Klabu Bingwa Barani Afrika: ASEC Mimosas yatangulia robo fainali

Klabu Bingwa Barani Afrika: ASEC Mimosas yatangulia robo fainali

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,307
Reaction score
25,932
Kufuatia ushindi wao wa 3-0 dhidi ya Galaxy hivi punde na kimahesabu, ASEC Mimosas wametinga hatua ya robo fainali ya Klabu Bingwa barani Afrika.

Hadi sasa, ASEC wamefikisha alama 10 huku ikibaki michezo miwili. Simba wana alama 5, Galaxy alama 4 na Wydad alama 3.

Kimahesabu, Simba au Galaxy tu ndio wanaoweza kufika alama 10 au zaidi huku wakiwa na mechi moja baina yao. Wydad kama atashinda michezo yake iliyobakia atakomea alama 9.

Hata kama ASEC watapoteza michezo yao miwili iliyobakia bado watakuwa wameshafuzu kwakuwa wanaoweza kuwafikia ni Simba au Galaxy tu.

Kongole ASEC Mimosas, mabingwa wa Ivory Coast!
 
Tungempata kocha wao tungekula bingo
Hapo kauza mastaa majuzi tu
 
ASec mimosa Goal difference yao pia nzuri sana

Simba na hata Jwaneng galaxy ngumu sana kumfikia Asec goal difference yake.

Point 10 kwa Asec na uwiano wake wa magoli ni umeshamvusha kwenda robo fainali
 
ASec mimosa Goal difference yao pia nzuri sana

Simba na hata Jwaneng galaxy ngumu sana kumfikia Asec goal difference yake.

Point 10 kwa Asec na uwiano wake wa magoli ni umeshamvusha kwenda robo fainali
Hakika. Halafu, Simba na Galaxy wana mechi yao.
 
Kufuatia ushindi wao wa 3-0 dhidi ya Galaxy hivi punde na kimahesabu, ASEC Mimosas wametinga hatua ya robo fainali ya Klabu Bingwa barani Afrika.

Hadi sasa, ASEC wamefikisha alama 10 huku ikibaki michezo miwili. Simba wana alama 5, Galaxy alama 4 na Wydad alama 3.

Kimahesabu, Simba au Galaxy tu ndio wanaoweza kufika alama 10 au zaidi huku wakiwa na mechi moja baina yao. Wydad kama atashinda michezo yake iliyobakia atakomea alama 9.

Hata kama ASEC watapoteza michezo yao miwili iliyobakia bado watakuwa wameshafuzu kwakuwa wanaoweza kuwafikia ni Simba au Galaxy tu.

Kongole ASEC Mimosas, mabingwa wa Ivory Coast!
ASEC ,akifungwa mechi zote mbili zilizobakia itakuwaje
 
Back
Top Bottom