Klabu ya Simba imeingia mkataba wa miaka miwili na kampuni ya MobiAd

Klabu ya Simba imeingia mkataba wa miaka miwili na kampuni ya MobiAd

Izy_Name

JF-Expert Member
Joined
Apr 9, 2020
Posts
772
Reaction score
1,733
Klabu ya Simba imeingia mkataba wa miaka miwili na kampuni ya MobiAd kwa ajili ya kusaidia ukuzaji wa maendeleo ya soka la Vijana huku Mkataba huo ukiwa na Thamani ya 500M huku kukiwa na nafasi ya kuboresha zaidi.

“Soka la vijana ni muhimu sana. Ili uwe na timu ya vijana iliyo bora lazima iwezeshwe. Kama ilivyo kwa wachezaji wengine kama Mohamed Hussein kutoka kwa timu ya vijana.”

“Simba inakwenda mbele kutambua vipaji, kuvichukua na kuviendeleza na kuweza kutengeneza timu yenye vipaji vikubwa sana. Tunaamini Simba imara yenye vipaji haitaisaidia Simba pekee bali hata taifa letu.”
“Yawezekana wachezaji tunaowaona ni sababu ya bahati, lakini tunatengeneza mfumo ambao kila kijana mwenye kipaji tutamwezesha kukuza kipaji chake, lakini sio tu kuendeleza kipaji cha mpira lakini pia kusoma shule.”

“Leo tupo kwenye historia nyingine ya kuendeleza soka la vijana Tanzania. Mfumo wetu utakuwa mfumo wa wazi na endelevu.”

“Namshukuru meneja wa timu Patrick [Rweyemamu] sababu ametumika sana kujenga vijana ambao tunawaona leo wakifanya vizuri.”

Mtendaji Mkuu wa Simba sc Imani Kajula.

337106150_3485029798445911_943571226090208606_n.jpg
“Tumeona hii ni fursa kuungana kwenye hii safari. Tunatangaza udhamini kwa timu ya vijana ya Simba Sports Club kwa mkataba wenye thamani ya Tsh. 500 milioni kwa miaka miwili.”

“Tunaamini mpira wa miguu ni sehemu ya suluhisho la ajira kwa vijana. Simba ni timu kubwa Afrika na inazidi kuwa kubwa hivyo ni vizuri kuandaa vijana ambao watachukua nafasi ya hawa wa sasa.”

CEO wa MobiAd Africa, Rumisho Shikonyi

photo_2023-03-23_11-45-16.jpg
“Jambo hili lina neema kubwa. Niwashukuru MobiAd kwa kukubali kudhamini timu yetu ya vijana. Kama Simba SC tunawaahidi kwamba fedha hizi zitatumika vizuri kwani vijana ndio msingi wa timu yetu.”

“Tuna malengo ya kuboresha soka la vijana, shamba ambalo tunajua litatusaidia kuvuna vipaji kwa ajili ya timu ya wakubwa. Ndugu Dewji amekubali kusaidia kuendeleza soka la vijana. Hivi karibuni tutaanza ujenzi wa kituo chetu."

Mwenyekiti wa Bodi Simba sc Salim Abdallah “Try again”
Mdhamini mpya wa @simbayouthtz MobiAd Africa atakaa kifuani mwa jezi ambazo timu hiyo ya vijana itakuwa inatumia kwa kuwa ndiyo mdhamini mkuu wa klabu hiyo kwa timu za vijana.
 
Jezi ime jaa mta weka nembo yake ndan ya jezi au makolo fc [emoji81][emoji81]
 
Klabu ya Simba imeingia mkataba wa miaka miwili na kampuni ya MobiAd kwa ajili ya kusaidia ukuzaji wa maendeleo ya soka la Vijana huku Mkataba huo ukiwa na Thamani ya 500M huku kukiwa na nafasi ya kuboresha zaidi.
“Soka la vijana ni muhimu sana. Ili uwe na timu ya vijana iliyo bora lazima iwezeshwe. Kama ilivyo kwa wachezaji wengine

Wivu tu
 
Makolo na soka la vijana wapi na wapi, hiyo timu ya wakubwa tu imejaa wazee watupu msimu ujao watacheza na mikongoja
 
Upande ule pia utaiga hongera sana Simba timu inayoongoza njia ili wengine wafuate, Simba baba wa soka la Tanzania
 
Habari njema. Niliwahi kutoa ushauri wa Simba fufueni timu yenu ya vijana.

Ila huo udhamini mbona kama ni mdogo sana kwa miaka 2? Serikali pia ingetoa motisha kwa timu za ligi kuu zinazoanzisha academy zao.

Hata wangetoa milioni 200 kwa kila timu, itasaidia maana mwisho wa siku hao wachezaji wataenda kulisaidia taifa. Hiyo pesa inaenda kurudi mara dufu wachezaji wakifanikiwa.
 
Habari njema. Niliwahi kutoa ushauri wa Simba fufueni timu yenu ya vijana.

Ila huo udhamini mbona kama ni mdogo sana kwa miaka 2? Serikali pia ingetoa motisha kwa timu za ligi kuu zinazoanzisha academy zao. Hata wangetoa milioni 200 kwa kila timu, itasaidia maana mwisho wa siku hao wachezaji wataenda kulisaidia taifa. Hiyo pesa inaenda kurudi mara dufu wachezaji wakifanikiwa.
Umendika point muhimu sana. Ni kama serikali inasibiri matokeo bila kupanda mbegu. Tazama timu hizi zinafanya vizuri kimataifa lakini zimejaa wachezaji wageni.

Serikali ina wajibu wa kutumia fursa ya uwepo wa wageni kuongeza nguvu kwa timu za vijana ili wajifunze kwa hao wageni.

Serikali haina mitigation strategy yeyote kwenye risk ya wingi wa wageni Simba na Yanga. Fikiria ukitoa hao wageni Simba na Yanga zitabaki na nini.
 
Umendika point muhimu sana. Ni kama serikali inasibiri matokeo bila kupanda mbegu. Tazama timu hizi zinafanya vizuri kimataifa lakini zimejaa wachezaji wageni. Serikali ina wajibu wa kutumia fursa ya uwepo wa wageni kuongeza nguvu kwa timu za vijana ili wajifunze kwa hao wageni.

Serikali haina mitigation strategy yeyote kwenye risk ya wingi wa wageni Simba na Yanga. Fikiria ukitoa hao wageni Simba na Yanga zitabaki na nini.
Wamelala sana. Tumefuata njia ya EPL katika kukuza thamani ya vilabu vyetu na ligi yetu ila tunaenda kuiua timu ya taifa kama bado ilikuwa haijafa.

Tunasahau hao EPL at least wana academies, wanawalipa mastar wazawa sawa au wakati mwingine zaidi ya wageni. Sisi hatufanyi hayo.
 
Mbona sijaona sehemu yoyote ile wakimshukuru rais mama Samia au hata kumtaja tu???
 
Habari njema. Niliwahi kutoa ushauri wa Simba fufueni timu yenu ya vijana.

Ila huo udhamini mbona kama ni mdogo sana kwa miaka 2? Serikali pia ingetoa motisha kwa timu za ligi kuu zinazoanzisha academy zao. Hata wangetoa milioni 200 kwa kila timu, itasaidia maana mwisho wa siku hao wachezaji wataenda kulisaidia taifa. Hiyo pesa inaenda kurudi mara dufu wachezaji wakifanikiwa.
Yaan serikali iweke pesa?
Timu zijiendeshe zenyewe
 
Yaan serikali iweke pesa?
Timu zijiendeshe zenyewe
Support kwa maana ni jambo linalokuja kufanikisha uchumi na ajira kwa vijana ukiachilia faida zingine.

Milioni 500 ki ukweli ni pesa ndogo sana kwa mradi wa namna hii, labda wanaenda kutafuta wadhamini zaidi ila kwa kuwa huyu ndiye main sponsor ina maana wengine watakuwa wanatoa pesa ndogo zaidi ya hiyo.
 
Udhamini ndio hela zenyewe, ukitaka jezi iwe plain sawa tu, wenzio wanaingiza hesabu
Usimsikilize huyo. Jezi zimeonyeshwa, kilichobadilika sehemu ya M-Bet ndiyo wamechukua wao.
 
Back
Top Bottom