Koboko (Black Mamba) - Nyoka hatari zaidi duniani

Koboko (Black Mamba) - Nyoka hatari zaidi duniani

Mkuu ukiumwa na Koboko usikimbie wala ku-move sababu circulation ya blood kadri inavyozidi ndiyo sumu inavyosambaa mwilini, so ukiumwa na ukatulia same place unaweza kufikisha walau 2 to 3 hours kabla hujafa.

Lakini jibu alilonipa Babu lilikuwa ni moja tu " Ni mwiko kuondoka eneo ambalo umeumwa na koboko" bila kutoa maelezo zaidi.
Sasa mkuu si atakugonga mara nyingi sana ukibaki hapo
 
Hapo yupo uvunguni
Na baadae kukamatwa na mtaalamu wa majoka
20180512_123143.jpeg
20180512_123219.jpeg
 
Koboko moja kati ya nyoka mbabe na mwenye hasira za hali ya juu, nyoka uyu anaweza kukimbia kwa 12mile/hour na kusimama urefu wa futi 4 kwenda juu.
Ni nyoka anaeweza kukung’ata zaidi ya mara moja kama ataona ajakung’ata vizuri.
Ni nyoka mwenye meno marefu (0.8”) most dangerous specie.
 
Katika ulimwengu wa Nyoka kuna mambo ya kushangaza sana,kuna wakati Cobra alioekana akimmeza Koboko mdogo huko Msumbiji,na Kuna Koboko mkubwa aliyeuwawa na wanajeshi huko Botswana alipopasuliwa tumboni walikuta ame mmeza Cobra mkubwa sana.
 
Wataalam tusaidieni huduma ya kwanza ni ipi unaoumwa na nyoka
Kuna Nyoka wa aina nyingi sana,kuna wengine wanang'ata bila kudunga sumu,kuna wenye mild venom,kuna dry bite, na kuna wengine sumu yao ni inaitwa two steps to death..guess what huyo ndio Koboko.
 
Cape file snake ndie nyoka ambaye hauwawi na sumu ya nyoka yeyote hata ya Koboko,na huwa anawala koboko wadogo,alipo nyoka huyu ambaye hana sumu Koboko hukimbia.
 
Kuna snake island huko Brazil ni the most dangerous Island in the world
Yaani kila unapokanyaga ni nyoka.
Ni marufuku kufika eneo hilo ila jeshi tu hapo utajua heshima ya Sniper hahahaha
Ngoja na mimi nikatembelee huko kama watanipa kibali wajeda wa UK
 
Huko nyumbani kuna kijiji kinaitwa Koboko kutokana na huyo nyoka.. Kila mara lazima usikie mazishi, chanzo ni koboko.. Nilikuaga nasikia stori zake tuu, ila sikumtilia maanani..

Siku hiyo natoka sehemu fulani nikakatiza kwenye hicho kijiji ili nitokee kijiji chetu, kuna kanjia kanakatiza msituni na mto.. Sina hili wala lile, narusha mikono huku na kule natembea kwa raha zangu..

Hamadi!! Mita kama 4-5 toka nilipokuwepo nikamuona koboko rangi ya kijivu na weusi katanda njiani.. Alivyoniona akatulia kwanza, akanicheki huku akijiinua taratibu huku ulimi wake ukiwa unacheza cheza na domo lake leusi..

Aiseee, jasho lilitoka kama mvua, vinyoleo vyote vilisisimka nikaona mwisho wa maisha ndio leo..
Tukawa tunaangalia, sikupepesa hata jicho wala kusogeza kiungo chochote, nae akawa katulia tuu ananiangalia..

Nikaanza kusali sala ya Baba yetu moyoni na sala ya toba juu.. Tulikaa hivo kama dakika 5-10, nikaona huyo anaanza kujisogeza mdogo mdogo na kuingia machakani..

Nilitulia pale hadi akapotelea huko msituni, nikamwongezea dakika zingine ili afike mbali.. Nilichomoka hiyo spidi, breki ya kwanza kitandani na usingizi juu.. Haikuisha hata mwezi nikasikia kuna mtu tayari kashakobokolewa..
Mungu mkubwa aisee, ndo wanasema unatakiwa ufanye hivyo ukimuona
 
Mjomba sio chumvi ni kweli kabisaa koboko hata uwee na silaha moto na mpo wengi wote mnakula doziiii hata muende maji ya kuwasha,mabomu ya machozi, risasi za moto mapambano yake si ya kitoto.

Kuna uzii nautafutaa waziri nyalandu akiwa waziri wa maliasili alituma kikosi maalumu cha kupambana na koboko vita yake ilikuwa sio mchezoo huo uzi ulishawahi kuwekwa humu ngoja nitauweka kuna watu walikuwa wanatoa ushuhuda kuhusu mapambano yake
huu hapa. Nyalandu alikua anachekesha
Nyalandu atuma kikosi kazi kumaliza nyoka wa Koboko Urambo
 
Niliwahi kutembelea Meserani snake park huko Arusha, sikuwa na idea na baadhi ya nyoka, je huyu mdudu anapatikana pale? Na pia kuna snake park moja pale Mapinga Bagamoyo ningependa kujua kama wapo ili nifanye utalii wa ndani tena
 
Back
Top Bottom