Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Mmiliki wa klabu ya African Lyon, Rahim Zamunda Kangezi, anapambana kuihamisha timu hiyo kutoka Dar es salaam kwenda mkoa mwingine kwa sababu ya kukosa mashabiki wa kuiunga mkono katika jiji la Dar es salaam.
"Huwezi kuwa na timu Yatima, aliyeanzisha timu alikosea, umewahi kusikia timu haina mashabiki? Sio rahisi kuendesha timu bila mashabiki ndo maana tunataka tuhame Dar es salaam".
"Tutabadilisha Jina, na kuna mikoa mitatu tunaongea nayo ikiwemo Kilimanjaro, lakini tutaona ni mkoa gani halafu tunahamia moja kwa moja hatuendi kwa michezo ya ligi, tukiondoka haturudi tena, tunataka tuwe na mji wetu, Dar ni pagumu sana Simba na Yanga wameshachukua mji".
"Siwakimbii Simba na Yanga lakini inabidi ujue maana ya 'African Lyon' African ni Yanga Afrika na Lyon ni Simba, kwahivyo walikuwa wanataka tuwaunganishie mashabiki tukae katikati lakini mpango huo haukufanikiwa". Amesema Rahim
"Huwezi kuwa na timu Yatima, aliyeanzisha timu alikosea, umewahi kusikia timu haina mashabiki? Sio rahisi kuendesha timu bila mashabiki ndo maana tunataka tuhame Dar es salaam".
"Tutabadilisha Jina, na kuna mikoa mitatu tunaongea nayo ikiwemo Kilimanjaro, lakini tutaona ni mkoa gani halafu tunahamia moja kwa moja hatuendi kwa michezo ya ligi, tukiondoka haturudi tena, tunataka tuwe na mji wetu, Dar ni pagumu sana Simba na Yanga wameshachukua mji".
"Siwakimbii Simba na Yanga lakini inabidi ujue maana ya 'African Lyon' African ni Yanga Afrika na Lyon ni Simba, kwahivyo walikuwa wanataka tuwaunganishie mashabiki tukae katikati lakini mpango huo haukufanikiwa". Amesema Rahim