Klabu ya Simba imetangaza kumsajili mshambuliaji Moses Phiri

Dilunga na Mkude wabaki, waondoke mhilu,gadiel na mwanuke (atolewe mkopo). Bila kumsahau mzee Wawa nae aondoke
 
Kwa maoni yangu wachezaji hawa wapewe mkono wa kwaheri:

Wakigeni;
Wawa
Bwalya
Kagere
Mugalu
Lwanga
Morisson (Tayari kaondoka)

Wazawa;
Gadiel
Nyoni
Mhilu

Wafuatao watolewe kwa mkopo;
Mwanuke na
Banda.

Kulingana na tetesi za usajili, wachezaji 6 wakigeni wanaofaa ni;

1. Mosses Phiri (Zanaco-Zambia)[emoji3514]
2. Morlaye Sylla (Horoya-Guinea)
3. Augustine Okra (Bechem-Ghana)
4. Cesor Manzoki (Vipers-Uganda)
5. Fasika(Cape Town City) au Frederic (Chippa)
6. Udoh (Nigeria) au Diarra (Mmali huyu anacheza Zambia).
7. Aongezwe mwingine wa kuchukua nafasi ya Banda (au Banda anaweza kubaki).

Wazawa watatu tu wanatosha kuziba nafasi za Gadiel, Nyoni na Mhilu
 
SIMBA kuna wachezaji walimaliza na magoili zaidi ya matatu ila hapo kwenye list uchwara sijawaona, labda ndiomaana hata Phiri hayupo.
Ungeanza kwa kuingia kwenye hiyo source uangalie. ESPN ni source uchwara? Mwenye magoli matatu ni nani huyo?
 
Tz ianze utaratibu wa kuweka dau na mishahara inayotumika
Mimi pia huwa sioni maana ya kuweka usiri katika hili swala, huko ulaya mbona mambo yapo wazi tu na hata hapa Afrika kwenye nchi zilizoendelea kimpira kama Misri, Morocco, SA, Algeria huwa hawana mambo ya kuficha.
 
Sasa hapo si mnabadilisha timu nzima! Na hao wachezaji wapya mnawatoa wapi? Hela za kuvunja mikataba ya baadhi ya hawa wachezaji mnatoa wapi?

Acheni utani bhana.
 
Sasa hapo si mnabadilisha timu nzima! Na hao wachezaji wapya mnawatoa wapi? Hela za kuvunja mikataba ya baadhi ya hawa wachezaji mnatoa wapi?

Acheni utani bhana.
Unavyoongea utafikiri nyinyi mlishawahi kufanya usajili wa kuvunja mikataba ya wachezaji, wale wa Congo wa As Vita, Chiko na wengine mlivunja mikataba?
 
Sasa hapo si mnabadilisha timu nzima! Na hao wachezaji wapya mnawatoa wapi? Hela za kuvunja mikataba ya baadhi ya hawa wachezaji mnatoa wapi?

Acheni utani bhana.
Hoja ya kitoto kabisa hii, ambapo inafahamika wazi kuwa asilimia kubwa ya wachezaji hasa wa Kimataifa mikataba yao imekwisha.

Na wazawa hakuna ambaye Simba watashindwa kufikia nao mwafaka kama si kumtoa kwa mkopo.
 
Hoja ya kitoto kabisa hii, ambapo inafahamika wazi kuwa asilimia kubwa ya wachezaji hasa wa Kimataifa mikataba yao imekwisha.

Na wazawa hakuna ambaye Simba watashindwa kufikia nao mwafaka kama si kumtoa kwa mkopo.
Wewe umemuelewa ila Mac Alpho hakumuelewa.
 
Mkuu hii ni ESPN au maan nimcheki playstore inaonyesha muonekano tofauti kabisa
 
Hoja ya kitoto kabisa hii, ambapo inafahamika wazi kuwa asilimia kubwa ya wachezaji hasa wa Kimataifa mikataba yao imekwisha.

Na wazawa hakuna ambaye Simba watashindwa kufikia nao mwafaka kama si kumtoa kwa mkopo.
Sawa. Ila tusiwasikie tena msimu ujao mkilia lia humu kwa sababu ya kuwa na kikosi chenye wachezaji wengi wapya na wasio na uwezo mkubwa wa kuwaletea matokeo chanya uwanjani.
 
Kuna watu hapa huwa sijui wanautazamaje mpira. Mtu anakomaa kabisa eti Dilunga na Jimson Mwanuke waondoke Simba. Hivi "work rate" ya Dilunga uwanjani ya kukaba na kushambulia kutokea pembeni huyo Peter Banda anaingia hata nusu yake kweli? Au watu wanapenda tu zile baiskeli ambazo hazina faida kwa timu. Dilunga asubiriwe tu apone apewe muda acheze ndipo aangaliwe kama majeraha yameathiri kiwango chake kwa kiasi kikubwa ndio aachwe wakati wa dirisha dogo. Jimson ameonyesha kabisa kile kilichowashinda vijana wengi wanaposajiliwa na hizi timu kubwa mbili kuwa huwa wanapotea kabisa lakini yeye ametumia vizuri sana mechi chache alizopewa kucheza licha ya kuchezeshwa nafasi tofauti tofauti na alizozizoea uwanjani.

Watu hawajui tu sababu kubwa mojawapo ya Simba kuyumba mwaka huu pamoja na usajili mbovu lakini pia kukosekana ile "work rate" ya Miquisone kumeiyumbisha sana timu uwanjani. Na Simba inapaswa iwe makini sana wakati huu wa usajili kwani pamoja na kusajili wachezaji wenye vipaji lakini lazima wachezaji hao wawe na "work rate" kubwa uwanjani. Wawe wapambanaji haswa uwanjani kwa dakika zote tisini. Sio mchezaji baada ya dakika ya 30 tu anapotea anaanza kutembea uwanjani na akinyangánywa mpira basi anasubiria wenzake wakabe.

Kwangu mimi nikiambiwa nitaje wachezaji kumi wenye vipaji vikubwa uwanjani kwenye ligi yetu lazima Morison na Bwalya wawe ndani kati ya hao kumi kwa sababu wana vipaji kweli kweli. Lakini vipaji vyao na uwezo wao kama haviisadii timu kupata matokeo inakuwa havina faida kwa timu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…