Koboko (Black Mamba) - Nyoka hatari zaidi duniani

Nipo chunya huku wako wengi ni nyoka hatari sana wanaweza kuua ng'ombe mia kwa dakika chache tu!..
 
Hivi koboko kwanini watu hawamtajitaji hovyo ni kwa namna alivyo na sumu kali, na kwa hapa Tanzania wapo maeneo gani hasa
Huu ni moto wa kuotea mbali
Nakumbuka wakati Marehemu Samuel Sita aliomba watumwe kikosi kazi wakawasake hawa viumbe Urambo lakini walitahadharishwa wakaambiwa wanakwepa shaba hao na wana mbio za 12miles/h
Ilibidi waombwe na wanakijiji wasaidie lakini wapi walikuwa wameishaua wanne

Ni kiumbe hatari kuwahi kuishi na wanapatikana maeneo mengi East and southern Africa
Wanatajwa sana kwa hilo jina mimi sijawahi kuambiwa usimtaje
 
Nyoka wengi hua wana aibu na huwa wa kwanza kuretreat unless wawe cornered, koboko hajui kuretreat, ana accuracy, speed na bado yeye ndiyo ataanzisha ugomvi.

Iwe iwavyo ninachojua hachomoki mbele ya honey badger.
 
Koboko ni Black Mamba... Huyu nyoka akiingia darasani akiwakuta wanafunzi dakika tano wamekauka..
Tofauti ya simba na chui ukikutana nao ukipiga kelele wanakimbia...
Koboko ukim provoke imekula kwako...
Wafugaji wakisikia pori lina koboko wana hama..
 
Mzembe sana mkuu yani huyo nyoka usipo mkanyaga akugongi ng’ooo
Unamkosea heshima.

Puff ader ametoka kuzaliwa sasa hivi na sasa hivi akikung'ata ujue ndiyo safari hiyo.

Ana camouflage nzuri sana inayomsaidia mawindoni, huko kutulia unakokusema ni sehemu ya mbinu za akiwa mawindoni.

Force anayotoka nayo ili kushambulia windo inatosha kuua windo hata bila kutumia sumu.
 
Puff ader mzembe?
Ni kweli kifutu ni mvivu anatumia rangi yake kutulia mahali hata kama utamsogelea ndio maana anauma watu wengi sana
Wengine wakisikia unakuja wanakimbia lakini huyu unaweza kukaa karibu yake bila yeye kuondoka ila akiona ni tishio anatumia silaha yake hapo yanakuwa mengine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…