Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,307
- 25,932
Mabingwa watetezi wa Klabu Bingwa barani Afrika, Esperance ya Tunisia na Wydad Casablanca ya Morocco wametinga fainali ya michuano tajwa baada ya kupata suluhu kwenye mechi zao za leo zilizoisha hivi punde ugenini.
Esperance ilipambana na TP Mazembe ya DR Congo huku Wydad Casablanca ikipepetana na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini. Katika michezo ya awali, Esperance walishinda 1-0 huku Wydad wakiibuka na ushindi wa 2-1.
Wote leo, wakiwa ugenini wamepata matokeo ya 0-0 yaliyowavusha kuwapeleka fainali. Esperance wapo kwenye nafasi ya kutetea kombe la michuano hiyo ambalo msimu uliopita walilitwaa wakiwabwaga Al Alhy ya Misri.
Esperance ilipambana na TP Mazembe ya DR Congo huku Wydad Casablanca ikipepetana na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini. Katika michezo ya awali, Esperance walishinda 1-0 huku Wydad wakiibuka na ushindi wa 2-1.
Wote leo, wakiwa ugenini wamepata matokeo ya 0-0 yaliyowavusha kuwapeleka fainali. Esperance wapo kwenye nafasi ya kutetea kombe la michuano hiyo ambalo msimu uliopita walilitwaa wakiwabwaga Al Alhy ya Misri.