huduma za kukutanisha wateja na house girls, kilikuwa kizuri sana.

Kwa ufupi utaona kwamba, radio nyingi hazina vipindi vina vyoelimisha vingi ni burudani na michezo tu, na udaku.

Tunatengeneza jamii ya watu wasio jielewa.
 
Mwaka jana nilibahatika kupata kalikizo kafupi so muda mwingi nilikuwa nakaa nyumbani tu.

Nikasema ngoja nifanye kautafiti binafsi contents za vipindi vya radio hapa nchini.

Almost 85 wameigana, asubuhi ni magazeti na sports, inakuja discussion mbali mbali za mambo ya mitaani, muziki halafu michezo tena halafu usiku mzima muziki.

Katika wiki nzima ya research yangu nilikutana na kipindi kimoja tu katika radio ambacho kilikuwa very educative, kilihusu kampuni flani inayotoa huduma za kukutanisha wateja na house girls, kilikuwa kizuri sana.

Kwa ufupi utaona kwamba, radio nyingi hazina vipindi vina vyoelimisha vingi ni burudani na michezo tu, na udaku.

Tunatengeneza jamii ya watu wasio jielewa.
Hiyo kampuni usikute ni ya Joyce kiria 😂😂
 
Enzi za RFA na Kiss FM unasikiliza VOA, DW na BBC. Walikuwa na propaganda zao lakini walihabarisha sana watanzania juu ya dunia. Kijana mdogo anafahamu yanayoendelea huko Mosul Iraq RFA wenyewe walikuwa na vipindi vizuri kama je wajua. Kiss kwenye burudani unasikiliza American top 40, weekeend top 30 nk nk. Millenials wa kitanzania walikuwa wana exposure ya kihabari na burudani. Kiss FM na RFA walitufungulia dunia kihalisi

Pengine zama za redio hizo na mtindo wao wa habari ukapita. Wamekuja hawa clouds.Habari kubwa ni umbea wa mjini na michezo. Wachambuzi wao wa mambo hamna kitu, ni ujanja ujanja tu wa kuzungumza. Upande wa burudani ndiyo kabisa, utasikia wale wale wabana pua.

Zamani niliamini kuwa kizazi cha mbele kina kuwa na watu werevu na walioelimika kuliko kilichopita, kumbe si kweli. Kumbe inawezekana muda ukaenda mbele lakini kizazi kikazidi kujaa ujinga na ushamba.
personal sana hii
 
Back
Top Bottom