KKKT : Maaskofu hatujagawanyika kuhusu Katiba

KKKT : Maaskofu hatujagawanyika kuhusu Katiba

Na serikali ni nani? Mbona serikali inasema Katiba ni nzuri na watu wapige kura ya Ndiyo?

Tumia kichwa chako kifikiri na siyo kufugia nywele!

Wewe ndio tumia akili yako, serikali inaongozwa na mwenyekiti wa CCM. CCM ndio iliyopewa ridhaa ya kuongoza nchi na kuunda serikali. Kwani maaskofu wameteuliwa au kupewa mamlaka yao na chama gani cha siasa?
 
kwa hiyo serikali na maccm wanavyozungumzia mambo ya mahakama ya kadhi kwani yenyewe ni madhehebu ya dini?

Kwahiyo tunajadili mahakama ya kadhi? Labda nikusaidie kitu huenda povu litakupungua. Mimi ni mwana CCM na Muislamu kabisa. Ila nitapiga kura ya hapana kukataa katiba pendekezwa kwasababu sioni kama inawakilisha mawazo yangu. Pia sikubaliani na serikali kujihusisha na masuala ya mahakama ya kadhi.
 
Kardinali Pengo alisema hivi;

Hawana nguvu za kumjibu Kardinali Pengo na wanachofanya ni kuzunguka mbuyu na kutafuta easy target!

Mkuu unaonekana uwezo wako Wa kutafakari mambo Mdogo sana. Pengo sio kiongozi Wa TEC. Yeye ni mjumbe tu,hana mamlaka ya kuwasemea wakatoriki Tanzania. Na yeye aliagizwa walaka usomwe jimboni kwake hadi ngazi ya jumuiya na ameshatekeleza parokia zote. Kama ulisoma shule ni Mara kumi usingesoma Kabisa ikajulikana.
 
Wewe ndio tumia akili yako, serikali inaongozwa na mwenyekiti wa CCM. CCM ndio iliyopewa ridhaa ya kuongoza nchi na kuunda serikali. Kwani maaskofu wameteuliwa au kupewa mamlaka yao na chama gani cha siasa?

Kumbe nabishana na mtu asiyejitambua...

Utabaki kupiga makitaimu ta hapa lakini Tamko la Maaskofu limeshatolewa na sasa kila mwanajumuiya analo.

Kila mikutano ya wanajumuiya sasa msisitizo ni kutii mamlaka ya Kanisa ya Kura ya Hapana kwa Katiba Haramu ya Chenge na Mafisadi.
 
CCM ikiangalia vibaya itajikuta inahifadhi kundi dogo la maghaidi lililojikusanyizia mali na kujipa nguvu ya kidola paspipo wao kujua au wakijua lakini wakakosa nguvu ya kujisafisha.

Hivi inawezekanaje ccm ithubutu kwenda kinyume na matakwa ya watanzania waliowengi ktk katiba wataikayo...katiba inayoonesha maadili ya uongozi! Aliyeyaloga haya magamba.....
 
We Mwenezi kwani Pengo ndiye Rais wa Tec? Mambo ya katoliki kabla ya 'kuvuvuzela' ni bora ukajiridhisha kwanza kwa Kikwete au Membe! Na kama huna aibu waweza kujiuliza kwa aliyekuwa katibu wa CCM tawi la Vatican Dr Slaa, 'babu' kama unavyopenda kumkejeli, UTAELIMISHWA na Upagani wa India utakutoka.
 
Askofu Benson Bagonza wa KKKT Dayosisi ya Karagwe amepinga vikali kauli ya serikali kwamba maaskofu wamegawanyika kuhusu Kura ya Hapana kwenye Katiba Mpya.

Askofu Bagonza ambaye ni mjumbe wa CCT ameonya kauli ya Samwel Sitta kwamba Serikali haitarudi nyuma kuhusu katiba mpya.

Askofu Bagonza ambaye ana msimamo thabiti amesema wapo maaskofu wa mfukoni wanaoandaliwa na Serikali ambao wanatumika kujibu hoja mbalimbali za kanisa.

Akizungumzia Kauli ya Kadinali Pengo kupingana na maaskofu wenzake, Askofu Bagonza amesema huo ni msimamo binafsi wa Kadinali Pengo na siyo msimamo wa Kanisa Katoliki nchini.

Askofu Bagonza amesema msimamo wa Kanisa Katoliki nchini unatolewa na TEC ambalo ni Baraza la Maaskofu Katoliki nchini.

Askofu Bagonza amesisitiza kwamba pamoja na msimamo binafsi wa Kadinali Pengo lakini ameruhusu Tamko la Maaskofu kusomwa katika Makanisa yote ya Jimbo lake la DSM.

Askofu Bagonza ameishangaa serikali kusema Kanisa halina haki ya kuwataka waumini kupiga kura ya Hapana.

Askofu Bagonza amesema.." Kama CCM na serikali yake wanawashawishi watu wapige kura ya Ndiyo, Ukawa wamewaeleza watu wao wasusie,iweje iwe tatizo kwa Jukwaa la Wakristo kuwaeleza wafuasi wao wapige kura ya Hapana?"...alihoji.
======================



Chanzo:
Mwananchi
Kamanda Greenwhich hawa ndio wazalendo tunaowataka kwenye nchi hii
 
Muislam yeyote angetoa kauli kama hiii, ungeskia mengine saa hii, defender kama 120 na askari FFU kama 70 hivi na wajeda kadhaa mlangoni kwa mtoa kauli, hii ni iwapo tu Muislam 1 angetoa kauli kama ya huyu kiongozi wa kanisa lenye wafuasi wengi zaidi duniani kusema waumini wapige kura ya hapana????
 
Hii katiba itapita tuuu, ni watanzania wachache sana wanaoweza kutumia uhuru wao vizuri. Mnacheza na magamba nini, yani wakubali muwang'oe madarakani halafu kodi zenu atakula nani ebo??? . Kuwang'oa ccm ni ndoto jamani hadi yesu arudi, kama mnabisha endeleeni tuu but huo ndo ukweli.
 
Pengo ana mamlaka kwa jimbo lake tu na si majimbo mengine. Msemaji wa TEC ni rais wake. Kura ni hapana

Catholic means universal hivyo kinachokubaliwa kinatekelezwa na wote. Hivyo hata katika jimbo lake bado yeye si supreme. TEC ndio inayotoa tamko wa ajiri ya wakatoliki wote nchini. Nafikiri Cardinal Pengo hawezi kupinga tamko la TEC kama askofu maana tamko linaunganisha maaskofu wote japo anaweza kuwa na maoni yake yeye kama Pengo na si kama Askofu wa Dar es Salaam
 
Pengo ana mamlaka kwa jimbo lake tu na si majimbo mengine. Msemaji wa TEC ni rais wake. Kura ni hapana

Watu wengin hawaelewi.Pengo ni Asofu wa jimbo la Dar e Salaam kama walivyo maaskofu wengine kutoka majimbo megine kama skofu wa jimbo la Ruvuma au Mbeya n.k.So hana mamlaka ya kuwasemea wakristu au wakatoliki.
Nikama ambavyo Mkuu wa mkoa wa Dar e Salaam ambavyo hana mamlaka katika mkoa wa Tabora au Dodoma.
Kuna vyombo vyenye mamlaka ya kusema on bealf of Wakristo ua Wakatoliki naPengo yuko chini ya hivyo vyombo na vikitoa simamo ni msimamo waumini wao.
 
Muislam yeyote angetoa kauli kama hiii, ungeskia mengine saa hii, defender kama 120 na askari FFU kama 70 hivi na wajeda kadhaa mlangoni kwa mtoa kauli, hii ni iwapo tu Muislam 1 angetoa kauli kama ya huyu kiongozi wa kanisa lenye wafuasi wengi zaidi duniani kusema waumini wapige kura ya hapana????

Ingekuwa vyema waislam nao wahamasishwe ili waikatae katiba pendekezwa ya nyoka wa makengeza na mwenzake six kwa kuwa imeandaliwa kulinda mafisadi zaidi
 
Back
Top Bottom