Klabu ya Matiyasi FC ya Afrika Kusini yafungiwa maisha kwa kushinda goli 59 katika mechi moja

Klabu ya Matiyasi FC ya Afrika Kusini yafungiwa maisha kwa kushinda goli 59 katika mechi moja

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1654156893154.png

Picha: Kikosi cha Wachezaji wa Matiyasi FC

Klabu moja yenye maskani yake Limpopo katika kitengo cha chini cha mfumo wa soka nchini Afrika Kusini imefungiwa maisha baada ya kufunga mabao 59 katika mechi moja.

Timu ya Matiyasi FC iliyokuwa ikiwania kupanda Ligi ya Mkoa wa ABC Motsepe, iliichapa Nsami Mighty Birds kwa mabao 59-1, huku mabao arobaini na moja kati ya hayo yalikuwa ya kujifunga.

Inaelezwa pia kuwa Mchezaji ambaye alirekodiwa kupewa kadi nyekundu katika kipindi cha kwanza pia alirekodiwa kufunga bao katika kipindi cha pili.

Ofisi ya kanda ya SAFA huko Limpopo iliita klabu zote mbili kwenye kikao cha Kamati ya Nidhamu mnamo tarehe 25 Mei 2022 huko Giyani.

Timu hizo zilishtakiwa na kupatikana na hatia ya rushwa na kukiuka sheria za chama.

Katika hukumu hiyo, klabu hizo zimefungiwa kabisa kujihusisha na masuala ya soka huku viongozi wanaohusishwa na timu zote mbili pia wakipewa adhabu ya kufungiwa miaka mitano ndani ya mkoa huo.

Katika mechi nyingine ya ligi hiyo hiyo, Shivulani Dangerous Tigers iliilaza Kototo Happy Boys 33-1 tarehe sawa. Mabao saba ya kujifunga yalirekodiwa.

👀 Afrika

===
A Limpopo-based club in the lower division of the South African football system has been banned for life after scoring fifty-nine goals in one match.

Matiyasi FC, who were vying for promotion to the Provincial ABC Motsepe League, beat Nsami Mighty Birds 59-1, with forty-one of the goals scored as own-goals.

A player who was recorded to have been given a red card in the first half was also recorded to have scored a goal in the second half.

The incident occurred last week and the South African Football Association (SAFA) has swiftly reacted.

According to FarPost.co.za, SAFA’s regional office in Limpopo summoned both clubs to a Disciplinary Committee hearing on 25 May 2022 in Giyani.

The teams were charged and found guilty of corruption and contravening the association’s statutes.

In the verdict, the clubs have been permanently banned from all football activities while the officials implicated from both teams have also been given a five-year suspension within the region.

In another match from the same league, Shivulani Dangerous Tigers beat Kototo Happy Boys 33-1 on the same date. Seven own goals were recorded.

The teams were also found guilty of contravening the SAFA rules and were handed a life-ban from all football activities.

Source: Soccer24
 
😆😆😆😆😆
 
South mbali sana hiyo staili mbona kama wameiga Zenji japo wao huko wamekomeshea kabisa!

Kuna ile video ilizunguka mtandaoni kipa huko Zenji akiuruka mpira ikawa goli sijui la 20!
 
Back
Top Bottom